EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 25, 2013

Tume ya Pinda yapingwa... Dk. Slaa adai hoja ya Mbatia ilikuwa na majibu yote

 
SIKU moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuunda tume maalumu ya kuchunguza matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hivi karibuni, wanasiasa na wasomi wamempinga wakidai ni kupoteza muda na fedha kwa kuwa hoja binafsi ya Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia ilikuwa na majibu.

Kwa nyakati tofauti katika mahojiano na gazeti hili, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, na Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Benson Bana walihoji ni tume na kamati ngapi zimeundwa na kutolewa taarifa kuhusu matatizo ya elimu katika miaka 15 iliyopita na hatua zipi zimechukuliwa kurekebisha dosari zilizoonekana.

Dk. Slaa alishangazwa na hatua hiyo ya Waziri Mkuu kuunda tume kwa ajili ya kufuatilia kufeli kwa wanafunzi, akisema ni juzi tu Bunge limemaliza kikao chake Dodoma na kuitupilia mbali hoja binafsi ya Mbatia.

Alisema hoja binafsi ya Mbatia ilikuwa na nia ya kupitisha azimio la Bunge kuunda kamati teule ya kuchunguza tatizo la udhaifu katika sekta ya elimu, lakini kwa ushabiki wa wabunge wa CCM akiwemo Waziri Mkuu, ilikataliwa.

“Wiki mbili hazijapita wameumbuliwa na matokeo, na sasa Waziri Mkuu anaunda tume. Huku ni kuwadanganya Watanzania. Pinda ni kiongozi wa shughuli za serikali bungeni na kiranja wa mawaziri wote, Waziri wa Elimu, Dk. Shukuru Kawambwa alilidanganya Bunge na taifa kuhusiana na swala la mitaala, ambalo lina uhusiano mkubwa na ubora wa elimu.
“Waziri Mkuu alikuwepo, hakuchukua hatua wala ya kumsahihisha Kawambwa au kusema ukweli na kuchukua hatua kwa waziri huyo kwa jambo lililotokea mbele ya macho na masikio yake,” alisema.

Aliongeza kuwa kwa hilo, Pinda hastahili kuchukua hatua ya kuunda tume, bali kujiuzulu kwa kushindwa kuwajibika na pia kushiriki kulidanganya taifa.
Dk. Slaa alisema kuwa Serikali ya CCM imeunda tume na kamati nyingi, lakini taarifa zilizotolewa hazijawahi kufanyiwa kazi, na kwamba kama hali ndiyo hiyo, hata tume hii inayoundwa hakuna jipya.

“Suala la elimu halihitaji kuundiwa tume wala kamati ya uchunguzi. Serikali ya Rais Kikwete na Pinda kweli hawajui matatizo yanayofanya elimu yetu kudorora mpaka waunde tume?” Alihoji Dk. Slaa na kuongeza kuwa Serikali ya CCM haijui kwamba bajeti ya elimu ni ndogo ikilinganishwa na zile za majirani zetu katika sekta hiyo.
Dk. Slaa alisema kuwa ni usanii na kuendeleza ufisadi kwani tume itaendelea kuangamiza fedha kwa vile serikali haijaonesha utashi wa kisiasa kuboresha elimu ya watoto ya Watanzania.

Alisema kinachotakiwa sasa ni kuunganisha nguvu na kukataa usanii wowote katika masuala ya msingi. Kwamba wale wote waliodanganya taifa wawajibike kwa kujiuzulu au wawajibishwe.

Aliongeza kuwa, watoto waliofeli waandaliwe utaratibu wa kunusuru maisha yao badala ya kuunda tume wakati maisha yao ya baadaye yakivurugika.
Naye Dk. Bana alimbeza Pinda kwa hatua hiyo ya kuunda tume kwa masuala ya mtihani, akisema tatizo la kufeli kwa wanafunzi halihitaji tume kwani kasoro ziko wazi.
Alisema kuwa matatizo ya walimu yanajulikana, huku serikali ikijidanganya kutengeneza sera ya elimu kinyemela bila kushirikisha wataalamu.

“Mtihani ni sehemu ndogo sana, lakini siasa za zimamoto ndizo zimetufikisha hapa. Tujue kuwa siasa za zimamoto hazisaidii Watanzania, tunapoteza muda na fedha zetu, lakini mfumo wa elimu unapaswa uangaliwe kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.
“Utaratibu huu wa kuanza kuunda tume kila darasa likifeli zitaundwa ngapi?” alisema na kuongeza kwamba tatizo la elimu ni la kitaaluma, si siasa.
Alisema kuwa wanangoja kuona wale watakaoteuliwa kutoka katika chuo hicho kuingia kwenye tume ya Pinda kama watakuwa tayari kwenda kuungana na suala hili ambalo halizingatii utaalamu, badala yake linatibu ugonjwa na kukwepa dalili zake.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate