SASA ni dhahiri kwamba benki zetu hapa
nchini zimezidiwa nguvu na mitandao ya wizi wa fedha kupitia mashine za
kutolea fedha (ATM). Vyombo vya habari vimekuwa vikitoa habari za wizi
huo kila kukicha, huku benki hizo zikihaha kuficha habari hizo kwa hofu
ya kukimbiwa na wateja.
Baadhi ya benki zimekiri kwamba tatizo la wizi wa fedha kutoka katika akaunti za wateja sasa limezizidi kimo, kwa maana ya kuota mizizi na kuwanyima usingizi watendaji wa benki hizo.
Pamoja na juhudi za benki hizo kujaribu kupata suluhisho la pamoja kuhusu wizi huo, mtandao huo wa wizi umekwamisha juhudi hizo kutokana na kubuni mbinu mpya siku hadi siku.
Maofisa wa benki pia wameshtushwa na kiwango kikubwa kinachoibwa hivi sasa, kutoka malaki na mamilioni miaka miwili mitatu iliyopita hadi kufikia mabilioni katika siku za hivi karibuni. Maofisa hao wanakubaliana katika mambo mawili makubwa. Kwanza, kwamba tatizo ni kubwa na liko juu ya uwezo wao. Pili, kwamba mtandao huo mkubwa ni wa kimataifa na unaratibiwa kutoka katika miji mikubwa duniani yenye mashina katika nchi zenye udhibiti legelege wa fedha kama Tanzania.
Hapa Tanzania, hapo mwanzo wizi huo ulikuwa katika Jiji la Dar es Salaam na baadaye benki zikashtukia mtandao huo ukiwa tayari umepanuka hadi miji mikubwa mikoani, kabla haujabisha hodi kwa kasi katika miji midogo iliyoko vijijini.
Hivyo, maofisa wengi wa benki hawalioni tukio la
juzi kama la kushangaza, ambapo polisi wilayani Rungwe, mkoani Mbeya
waliwanasa watu wanne, akiwamo mwanafunzi aliyemaliza kidato cha nne
mwaka jana wakiiba fedha katika ATM ya Benki ya NMB, Tawi la Tukuyu kwa
kutumia kadi 150 bandia za ATM.
Tumeambiwa kwamba hadi wanatiwa mbaroni tayari walikuwa na zaidi ya Sh20 milioni kibindoni. Polisi wanasema kadi zote walizokutwa nazo zilikuwa zinaonyesha ni za walimu kutoka wilayani Mbozi. Swali lililowatatiza maofisa wa benki na vyombo vya usalama ni kwa nini kadi zote hizo za wilayani Mbozi zipelekwe kutolea fedha katika ATM za wilayani Rungwe?
Kama benki sasa zimekiri kwamba hazina uwezo wa kuma liza tatizo hilo, lazima tukubaliane kwamba sasa zinahitajika nguvu na mbinu za ziada. Hatuwezi tena kuziachia benki zetu kupambana kichwakichwa na mitandao ya wizi wa fedha yenye zana na teknolojia ya kisasa, wakati tuki tambua kwamba kufanya hivyo ni kuziharakishia kifo.
Ebu tuangalie wajibu wa Benki Kuu ya Tanzania
(BoT) ambayo ina wajibu mkubwa wa kusimamia na kuratibu benki zote
nchini kisera.
Hatuoni benki hiyo mama ikifanya juhudi za kutosha kuishauri Serikali kuingilia kati suala la mitandao ya wizi wa fedha za wateja kupitia ATM. BoT inapaswa kutoa miongozo na maelekezo kwa benki hizo kuhusu masuala mbalimbali ya kuhakikisha fedha za wateja wa benki hizo zinakuwa salama.
Hatuoni benki hiyo mama ikifanya juhudi za kutosha kuishauri Serikali kuingilia kati suala la mitandao ya wizi wa fedha za wateja kupitia ATM. BoT inapaswa kutoa miongozo na maelekezo kwa benki hizo kuhusu masuala mbalimbali ya kuhakikisha fedha za wateja wa benki hizo zinakuwa salama.
Hii ni pamoja na kuangalia upya teknolojia inayotumiwa na benki zetu. Yapo madai kwa mba benki hizo zinatumia mashine chakavu za ATM ambazo ni mitumba kutoka nchi za nje. Madai mengine ni kwamba baadhi ya mafundi wa mashine hizo ndiyo wanashirikiana na mitandao ya wizi ndani ya benki zenyewe kuwaibia wateja.
Hata hivyo, yote hayo yanatokea kwa sababu vyombo
vyetu vya usalama vimelala usingizi wa pono na vinasubiri tu kuzinduliwa
na raia wema ndipo vichukue hatua. Tunadhani umefika wakati wa
kuviwajibisha ili vijihusishe tu na kazi vilivyoanzishwa kuzifanya.
No comments:
Post a Comment