EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, May 6, 2013

Maafa Arusha • Bomu lalipuliwa kanisani.

WATU wawili wamekufa na wengine 66 kujeruhiwa baada ya kutokea mlipuko wa kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu wakiwa katika ibada ya kutabaruku parokia mpya ya Olasiti, jijini Arusha jana.

Mlipuko huo umetokea huku kukiwa na vuguvugu la machafuko ya kidini nchini pamoja na onyo la Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Said Mwema, kuwataka Watanzania wawe macho na magaidi wa vikundi vya Al Shabab na Al-Qaeda wanaoweza kufanya mashambulizi wakati wowote.

Miongoni mwa walionusurika ni balozi wa Baba Mtakatifu nchini Mhashamu Askofu Mkuu Francisco Padila, Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Arusha Josephat Lebulu, mapadri na waumini waliohudhuria ibada hiyo.

Kati ya watu waliojeruhiwa, wengine walikimbizwa katika hospitali ya rufaa ya KCMC, mkoani Kilimanjaro, kwa matibabu zaidi.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo ambao walifika kusali katika kanisa hilo walisema lilikuwa la kushtukiza baada ya kitu ambacho wanadai kilikuwa katika mfuko wa Rambo kilipodondoka nje ya jengo la kanisa hilo na kulipuka.

“Kwa kweli tukio hili lilikuwa la ghafla sana ambalo hatukulitegemea kwa kuwa waumini wote tulikuwa tukimuangalia Askofu Mkuu akikaribia kukata utepe na ghafla ukatokea mlipuko huo na kuzua taharuki kubwa kwetu,” alisema mmoja wa mashuhuda hao.

Mpaka wakati tunaelekea mitamboni jeshi la polisi lilikuwa likimshikilia mtu mmoja kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo akidaiwa ndiye aliyerusha kitu kilichosababisha mlipuko huo katika kanisa hilo.

Akizungumzia tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, baada ya kufika katika eneo la tukio aliwataka waumini kutulia na kutohusisha tukio hilo na dini yoyote.

“Ndugu zangu tukio limeishatokea….., ni tukio kama mengine; tutulie linafanyiwa uchunguzi na tusilihusishe tukio hilo na dini yoyote,” alisema.
Mulongo alipata wakati mgumu wakati akitoka katika Hospitali ya Mount Meru baada ya kikundi cha wananchi waliokuwepo hapo kuanza kumzomea.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabasi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba jeshi hilo linamshikilia mtu mmoja kwa uchunguzi kuhusiana na mlipuko huo.
Kamanda Sabasi alisema wanashirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuchunguza sampuli za mchanga waliochukua katika eneo hilo la tukio ili kujua mlipuko huo umetokana na kitu gani.

Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema, akiwa ameongozana na mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari, walifika katika kanisa hilo na kuamsha kelele za kushangiliwa na wananchi kujisahau kama kuna janga limetokea katika eneo hilo.

Akizungumza katika eneo hilo, Lema aliwapa pole waliofikwa na maafa hayo huku akilitaka Jeshi la Polisi kutumia nguvu ileile waliyoitumia kumkamata yeye kufanikisha kukamatwa wahusika wa tukio hilo.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Frida Mokitu, alithibitisha kupokea majeruhi 42 na kuelezea kifo cha watu wawili ambao hawakulitambuliwa majina yao kwa wakati huo.
Majeruhi wengine 16 walipelekwa katika Hospitali ya Seliani iliyoko katikati ya jiji la Arusha wakiendelea kupata matibabu na wagonjwa wengine wawili wakikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC.

Baadhi ya majina ya majeruhi iliyopatikana jana walioko katika Hospitali ya Mount Meru ni Concesta Julius Mbaga, Edith Ndowo, Christopher Raymond, Frank Donatus, Deborah Joakim, Elizabeth Isidory, Beather Cornel, Neema Daudi na Anold Alex.
Wengine ni Sophia Kimolo, Lightness Nelson, Theophilda Inocent, Jackline John, Faustin Andrea, Regina Daud, Donald Swai, Restuta Alex, Alfonce Nyakondi, Mathias Kiya, Anna Didas, Albert Njou, Flomena Nyereza, Dereck Kessi, Mary Okeere na Joyce Okeele.
Aidha wengine ni Doreen Pankaras, Fatuma Tarimo, Faustin Andrea, Anna Didas, Anastazia Regine, Anna Kessy, Elizabeth Masawe na Faustin Shirima.

Utoaji damu
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Mbunge wa Arumeru Mashariki na kada wa CHADEMA James Ole Millya waliwahamasisha wananchi wa Arusha kujitokeza kujitolea damu kwa ajili ya kusaidia matibabu kwa majeruhi.

Akizungumza kwa simu na gazeti hili, Lema alisema, “Nimewahamasiha wapigakura wangu wafike kujitolea damu, zoezi hili limeongozwa na Nassari na Ole Millya nitafuatia mimi, na vijana wengi zaidi ya 200 wamefuatana nasi tuko hapa hospitali ya mkoa, maana tunajua katika hali hii ndugu zetu wanaweza kuhitaji damu.”

Akizungumzia tukio hilo, Makamu Mkuu wa Chuo cha Mtakatifu Agustino, Padri Charles Kitima, alisema kitendo hicho ni uhalifu uliotendwa ili kuvuruga ibada.
“Kama ni bomu tujiulize nini kinaingia nchini, nyumba za ibada ni tulivu, ni mahali ambapo tunapaswa kukimbilia hivyo hatutegemei vitu kama hivi kutokea huko, ila tusubiri taarifa ya jeshi la polisi, serikali inapaswa ijiulize ni kwa nini kwenye nyumba za ibada, ingawa tunatoa tahadhari kuwa uhalifu huu usihusishwe na mapenzi ya Mungu, ni maslahi ya waovu kwa maslahi ya kutesa watu.”

Wananchi wavunja geti
Wakati majeruhi wakiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Mount Meru, mgonjwa mmoja ambaye jina halikupatikana alizidiwa hali iliyolazimu ahamishiwe KCMC lakini gari la wagonjwa lililombeba mgonjwa huyo lilipofika getini halikufunguliwa kutokana na kutokuwapo kwa walinzi.
Kutokuwapo kwa walinzi hao kuliamsha hasira za wananchi ambao waliamua kusubiri kwa dakika 10 na baada ya hapo waliamua kuvunja geti la hospitali hiyo ili kuruhusu gari liwahi KCMC.

Bilal, IGP Mwema wazuru
Wakati huohuo Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Saidi Mwema, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima, na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele, walifika eneo la tukio jana jioni kuwajulia hali majeruhi na kutoa pole kwa waliofikwa na maafa hayo.

Dk. Bilal alivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwasaka wahusika wa tukio hilo ili sheria ichukue mkondo wake huku akiwataka watu wa dini mbalimbali kukaa kwa amani na kuepusha chokochoko ya aina yoyote ile.

Dk. Bilal aliamua kumchukua mtoto wa kiume Anorld Alex (10) aliyeumia katika tukio hilo na kuahidi kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili akapatiwe matibabu kutokana na hali yake kuwa mbaya.

Tukio la Arusha
Tukio la jana limetokea siku chache tu baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Saidi Mwema, kusema zipo dalili za kuibuka makundi ya kigaidi ndani ya nchi yakiratibiwa na makundi ya Al-Qaeda na Al-Shabab.

Mwema alitoa kauli hiyo April 21 visiwani Zanzibar kwenye semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambapo aliwakilishwa na Kamishna Mwandamizi wa Polisi Hussein Nassor Laisseri, alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu hali ya uhalifu Tanzania Bara na visiwani Zanzibar.
Matukio ya kigaidi yamekuwa yakitokea mara kwa mara nchi jirani ya Kenya ambapo inadaiwa kikundi cha Al Shabab kimekuwa kikiendesha matukio hayo kupinga serikali ya Kenya kupeleka majeshi yake nchini Somalia.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate