EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 2, 2013

Chadema yamng’ang’ania Kawambwa

WAKATI Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameunda tume kuchunguza matokeo mabaya ya mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012, Chadema kimesisitiza msimamo wake kwamba kitafanya maandamano kushinikiza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa na Naibu wake, Philipo Mulugo wajiuzulu.
 
Mapema wiki iliyopita Pinda alitangaza kuunda tume kuchunguza matokeo hayo, hatua ambayo Rais Jakaya Kikwete alitangaza kuiunga mkono katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi aliyoitoa juzi.

Lakini jana Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema watafanya maandamano makubwa aliyoyaita ya kihistoria, katika mikoa ya Mwanza, Arusha, Mbeya na Dar es Salaam ili kushinikiza kutekelezwa kwa hatua hiyo.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Mtatatila, Sumbawanga mkoani Rukwa, Mbowe alisema: “Lengo la maandamano ni kuwataka waziri wa elimu na naibu wake wajiuzulu kwani wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo na kusababisha watoto wa maskini kufanya vibaya kwenye mitihani yao.”


Alisema maandamano hayo yatahusisha wafanyakazi wa Serikali, mama lishe na wafanyabiashara wa usafirishaji wanafunzi wa shule za msingi na sekondari... “Siku hiyo hakutakuwa na masomo wala kazi, kila kitu kitasitishwa.”
Mbowe alisema maandamano hayo yatakuwa ya kihistoria na kwamba Chadema kinataka kuwafungua macho wananchi walio na kipato cha chini ambao hawana uwezo wa kusomesha watoto wao nje ya nchi ili washinikize Dk Kawambwa na Mulugo waachie ngazi.

“Tunataka shule za sekondari na msingi zisigeuzwe kuwa vituo vya kulelea watoto, bali vifanye kazi za kutoa elimu, kama ilivyokusudiwa,” alisema Mbowe.
Hata hivyo, Mbowe aliwataka wananchi kuwa makini na uchochezi unaofanywa na baadhi ya vyama vya siasa, badala yake waangalie chama chenye sera, mtazamo na harakati za kuleta mabadiliko yatakayokuwa na manufaa kwa Watanzania wote.

“Njia sahihi ni kuhakikisha mnajiondoa, kwani ili muweze kujua mustakabali wa maisha yenu ni lazima mhakikishe mnakuwa makini kufanya uamuzi ulio sahihi kwa viongozi mnaowataka, ”alisema Mbowe.
Hii ni mara ya pili katika mwaka huu kwa Chadema kutaka viongozi wajiuzulu. Mwezi uliopita, chama hicho kilimtaka Spika wa Bunge, Anne Makinda na Naibu wake, Job Ndugai wajiuzulu kwa maelezo kuwa wamekuwa wakiminya demokrasia, kuubana upinzani na kupendelea chama tawala (CCM) bungeni.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate