EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 4, 2013

Majeshi ya Ufaransa na Mali yapongezwa

Rais wa Ufaransa, Francois Hollande amesema kuwa majeshi ya nchi yake yatabakia nchini Mali kwa muda mrefu iwapo yatahitajika kuendelea kupambana na waasi wenye itikadi kali za Kiislamu kaskazini mwa nchi hiyo.

Akizungumza kwenye mji mkuu wa Mali, Bamako, hapo jana (02.02.2013), Rais Hollande alisema ugaidi umerudishwa nyuma, lakini bado haujatokomezwa kabisa. Wakati majeshi ya Ufaransa na Mali yakiendelea na jitihada za kuukomboa mji wa Kidal, ngome ya mwisho ya waasi waliolitawala eneo la kaskazini mwa miezi 10 kabla ya majeshi ya Ufaransa hayajaivamia nchi hiyo kijeshi, Rais Hollande amewaambia wananchi wa Mali kwamba ni muda kwa Waafrika kuongoza operesheni za kijeshi, lakini Ufaransa haitawatenga na kuwaacha peke yao.

Amesema Ufaransa itakuwa bega kwa bega na Mali kwa muda wote unaohitajika hadi hapo Waafrika watakapoweza wenyewe kuongoza operesheni za kijeshi. Akiwa mjini Timbuktu, alikopokewa kama shujaa, Rais Hollande aliwashukuru wanajeshi wa Ufaransa na Mali kwa juhudi zao za kuwaondoa waasi kaskazini mwa Mali, ingawa amekumbusha kuwa operesheni hiyo ya kijeshi bado haijamalizika.
Rais wa Mali amshukuru Hollande
Rais wa mpito wa Mali, Diancounda Traore, amemshukuru Rais Hollande kutokana na ufanisi wa wanajeshi wa Ufaransa, ambao amesema umelifanya eneo la kaskazini kukombolewa na kuwa huru.
Rais Francois Hollande na Rais Diancounda Traore Rais Francois Hollande na Rais Diancounda Traore
Mbali na Rais Traore kumshukuru Rais Hollande, wakaazi wa mji huo pia wamemshukuru kiongozi huyo wa Ufaransa na kuahidi kumshukuru milele ingawa wamemkumbusha kuwa amefanikiwa kuukata mti, lakini bado ana jukumu la kuondoa kabisa mizizi ya mti huo.
Marais hao wawili walizuru pia katika msikiti wa Djingareybar mjini Timbuktu uliojengwa kwa udongo miaka 700 iliyopita pamoja na maktaba ya Ahmed Baba kwa ajili ya mambo ya kale.

Aidha, walipozuru makaburi mawili ya maimamu ambayo waasi hao waliyaharibu mwezi Julai mwaka uliopita kwa madai kwamba wanaabudu sanamu, Rais Hollande amewaambia maimamu wa msikiti huo kuna haja ya kuuteketeza kabisa kwa sababu hakuna kitu kilichobakia. ''Tutayajenga tena mheshimiwa rais,'', alisema Irina Bokova, mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
Wakati rais huyo wa Ufaransa yuko Timbuktu, majeshi ya Ufaransa na Mali yalipambana na waasi. Afisa mmoja wa jeshi la Mali ameyasema hayo na kuongeza kuwa waasi waliitumia fursa hiyo kufanya mashambulizi yao, wakitarajia kwamba wanajeshi wangelikuwa wameshughulika zaidi na kuwasili kwa Rais Hollande.
Ufaransa na nia ya kukabidhi operesheni za kijeshi
Huku waasi wakiwa wamefurushwa kutoka miji yote mikubwa isipokuwa Kidal uliopo kaskazini mashariki, Ufaransa ina nia ya kukabidhi operesheni za kijeshi kwa karibu wanajeshi 8,000 wa Afrika ambao wanawasili taratibu nchini Mali na walioidhinishwa na Umoja wa Mataifa.
Wanajeshi wa Mali 
                                                    Wanajeshi wa Mali
Lakini kuna wasiwasi kuwa Mali inahitaji msaada wa muda mrefu na huku makundi ya haki za binaadamu yakiripoti mauji yaliyofanywa na wanajeshi wa Mali pamoja na waasi wenye itikadi kali za Kiislamu.
Shirika la Human Rights Watch limesema kuwa wanajeshi wa Mali wamewauwa kwa kuwapiga risasi watu wapatao 13 wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa waasi wenye itikadi kali za Kiislamu katika mji wa Sevare na kuitupa miili yao kwenye visima.
Baadhi ya waliokumbwa na mkasa huo kabla ya majeshi ya Ufaransa hayaijavamia Mali kijeshi, ni watu wa jamii wa Kituareg na Kiarabu. Kutokana na kuongezeka wasiwasi wa kuzuka mashambulizi zaidi, watu wa jamii hizo wamekimbia katika eneo hilo la kaskazini.
Mzozo wa Mali umesababisha watu 377,000 kuyakimbia makaazi yao, wakiwemo 150,000 ambao wameomba hifadhi ya ukimbizi katika mipaka ya Mali. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Rais Hollande amewatolea wito wanajeshi wa Mali kuheshimu na kuzingatia haki za binaadamu, wito ulioungwa mkono na Rais Traore ambaye pia ameahidi kuongoza mchakato wa maridhiano ya kitaifa na kurejea msimamo wake kwamba anataka kuitisha uchaguzi ifikapo Julai 31, mwaka huu.
Traore aipongeza timu ya mpira wa miguu ya Mali
Timu ya taifa ya soka ya Mali  
                                         Timu ya taifa ya soka ya Mali
Ama kwa upande mwingine, Rais wa mpito wa Mali, Diancounda Traore ameipongeza timu ya taifa ya mpira wa miguu ya Mali baada ya kupata ushindi wa mabao matatu kwa moja ikiwa ni mikwaju ya penalti dhidi ya Afrika Kusini katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika-AFCON 2013, inayoendelea nchini Afrika Kusini.
Timu hizo zililazimika kupigiana penalti baada ya mchezo kumalizika zikiwa zimetoka sare ya kufungana bao moja kwa moja. Amesema ushindi wa timu ya Mali kuingia nusu fainali, ambao ni ushindi wa kwanza tangu mwaka 1972 ni hatua ambayo imeongeza thamani na ufahari wa Mali, licha ya nchi hiyo kuwa katika mzozo. Amesema ushindi huo utaisaidia Mali kurejea tena katika amani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate