JUSTIN
BIEBER ‘ametoka’ na Rihanna, limeandika jarida la kila wiki la Life
& Style, ambalo limedai kuwa jambo hilo ndiyo sababu ya kweli nyuma
ya kuachana na mpenzi wake Selena Gomez.

Kwa
mujibu wa jarida hilo, Gomez alimpiga chini Bieber Desemba mwaka jana
baada ya kusikia habari za kushtua kwamba ‘amemchukua’ Rihanna.
Aliyeitwa
‘rafiki’ wa wenza hao wa zamani, amelieleza jarida hilo kuwa, “Justin
‘alifanya yake’ na Rihanna Februari mwaka juzi –wakati huo akiwa na
miaka 16, huku tayari alikuwa amezama kwenye mapenzi na Selena.
Chanzo
hicho kilisema kuwa, Bieber mwenye umri sawa na mdogo wa Rihanna,
hakumweleza yeyote jambo hilo kwasababu lingemfanya aonekane kama ‘mbwa
mchafu’.”
Kiliendelea
kupasha kwamba ‘shoo’ hiyo ilifanyika nyumbani kwa Rihanna Los Angeles
ama kwenye chumba cha hoteli ya Four Seasons, Beverly Hills, ambako
Bieber anapendelea kukaa.
Chanzo
kingine cha jarida hilo kilisema Bieber na Rihanna waliendeleza
‘kupeana raha’ wakati wa” walipokuwa wanachukua picha za viedo za
Victoria’s Secret Fashion Show mwezi November.
Life
& Style imetonywa kuwa, “Wakati wa mapumziko, walikwenda Hotel
Giraffe. Walikuwa peke yao — walinzi wao walihakikisha hili. Mfanyakazi
wa hoteli alizuia floo nzima kwaajili yao.”
Via www.saluti5.com
No comments:
Post a Comment