EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 4, 2013

Upinzani Syria wafanikiwa Munich

Activist preacher Moaz al-Khatib attends the General Assembly of the Syrian National Council in Doha November 11, 2012. al-Khatib was elected as the first leader of a new Syrian opposition umbrella group that hopes to win international recognition and prepare for a post-Assad Syria, in a poll counted before reporters on Sunday. REUTERS/Mohammed Dabbous (QATAR - Tags: POLITICS TPX IMAGES OF THE DAY) Upinzani Syria wafanikiwa Munich
Kiongozi wa upinzani wa Syria, Moaz al-Khatib, amekutana na maafisa wa Iran na Urusi kwenye mkutano wa usalama mjini Munich, Ujerumani, katika kile kinachoelezwa kama hatua ya kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Urusi na Iran zimekuwa washirika wakubwa wa Rais Bashar al-Assad na makubaliano yoyote wanayoweza kufikiwa na mahasimu wa Assad yanatazamiwa kuondoa kikwazo kwa pande hizo mbili kufikia makubaliano.

Al-Khatib alikutana kwanza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov, siku ya Jumamosi (tarehe 2 Februari), na inaaminika hatua hiyo ilitokana na ishara alizoonesha al-Khatib za kuwa tayari kuzungumza na serikali ya Syria.
"Urusi ina mtazamo wake mahsusi lakini kimsingi ni kuwa tunakaribisha majadiliano kuumaliza mgogoro huu na kuna mambo mengi yanayohitaji kujadiliwa," alisema al-Khatib baada ya mkutano huo.
Al-Khatib akubaliana na Iran
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Guido Westerwelle (kulia), na kiongozi wa upinzani wa Syria, Moaz al-Khatib.  
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Guido Westerwelle (kulia), na kiongozi wa upinzani wa Syria, Moaz al-Khatib.
Baada ya mkutano wa dakika 45 na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Ali Akbar Salehi, al-Khatib aliliambia shirika la habari la Reuters: "Tumekubaliana kwamba tunalazimika kutafuta njia ya kumaliza mateso ya watu wa Syria."
Wakati kukionekana kiwango fulani cha mafanikio yaliyofikiwa Munich, vyombo vya habari vya Iran vimeripoti kwamba Mkuu wa Baraza la Usalama la nchi hiyo, Saeed Jalil, alikwenda mjini Damascus kukutana na maafisa wa serikali ya Syria na kumsaidia Assad "kusimama imara dhidi ya njama zinazochochewa na kiburi cha ulimwengu" - kauli inayoelekezwa Marekani na mataifa ya Magharibi.
Al-Khatib alikutana pia na Makamu wa Rais wa Marekani, Joe Biden, na mjumbe maalum wa kimataifa kwa Syria, Lakhdar Brahimi.
Kiongozi mwengine wa upinzani wa Syria, Hassan Bali, ambaye yuko mjini Munich kama mwangalizi wa kujitegemea, aliuita mkutano wa al-Khatib na Biden kama "ishara kubwa kutoka kwa Wamarekani" kwamba wanaongeza msaada wao kwa waasi wanaopigana kumuangusha Assad.
Biden anasema alimtolea wito al-Khatib kuwatenga wapiganaji wenye itikadi kali za kidini na ´pia kuzikaribisha jamii nyengine kwenye upinzani, wakiwemo Wakristo, Wakurdi na hata watu wa kabila la Assad la Alawi.
Dhamira ya upinzani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Guido Westerwelle (kulia), na mjumbe wa kimataifa kwa Syria, Lakhdar Brahimi.  
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Guido Westerwelle (kulia), na mjumbe wa kimataifa kwa Syria, Lakhdar Brahimi.
Lengo la kiongozi huyo wa Muungano wa Baraza la Kitaifa la Syria kwenye mikutano hiyo lilikuwa ni kujadiliana namna ya kupata njia ya kuuondoa utawala "bila ya kuendelea kumwaga damu na kupoteza maisha."
Urusi imewahi kuzuia maazimio matatu ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yaliyodhamiria kumuondoa Assad madarakani au kumshinikiza kuzuia vita vya wenyewe kwa wenyewe, ambavyo hadi sasa vimeshagharimu maisha ya zaidi ya watu 60,000. Lakini serikali ya Urusi imejaribu pia kujitena na Assad ikisema kwamba haijaribu kumlinda na kwamba haitampa hifadhi.
Kauli ya Waziri Mkuu wa Urusi, Dmitry Medvedev, wiki hii kwamba fursa za Assad kubakia madarakani zinazidi kupungua, ilichukuliwa kama ishara ya kubadilika kwa sera ya serikali ya Urusi kuelekea Syria.
"Mazungumzo juu ya Syria yanazidi kushika kasi na Wairani sasa wameingizwa. Wacha tuone yatakavyomaliza," kilisema chanzo kimoja cha kidiplomasia.
Mgawanyiko kwenye upinzani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergey Lavrov (kushoto) na Makamo wa Rais wa Marekani, Joe Biden.  
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergey Lavrov (kushoto) na Makamo wa Rais wa Marekani, Joe Biden.
Mapema wiki hii, al-Khatib alihatarisha madaraka yake ndani ya vuguvugu la upinzani pale alipodaiwa kukiuka taratibu kwa kusema kwamba alikuwa tayari kukutana na maafisa wa serikali ya Syria kujadiliana kipindi cha mpito ikiwa wafungwa wa kisiasa wataachiliwa huru.
Kamati kuu ya kisiasa ya muungano huo wa upinzani yenye wajumbe 12 ilimwambia al-Khatib kwamba asikubali mapendekezo yoyote yatakayotolewa Munich bila ya kwanza kushauriana nao, huku chanzo kimoja kutoka upinzani kikisema kwamba hatua hiyo ya al-Khatib inaweza kuwavunja moyo wapambanaji.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayemaliza muda wake, Hillary Clinton, aliupongeza utayarifu wa al-Khatib kukutana na wajumbe wa Assad nje ya Syria, akisema "sio tu ni shujaa bali pia mtu madhubuti." Clinton pia alionyesha wasiwasi wake kwamba kwa siku za hivi karibuni, Iran imeongeza msaada wake wa kijeshi kwa Assad.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate