EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, November 28, 2012

King Majuto amlilia Sharo Milionea.

KIFO cha msanii Hussein Ramadhan ‘Sharo Milionea’ kimemshutua msanii mwenzake King Majuto hadi akaanguka na kupata shinikizo la damu.

Majuto alipatwa na hali hiyo baada ya kupata taarifa za msiba huo na hadi anazungumza na gazeti hili, ingawa alikuwa na nafuu, mwili wake ulikuwa umevimba.
Akizungumza na Mwananchi Majuto alisema: “Kimeniuma sana kifo cha mwanangu Sharo.
“Nimeshirikiana naye kwa mambo mengi, nilifahamiana naye tangu mwaka 2009 tulikutana pale Vijana Production, na tangu nimefahamiana naye, kuna mambo mengi sana tumefanya,” alisema Majuto ambaye mara baada ya kupata taarifa ya kifo cha msanii huyo alipata na shinikizo la damu.

“Nilimuongoza kwenye mambo mengi na siku zote nilikuwa nikimsihi asikimbilie kuoa kama walivyo vijana wengine ambao wakipata hela kidogo wanachokimbilia ni kuoa.
“Nilikuwa ninamwambia jenga maisha yako kwanza, hakikisha unakuwa na nyumba, gari na miradi, ili hata ukioa mtoto asipate shida nashukuru alinisikiliza alianza kupata mafanikio kifo ndo kimemchukua.

“Sijui nisemeje kifo kina siri nzito, ningejua anakufa lini ningekata rufaa na hata kutoa rushwa lakini hiyo ni siri ya Mungu pekee...alikuwa ameanza kupata mafanikio masikini, sijui ni macho mabaya ya watu, sijui Mungu pekee ndio anajua kwa sababu alikopatia ajali wala hakukuwa na kona kali.

“Alikuwa meneja wangu, matangazo yote mnayoyaona yeye ndio alikuwa akiingia mikataba yote na fedha zote, hakuwa mdhulumishi, kazi zote tulizofanya pamoja na yeye ndio alikuwa akisimamia, akiniambia mzee tusifanye hii kazi nami sifanyi.

“Alikuwa ana msimamo wake, akisema Sh1milioni ni hiyo hiyo habadiliki tofauti na mimi na roho ya huruma, nikimtajia mtu bei akiniomba basi napunguza, sifanyi hivyo kwa njaa, hapana, ila ni ile imani niliyonayo sasa tofauti na Sharo.

“Sidhani kama pengo lake kwangu litazibika na sijui kazi zangu nitazifanyaje tena bila yeye, alikuwa ni kila kitu kwangu pamoja na kumzidi umri.”
Mwenyekiti Simba
Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage alitoa pole kwa wadau wa filamu na kumuelezea marehemu Sharo Milionea kuwa hakuwa msanii wa kawaida kwani ni miongoni mwa kizazi kipya cha vijana wa Kitanzania walioamua kutafuta maisha kwa kutumia vipaji walivyopewa na Mungu.

Yeye alijitumbukiza zaidi katika uchekeshaji na baadaye akaonyesha uwezo mkubwa katika fani ya muziki.
Maisha ya Sharo Milionea
Kila kona za miji na vitongoji vyake nchini, huwezi kukosa kusikia watoto wakisema ‘umebugi meen...nataka kula meen’ na yote hiyo ni staili na ubunifu wa msanii huyo.

Sharo Milionea aliyejizolea umaarufu kwa staili yake ya utembeaji na uongeaji, na aliwateka mashabiki wa vichekesho hususani vijana na watoto kutokana na kubuni staili yake ya kuiga madoido ya watu wa Marekani, na kujiweka katika maisha ya juu ambayo kwa hakika hawezi kuyafikia.

Ingawa aliigiza maisha hayo yeye binafsi hakupenda kabisa staili hiyo ya maisha na lengo la kuigiza ni kuwafundisha wenye tabia kama hizo kuacha, kwani binadamu wote ni sawa na hakuna aliyebora kuliko mwingine.

Alizaliwa Septemba 12, 1987 Muheza, Tanga. Alijiunga na Shule ya Msingi Lusanga na baadaye akasoma Sekondari ya Kwabutu, Tanga.
Alipomaliza shule mwaka 2005, alihamia jijini Dar es Salaam kumfuata mama yake aliyekuwa akiishi jijini kwa muda mrefu.CHANZO CHA HABARI GAZETI LA MWANANCHI.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate