EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, December 15, 2012

Apendekeza wabunge kuchapwa viboko.

MKAZI wa Kata ya Makuburi Wilaya ya Kinondoni, Pendo Mlyauke (35) jana alipendekeza adhabu ya viboko isiishie shuleni tu bali ifike hadi bungeni. Alisema kuwa kutokana na kukithiri kwa vitendo vya utovu wa nidhamu bungeni, Katiba Mpya haina budi kuja na sheria itakayo ruhusu adhabu ya viboko kwa wabunge wasio na maadili.
Pendo aliyasema hayo wakati akiwasilisha maoni yake ya kuundwa kwa Katiba Mpya mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Alisema kuwa kitendo cha wabunge kuwa huru bila utendaji wao kufuatiliwa na kuhojiwa ndiyo sababu inayochangia wengi wao kukosa nidhamu wawapo bungeni.
“Siku hizi Bunge limekuwa kama uwanja wa malumbano. Utawakuta wanasema na kujibizana ovyo ovyo, wengine wanalala muda wote wakati Bunge linaendelea, napendekeza kuwepo adhabu ya viboko kwa wabunge wa aina hiyo kwani wanayoyafanya ni kinyume cha maadili,” alisema Pendo.

Aliongeza kuwa kama nchi za Rwanda na Burundi wabunge wasiokuwa na maadili wanaadhibiwa, inakuwaje hapa nchini wanaachwa huru. Alisema kuwa ili kukomesha utovu huu wa nidhamu kwa wabunge, Katiba Mpya inapaswa kutoa adhabu kali ya viboko visivyopungua 4 na adhabu hiyo akapendekeza itolewe na wanajeshi.

Kuhusu wanafunzi, alisema kuwa hivi sasa kuna tatizo kubwa la nidhamu kwa wanafunzi shuleni kutokana na adhabu ya viboko kuondolewa. Alipendekeza adhabu hiyo irudishwe mashuleni na ikiwezekana kila mwalimu awe na uwezo wa kuchapa kama ilivyo zamani.

Naye Thomas Muhahate (63) alipendekeza kuwa maneno yanayosemeka katika Katiba iliyopo kuwa kila mtu na haki ya kumiliki mali yana upungufu, hivyo akapendekeza kwenye Katiba Mpya neno halali liongezwe. Alisema kwamba kama Katiba ikiendelea kuweka mwanya huu, matokeo yake ni kuongeza kundi la mafisadi wa mali za umma ambao mali walizonazo siyo halali.

“Mali za Watanzania zinahujumiwa kila siku, hii inatokana na Katiba iliyopo kusema kuwa kila mtu ana haki ya kumiliki mali. Mimi nasema Katiba Mpya itamke kuwa kila Mtanzania awe na haki ya kumiliki mali halali, ili mafisadi waweze kuhojiwa kama mali walizonazo ni halali na watoe uthibitisho,” alisema Muhahate.
Aliongeza kuwa vitendo vya ufisadi hapa nchini vimechangiwa na Azimio la Zanzibar lililofuta Azimio la Arusha. Alisema kuwa kufutwa kwa Azimio la Arusha kumechangia kuporomoka kwa maadili ya viongozi wa umma na matokeo yake wengi wamekuwa wakwapuaji wa mali za umma.

“Kumekuwa na wimbi la majumba kujengwa kama uyoga kila mahali. Haya ni matokeo ya ufisadi. Mbaya zaidi ni kwamba hakuna sheria ya kuwabana au kuwauliza wamepata wapi pesa za kujenga majumba hayo. Napendekeza Azimio la Arusha lirudishwe ili kujenga upya maadili ya viongozi wa umma na jamii,” alisema Muhahate.CHANZO NI MWANANCHI.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate