EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, March 4, 2013

USIJIDANGANYE…BILA MPENZI MAISHA HAYAWEZI KUWA KAMILIFU!

Mpenzi msomaji wangu, katika ulimwengu wa mapenzi kuna mambo ambayo yamekuwa yakijitokeza na kuwafanya baadhi ya watu kuishia kusema kuwa ni bora waishi peke yao kuliko kuwa na wapenzi.
Wanaosema hivyo ni wale ambao wametendwa kwa kiwango kikubwa. Wapo ambao wametokea kuwapenda sana wapenzi wao lakini kinyume chake ikawa ni kulizwa kila siku huku usaliti ukiwa ni sehemu ya maisha yao ya kila siku.
Kimsingi hakuna kitu kinachouma kama kusalitiwa, tena kusalitiwa na mtu ambaye moyo wako umempa nafasi kubwa sana. Zaidi ya yote inaumiza sana unapompenda mtu lakini yeye akawa hakupendi, matokeo yake yakawa ni mpenzi kukutesa. Kwa hayo kweli unaweza kufikia wakati ukasema ni bora kumuacha na kuishi peke yako.
Cha kujiuliza ni kwamba, ni kweli unaweza kuishi peke yako bila kuwa na mpenzi? Ni wangapi ambao waliwahi kusema hivyo lakini leo hii wako kwenye uhusiano na watu wengine? Ni wengi tu na imetokea hivyo kwa kuwa, mapenzi ni sehemu muhimu sana katika maisha ya binadamu.
 
Hata kama una uwezo mkubwa kiasi gani lakini huwezi kusema umetosheka bila kuwa na mpenzi na ndiyo maana wapo ambao wana kila kitu lakini mapenzi yakiwakorofisha kidogo tu wanakonda na kutoona umuhimu wa kuendelea kuishi.
Ndiyo maana tunaambiwa kwamba, tunapokwazwa na wale tuliotokea kuwapenda sana tusione kuwa ni mwisho wa sisi kupenda. Tuone ni hatua ya kuelekea kuwapata wale wenye mapenzi ya kweli na sisi.
 
Nimeshawahi kusema huko nyuma kwamba, wale ambao leo unawaona wako kwenye uhusiano bora wenye furaha wengi waliwahi kutendwa sana, nikasema katika safari ya kumpata mtu mwenye mapenzi ya kweli ni lazima uwe tayari kuumizwa kwanza, huo ndiyo ukweli wenyewe.
 
Utakuwa ni mtu wa ajabu kama utakata tamaa ya kuwa na mpenzi baada ya kuumizwa na mtu wa kwanza. Hivi unajuaje kama baada ya huyo utampata yule uliyepangiwa na Mungu?
Tusiwe watu wa kukata tamaa mapema na kufikia hatua ya kusema hauko tayari kupenda. Kama hauko tayari kupenda basi utakuwa hutaki kuendelea kuishi na kama ni hivyo ni bora uondoke tu duniani.
 
Najua wakati mwingine tunatamka maneno hayo kwa hasira hasa tunapofikiria jinsi tulivyopoteza muda wetu kwa watu tuliotokea kuwapenda sana lakini maumivu hayo yasitupeleke kule ambako tunaweza kuyaharibu maisha yetu kwa kupoteza furaha.
Wapo ambao eti mpaka leo wanajifanya ni wagumu. Hawataki kuwa na wapenzi kwa sababu waliwahi kutendwa. Sikatai, hayo ni maamuzi ya mtu lakini watu hao ukijaribu kuwafuatilia utabaini wanakosa furaha iliyokamilika. Wanajikaza wakidhani wanaziridhisha nafsi zao lakini kiukweli wanaathirika sana.
 
Naomba nisema tu kwamba, unaposema hutaki tena kuwa na mpenzi unajiweka kwenye mazingira mazuri ya kuathirika kisaikolojia. Mpenzi ni muhimu sana kwenye maisha yako lakini uvumilivu pia unatakiwa kuchukua nafasi yake.
Mpende akupendaye na asiyekupenda achana naye ili kumpa nafasi yule ambaye Mungu amepanga kuwa wako. Unapofanyiwa yale ambayo hukutarajia kufanyiwa na ‘mtu’ wako, kama yanavumilika, vumilia lakini kama unaona yanaukwaza moyo wako, muweke pembeni kisha kuwa na subira kwani naamini Mungu hawezi kukutupa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate