EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, May 6, 2013

CUF: Spika Makinda hafai • Wadai ana uwezo mdogo wa kuongoza.

MWENYEKITI wa taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesema Spika wa Bunge, Anna Makinda, ameshindwa kukiongoza chombo hicho kwa maslahi ya taifa, badala yake amegeuka kuwa kinara wa upendeleo kwa chama na serikali ya CCM.

Profesa Lipumba amemtaka Makinda atafakari na apime uwezo wake wa kiuongozi katika Bunge na afanye maamuzi magumu ya kubadilika kifikra kwa kuacha upendeleo anaoufanya kwa sasa.

Kauli hiyo aliitoa juzi jijini Mwanza alipokuwa akizungumza na Tanzania Daima, muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkutano wa kujadili na kuchangia mawazo juu ya maendeleo kwa wote mkoa wa Mwanza, uliofanyika katika Hoteli ya JB Belmont.
Alisema Spika amejionyesha uwezo wake mdogo wa kuongoza Bunge na akubali kushauriwa au kubadilika kifikra ili alinusuru Bunge lisiendelee kudharaulika ndani na nje ya nchi.

“Spika ameshindwa kutenda haki kwa nafasi yake aliyonayo bungeni. Hawatendei haki wabunge wa vyama vya upinzani….mbaya zaidi kiti chake kimeonesha wazi kuegemea chama na serikali ya CCM katika mijadala ya kitaifa na wananchi wake.
Profesa Lipumba alitaka Katiba mpya ijayo lazima itamke Spika asitokane na wabunge, bali atoke nje ya Bunge ili kukiongoza chombo hicho kwa manufaa ya taifa zima.

Alisema Bunge ni chombo muhimu sana katika maendeleo na kugawa haki kwa wote, hivyo kinapoongozwa na mtu anayeegemea upande wa serikali na chama chake anawanyima Watanzania kupata haki za kimaendeleo.
“Tunataka Katiba mpya izuie Spika asitokane na wabunge. Tunataka Spika atoke nje ya Bunge ili aweze kutenda haki kwa Watanzania wote,” alisema.

Alisema uwajibikaji mbovu wa Bunge unazorotesha sana kasi na mwelekeo wa maendeleo ya wananchi na taifa zima na kwamba upo ulazima Watanzania kufanya maamuzi magumu ya kuiondoa madarakani CCM ifikapo mwaka 2015.

Kwa mujibu wa Profesa Lipumba, serikali ya CCM imeshindwa kutekeleza matakwa ya wananchi waliyoiweka madarakani, hivyo hawana budi kuiangusha CCM katika uchaguzi mkuu ujao ili wapate maendeleo.

Wakati huohuo, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, amewashambulia watumishi wa Bunge kwa kusema karibu nusu ya watumishi hao ni mzigo kutokana na kushindwa kufanya kazi katika kiwango kinachotakiwa.

Ndugai aliitoa kauli hiyo mjini hapa jana alipochangia katika semina ya wabunge iliyoandaliwa na tume ya mipango iliyojadili jinsi ya uendelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Alisema kumekuwepo na tatizo la viongozi kufanya uozo ndani ya ofisi zao, lakini cha kushangaza hakuna mtu mwenye ujasiri wa kuwafukuza na matokeo yake watumishi wanaendelea kufanya jambo ambalo si sahihi.

“Mfano mzuri kuna walimu wanafelisha wanafunzi wao karibu kwa miaka mitano mfululizo, lakini hakuna mtu anayewafukuza au kuwapa adhabu yoyote jambo hilo ni hatari na kuendeleza kufanya kazi kwa mazoea.

“Sisi wabunge ambao tuko majimboni tunapata shida sana na watumishi wa halmashauri wengi wanafanya kazi hovyo, lakini pia hata bungeni si wote ambao wanafanya kazi kwa uaminifu, hata hapa karibu nusu ya wafanyakazi wa Bunge ni mzigo lakini hakuna mtu ambaye anaweza kuwawajibisha,” alisema Ndudai.

Mbunge wa Viti Maalumu, Riziki Lulida (CCM), akichangia alisema kuwa bado kuna tatizo kubwa la watumishi wa serikali kulindana na ndiyo maana kuna uharibifu.
Lulida alisema kinachosumbua katika mipango mingi serikalini ni kuwepo kwa urasimu, upendeleo ikiwa ni pamoja na kulindana pasipo na sababu za msingi.

Akichangia hoja hiyo, mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola, alisema kamwe Tanzania haiwezi kuwa na maendeleo kutokana na kuwepo kwa utamaduni wa kufanya kazi kwa mazoea.
Pia alisema mawaziri hawawezi kufanya vizuri katika kuendeleza miradi kwa kuwa wanakwamishwa na makatibu wakuu wa wizara husika kwa kuwachukulia mawaziri kama wapitaji na wao ndio wa kudumu.

“Tumekuwa tukililia mfumko wa bei nani asiyejua kuwa wafanyabiashara wanafanya makusudi kuficha bidhaa, ili waweze kupata nafasi ya kupandisha bei bidhaa hizo? Fikiria vipo viwanda vya kuzalisha sukari lakini wenye viwanda wanafanya kusudi kuzalisha kidogo.
“Waziri Mkuu amepiga kelele juu ya kupanda kwa bei ya sukari lakini hakuna kilichofanyika, jambo ambalo ni hatari na kamwe hakuna maendeleo ambayo yanaweza kujitokeza kama hali hiyo itaendelea katika maeneo mbalimbali,” alisema Lugola.
CHANZO TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate