EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 7, 2013

SAMATTA MATAWI YA JUU:Tanzania 1- 0 Cameroon



MBWANA Samatta, mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania anayecheza soka la kulipwa katika klabu ya TP Mazembe ya Lubumbashi, DR Congo, alitumia vizuri pasi iliyotoka kwa Frank Domayo na kuukwamisha mpira wavuni dakika ya 90.
Bao hilo lilitokana na makosa ya kipa wa Cameroon, Komguep aliyeruka juu kutaka kuokoa mpira huo, lakini ukatua miguuni mwa Samatta na kuusindikiza wavuni.

Katika mchezo, Taifa Stars walianza kwa kasi na kulishambulia lango la Cameroon, dakika ya nne walifanikiwa kulifikia lango la wapinzani wao, lakini walishindwa kujipatia bao la haraka.
Ndani ya dakika saba ya kipindi cha kwanza, mshambuliaji wa kimataifa wa Taifa Stars, Mbwana Samatta, alichezewa vibaya mara tatu.
Wakicheza kwa kuonana vizuri, Frank Domayo na Abubakari ‘Sure Boy’, waliweza kuwasumbua viungo wa Cameroon dakika ya 12, huku kipa Juma Kaseja akiwa mapumziko.
Cameroon walipata nafasi nzuri ya bao, kufuatia mpira wa kona, lakini beki kisiki wa Stars, Kelvin Yondan aliondoa hatari hiyo langoni kwao.
Dakika ya 14, Kaseja alipata maumivu kidogo  baada ya kuangukiwa na mshambuliaji wa Cameroon, Tchami Herve, lakini baada ya kutibiwa aliendelea kukaa langoni.
Cameroon walifanya shambulizi la nguvu dakika ya 24, lakini shuti kali la Tchami lilitoka nje kidogo ya lango la Stars, huku Kaseja akiwa amesimama bila ya kujaribu kuufuata mpira.
Mashambulizi ya Stars yalifanikiwa kuwachanga mabeki wa Cameroon na kuzaa penalti baada ya beki mmoja wa timu hiyo kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari na mwamuzi Munyemana Hundu kutoka Rwanda kupuliza filimbi ya adhabu hiyo.
Beki wa Stars, Erasto Nyoni, alikosa penalti hiyo baada ya kipa wa Cameroon, Effala Komguep, kuudaka mpira huo.
Stars walikianza kipindi cha pili kwa kuliandama lango la wapinzani wao, ambapo dakika ya 49, lakini krosi ya Nyoni ilitoka nje ya lango.
Stars wakicheza soka safi na kuwafanya Cameroon, washindwe kumfikia kipa Juma Kaseja, kwa muda wa dakika 29, wakati dakika ya 78, Thomas Ulimwengu alishindwa kuunganisha vizuri kwa kichwa mpira wa krosi uliopigwa na Mbwana Samatta.
Kwa ushindi huo, Stars itakuwa inajitengenezea nafasi kubwa ya kuombwa mechi za kirafiki na nchi nyingine zilizo bora katika soka barani Afrika.
Mwanzoni mwa mwaka huu, Stars ilifanikiwa kuwachapa mabingwa wa Mataifa ya Afrika mwaka jana, Zambia ‘Chipolopolo’, bao 1-0, bao lililofungwa na Mrisho Ngassa.
Matokeo hayo ndiyo yaliyowavutia Cameroon, mpaka wakaomba kucheza mechi ya kirafiki na Stars, hivyo baada ya kipigo cha leo, itakuwa imepanua wigo zaidi wa mataifa mengine kuomba mechi ya kirafiki.
Stars: Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Kelvin Yondan, Aggrey Morris, Salum Abubakari ‘Sure Boy’, Mrisho Ngassa, Frank Domayo, Mbwana Samatta, Mwinyi Kazimoto/Thomas Ulimwengu, Amri Kiemba.
Cameroon: Effala Komguep, Assout Ekotto, Aminou Bouba, Ngoula Patrick, Nyom Allan, Pierre Wome, Kiunge Mpondo, Benino Henry, Tchami Herve/Elounu, Olinga Fabrice, Aboubakar Vincent.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate