Mpenzi msomaji wangu, katika ulimwengu wa mapenzi kuna mambo ambayo
yamekuwa yakijitokeza na kuwafanya baadhi ya watu kuishia kusema kuwa ni
bora waishi peke yao kuliko kuwa na wapenzi.

Wanaosema hivyo ni wale
ambao wametendwa kwa kiwango kikubwa. Wapo ambao wametokea kuwapenda
sana wapenzi wao lakini kinyume chake ikawa ni kulizwa kila siku huku
usaliti ukiwa ni sehemu ya maisha yao ya kila siku.
Kimsingi hakuna
kitu kinachouma kama kusalitiwa, tena kusalitiwa na mtu ambaye moyo wako
umempa nafasi kubwa sana. Zaidi ya yote inaumiza sana unapompenda mtu
lakini yeye akawa hakupendi, matokeo yake yakawa ni mpenzi kukutesa. Kwa
hayo kweli unaweza kufikia wakati ukasema ni bora kumuacha na kuishi
peke yako.
Cha kujiuliza ni kwamba, ni kweli unaweza kuishi peke yako bila kuwa na mpenzi? Ni wangapi ambao waliwahi kusema hivyo lakini leo hii wako kwenye uhusiano na watu wengine? Ni wengi tu na imetokea hivyo kwa kuwa, mapenzi ni sehemu muhimu sana katika maisha ya binadamu.
Cha kujiuliza ni kwamba, ni kweli unaweza kuishi peke yako bila kuwa na mpenzi? Ni wangapi ambao waliwahi kusema hivyo lakini leo hii wako kwenye uhusiano na watu wengine? Ni wengi tu na imetokea hivyo kwa kuwa, mapenzi ni sehemu muhimu sana katika maisha ya binadamu.
Hata
kama una uwezo mkubwa kiasi gani lakini huwezi kusema umetosheka bila
kuwa na mpenzi na ndiyo maana wapo ambao wana kila kitu lakini mapenzi
yakiwakorofisha kidogo tu wanakonda na kutoona umuhimu wa kuendelea
kuishi.
Ndiyo maana tunaambiwa kwamba, tunapokwazwa na wale tuliotokea kuwapenda sana tusione kuwa ni mwisho wa sisi kupenda. Tuone ni hatua ya kuelekea kuwapata wale wenye mapenzi ya kweli na sisi.
Ndiyo maana tunaambiwa kwamba, tunapokwazwa na wale tuliotokea kuwapenda sana tusione kuwa ni mwisho wa sisi kupenda. Tuone ni hatua ya kuelekea kuwapata wale wenye mapenzi ya kweli na sisi.
Nimeshawahi
kusema huko nyuma kwamba, wale ambao leo unawaona wako kwenye uhusiano
bora wenye furaha wengi waliwahi kutendwa sana, nikasema katika safari
ya kumpata mtu mwenye mapenzi ya kweli ni lazima uwe tayari kuumizwa
kwanza, huo ndiyo ukweli wenyewe.
Utakuwa ni mtu wa ajabu kama
utakata tamaa ya kuwa na mpenzi baada ya kuumizwa na mtu wa kwanza. Hivi
unajuaje kama baada ya huyo utampata yule uliyepangiwa na Mungu?
Tusiwe watu wa kukata tamaa mapema na kufikia hatua ya kusema hauko tayari kupenda. Kama hauko tayari kupenda basi utakuwa hutaki kuendelea kuishi na kama ni hivyo ni bora uondoke tu duniani.
Tusiwe watu wa kukata tamaa mapema na kufikia hatua ya kusema hauko tayari kupenda. Kama hauko tayari kupenda basi utakuwa hutaki kuendelea kuishi na kama ni hivyo ni bora uondoke tu duniani.
Najua wakati mwingine
tunatamka maneno hayo kwa hasira hasa tunapofikiria jinsi tulivyopoteza
muda wetu kwa watu tuliotokea kuwapenda sana lakini maumivu hayo
yasitupeleke kule ambako tunaweza kuyaharibu maisha yetu kwa kupoteza
furaha.
Wapo ambao eti mpaka leo wanajifanya ni wagumu. Hawataki kuwa na wapenzi kwa sababu waliwahi kutendwa. Sikatai, hayo ni maamuzi ya mtu lakini watu hao ukijaribu kuwafuatilia utabaini wanakosa furaha iliyokamilika. Wanajikaza wakidhani wanaziridhisha nafsi zao lakini kiukweli wanaathirika sana.
Wapo ambao eti mpaka leo wanajifanya ni wagumu. Hawataki kuwa na wapenzi kwa sababu waliwahi kutendwa. Sikatai, hayo ni maamuzi ya mtu lakini watu hao ukijaribu kuwafuatilia utabaini wanakosa furaha iliyokamilika. Wanajikaza wakidhani wanaziridhisha nafsi zao lakini kiukweli wanaathirika sana.
Naomba nisema tu kwamba, unaposema hutaki
tena kuwa na mpenzi unajiweka kwenye mazingira mazuri ya kuathirika
kisaikolojia. Mpenzi ni muhimu sana kwenye maisha yako lakini uvumilivu
pia unatakiwa kuchukua nafasi yake.
Mpende akupendaye na asiyekupenda achana naye ili kumpa nafasi yule ambaye Mungu amepanga kuwa wako. Unapofanyiwa yale ambayo hukutarajia kufanyiwa na ‘mtu’ wako, kama yanavumilika, vumilia lakini kama unaona yanaukwaza moyo wako, muweke pembeni kisha kuwa na subira kwani naamini Mungu hawezi kukutupa.
Mpende akupendaye na asiyekupenda achana naye ili kumpa nafasi yule ambaye Mungu amepanga kuwa wako. Unapofanyiwa yale ambayo hukutarajia kufanyiwa na ‘mtu’ wako, kama yanavumilika, vumilia lakini kama unaona yanaukwaza moyo wako, muweke pembeni kisha kuwa na subira kwani naamini Mungu hawezi kukutupa.
No comments:
Post a Comment