EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 25, 2013

Zitto ahusishwa kifungo cha MwanaHalisi

WAKATI wadau wa tasnia ya habari wakihoji ubabe uliotumiwa na serikali kulifungia gazeti la wiki la MwanaHalisi kwa madai ya uchochezi, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assa Mwambene, amembebesha sakata hilo Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto.

Mwambene katika kuivua lawama serikali, alidai kuwa Zitto alikuwa mtu wa kwanza baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo, aliyemtahadharisha asiende ofisini kumchekea Mkurugenzi wa Kampuni ya Hali Halisi, wachapishaji wa MwanaHalisi, Said Kubenea ili isije kumharibia kazi.

Serikali ililifungia gazeti la MwanaHalisi Julai 30 mwaka jana, kutochapisha nakala yoyote kwa muda usiojulikana kwa madai ya kuandika habari na makala ya uchochezi.
MwanaHalisi ndilo gazeti lililoandika kwa undani tukio zima la watu wanaoshukiwa kumteka kumpiga, kumng’oa meno na kisha kumtelekeza Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madakatari nchini, Dk. Stephen Ulimboka.

Mwambene ambaye aliteuliwa kushika nafasi hiyo kutoka kwa Clement Mshana aliyehamishiwa TBC, alijikuta akitoa siri hiyo Ijumaa iliyopita wakati wa kongamano la kutimiza miaka 50 ya Redio ya Ujerumani ‘Deutsche Welle’ (DW) Idhaa ya Kiswahili lililofanyika kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo ilikuja baada ya kubanwa kwa maswali yaliyokuwa yanamshutumu yeye na serikali yake kubana uhuru wa vyombo vya habari, huku baadhi ya washiriki wakiinyooshea kidole cha moja kwa moja serikali katika suala zima la kulifungia MwanaHalisi ili lisizidi kuwaumbua.

Katika utetezi wake, Mwambene alisema serikali haizuii uhuru huo, na hata hatua ya kufungiwa kwa baadhi ya magazeti ni kwa sababu ya kulinda hadhi ya nchi.
Alitolea mifano nchi za Magharibi zinazodaiwa kuwa na demokrasia kuwa nazo zinafungia au kuvifuta vyombo vya habari vyenye mwelekeo wa uchonganishi.
Alisema kwa mara ya kwanza akiwa mkurugenzi wa idara hiyo, alipofika bungeni kujitambulisha kwa wabunge, aliitwa pembeni na Zitto, na kutahadharishwa juu ya MwanaHalisi.

“Mnasema sisi tunaminya uhuru wa vyombo vya habari kwa kutolea mifano nchi za Uingereza na Marekani…mnaweza kuniambia leo Assange, yule mmiliki wa mtandao wa Wikileaks yuko wapi au gazeti la News of the World lilipo? Haya mambo yanafanyika hata katika nchi mnazozisifia kuwa na demokrasia.
“Na niseme kabisa nilipokwenda bungeni kama Mkurugenzi wa Idara ya Habari - Maelezo, Zitto aliniita pembeni na kuniambia katika kazi yangu mpya nisiende kumchekea Said Kubenea,” alisema Mwambene.

Kauli hiyo ilizua minong’ono kutoka kila kona ya ukumbi huo, huku baadhi ya washiriki wakisema serikali inatafuta sehemu ya kufichia udhaifu na ukandamizaji wa uhuru wa vyombo vya habari kwa kuwahusisha baadhi ya watu na uamuzi wa kuminya uhuru huo.
Tanzania Daima lilimtafuta Zitto kujua msimamo wake kuhusu kauli hiyo ya Mwambene katika suala zima la kufungiwa kwa gazeti la MwanaHalisi, lakini akajibu kwa kifupi kuwa hausiki.

“Sasa mimi ni mwajiri wake? Hayo maneno ni ya kutuchonganisha tu hayo, mimi nina nguvu gani ya kusema hivyo? Inaingia akilini kweli?” alijibu Zitto kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu yake ya mkononi.
Hata hivyo, Mwambene aliwashangaza waliohudhuria kongamano hilo baada ya kusema kuwa serikali imetoa uhuru mkubwa wa habari ambapo baadhi huitukana serikali, lakini hawafanywi kitu.

Baadhi ya wageni wengine walioalikwa kama wazungumzaji wakuu na kutia fora, ni nguli wa habari nchini, Jenerali Ulimwengu, mwanablog mahiri Majjid Mjengwa, Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Valerie Msoka na Naibu Mkuu wa Idhaa DW, Mohamed Abdulrahman.

Sakata la kufungiwa kwa gazeti hilo kwa sasa limezidi kuwa tata kutokana na Rais Jakaya Kikwete kunukuliwa hivi karibuni akiwa mjini Addis Ababa nchini Ethiopia kuwa hatalifungulia kamwe kutokana na kosa la kuchochea.
Pamoja na kwamba hakulitaja kwa jina, lakini kwa sasa nchini gazeti hilo ndilo limefungiwa kwa kosa hilo la kudaiwa kuchochea.
Kutokana na msimamo huo wa Rais Kikwete, Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini (MOAT) hivi karibuni kilikutana na kujadili sakata hilo na kuteua kamati ya wajumbe wa kukutana na rais kumshauri.
Wajumbe hao wataongozwa na Mwenyekiti wa MOAT, Reginald Mengi ili kukutana na Rais Kikwete ambaye wanaamini kwa sasa ndiye pekee anaweza kutoa uamuzi wa kufunguliwa kwa gazeti hilo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate