ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), 
Barnabas 
  Mtokambali, amekemea vitendo vya baadhi ya wanaume wanaovaa suruali 
chini ya makalio, akisema wanaofanya hivyo ni sawa na mashoga.
Alisema mwanamume kuvalia suruali chini ya makalio ni sawa na 
kujitangazia biashara ya ushoga ya kufanya mapenzi ya jinsia moja.
Mtokambali alitoa kauli hiyo juzi wakati akizindua Chuo cha Ualimu cha
 Mount Sinai kilichopo Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
  Alisema kama ilivyokuwa kwa machangudoa ambao huvaa nusu uchi kuonesha
 kuwa wapo katika biashara, ndivyo hivyo kwa mashoga nao wanavaa ili 
kujitambulisha.
Kutokana na kukithiri kwa vitendo hivyo, aliwaasa wanafunzi wa chuo 
hicho kuvaa kwa kuzingatia maadili ili wawe walimu bora kwa taifa na 
mfano wa kuigwa.
  Makamu Mkuu wa chuo hicho, Alexander Chuwa, alisema  licha ya chuo 
hicho kutoa mafunzo ya ualimu, pia kinatoa mafunzo ya elimu ya biashara 
na malengo ya baadaye ni kuwa chuo kikuu.
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment