EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, February 24, 2013

Mama Kikwete akabidhi msaada wa vifaa vya tiba Rufiji, Pwani

Picture
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania,mara baada ya makabidhiano ya msaada wa vifaa vya tiba na dawa wenye thamani ya shilingi Mil 20 kutoka Vodacom Foundation kwa ajili ya wakazi wa eneo Nyamisati iliyopo wilaya Rufiji Mkoa wa Pwani.
Rufiji-Pwani -- Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, mama Salma Kikwete, amekabidhi msaada wa vifaa vya tiba na dawa wenye thamani ya shilingi Mil 20, kwenye Kituo cha Afya cha Nyamsati, mkoani Pwani, uliotolewana Mfuko wa Huduma za Jamii wa Vodacom Tanzania(Vodacom Foundation) Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo, katika Kituo cha Afya cha Nyamsati mkoani hapa, ambapo pamoja na mambo mengine, mama Kikwete ameishukuru Vodacom Foundation kwa msaada huo, nakutoa rai kwa wadau wengine kujitokeza na kuunganisha Nguvu katika kukabiliana na matatizo ya kijamii, hasa eneo la afya ya mama na mtoto.

"Idadi ya vifo vya mama na mtoto, mapambano dhidi ya Malaria na UKIMWI, chanjo kwa watoto ikiwemo ya ugonjwa wa Nimonia, mimba kwawanafunzi wa kike pamoja na kuwawezesha wajasiriamaliwa kike ni mambo muhimu ambayo jamii inapaswa kuyatazama kama changamoto na kuangalia namna ya kukabiliana nayo," amesema.

Mama Kikwete amesema upungufu wadawa na vifaa tiba kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali nchini bado ni changamoto, na kwamba msaada uliotolewa utasaidia kuunga mkono jitihada za Serikali zenye lengo la kuleta ustawi wa huduma za  Afya kwa manufaa ya watu wa Nyamsati na mkoa wa Pwani kwa ujumla.

Akipokea msaada huo, Mganga Mkuu wa Zahanati ya Nyamsati wilaya ya rufiji mkoa wa pwani Bw.Haruna Mhina alisema Kituo hicho cha afya  ambacho kinahudumia wastani ya wagonjwa 2000 kwa mwezi kinakabiliwa na changamoto kubwa ya upungufu wa madawa na vifaa tiba lakini kupitia msaada huo, kwa kiasi kikubwa utasaidia kutatua ukubwa watatizo hilo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mfuko wa Kusaidia Jamii wa Vodacom,Bw. Yessaya Mwakifulefule, amesema kuwa mfuko huo siku zote umekuwa mstari wa mbele kushirikiana na taasisi na vituo kadhaa vya afya nchini katika kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta ya afya nchini kupitia misaada mbalimbali wanayoitoa.

"Azma ya Vodacom nikuhakikisha tunaifikia jamii na kushirikiana nayo katika kukabiliana na changamoto zinazoizunguka kwenye maeneo yote,hususani afya na elimu, na tutaendelea kuisaidia Nyamsati kadiri itakavyowezekana ili kuleta ustawi mzuri kwa afya ya watu wake," amesema Mwakifulefule.
Picture
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA,Mama Salma Kikwete(katikati) pamoja na Mganga Mkuu wa Zahanati ya Nyamisati, iliyopo wilaya Rufiji Mkoa wa Pwani Bw.Haruna Mhina,wakipokea msaada wa vifaa vya tiba na dawa wenye thamani ya shilingi Mil 20 kutoka kwa Mkuu wa Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate