
STAA wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe anadaiwa kutupiwa nje na baadaye kuzuiliwa vyombo vyake kwenye ile nyumba ya kifahari ya kupanga aliyokuwa akiishi Mbezi Beach, Dar es salaam.
Madai hayo yalitua kwenye dawati la Ijumaa Wikienda hivi karibuni
ambapo ilielezwa kuwa ishu hiyo ilijiri maeneo hayo baada ya bishosti
huyo kudaiwa kuwa alishindwa kulipa kodi ya pango ya mwezi mmoja ambayo
ni Dola 1,500 (zaidi ya Sh. milioni 2.4 za madafu).
Kwa mujibu wa
‘sosi’ wetu aliyekuwepo eneo la tukio, Wolper aliwatuma ndugu zake
kwenda kuchukua vyombo hivyo lakini walipofika mama mwenye nyumba (jina
tunalo), aliwazuia na kumpigia simu staa huyo akimwambia kuwa anatakiwa
kulipa fedha kabla ya kuchukua vitu vyake.
“Wolper alipopigiwa simu
alikuja juu na kumwambia mama mwenye nyumba kuwa kama anamfuatilia eti
atamfunga kama mume wa mama huyo alivyofungwa na kumwambia kuwa
atampelekea polisi wakamkamate,” alidai mtu huyo.
Sosi huyo aliendelea kudai kuwa baada ya kuona soo limekuwa la kutishana, mama huyo alikwenda kumfuata mjumbe wa nyumba kumi aliyefahamika kwa jina moja la Musa na kumueleza kisha kumuomba asimamie zoezi hilo.
Sosi huyo aliendelea kudai kuwa baada ya kuona soo limekuwa la kutishana, mama huyo alikwenda kumfuata mjumbe wa nyumba kumi aliyefahamika kwa jina moja la Musa na kumueleza kisha kumuomba asimamie zoezi hilo.
Baada
ya kujazwa data hizo, Ijumaa Wikienda lilifanya jitihada za kumsaka
Wolper na alipopatikana alisema kuwa hajawahi kudaiwa na huyo mama na
anayesema hivyo huenda alimuona wakati anahamisha vitu vyake kwani kwa
sasa amehama kwenye nyumba hiyo.
Mwandishi wetu hakuishia hapo, alimtafuta shemeji wa mama mwenye nyumba aliyetajwa kwa jina moja la Jamal ambaye alikiri kutokea kwa ishu hiyo na kwamba suala hilo lilimalizika ambapo vyombo vya Wolper vilitolewa kwa ajili ya kufanya usafi kwani kuna mtu mwingine alikuwa akihamia.
Mwandishi wetu hakuishia hapo, alimtafuta shemeji wa mama mwenye nyumba aliyetajwa kwa jina moja la Jamal ambaye alikiri kutokea kwa ishu hiyo na kwamba suala hilo lilimalizika ambapo vyombo vya Wolper vilitolewa kwa ajili ya kufanya usafi kwani kuna mtu mwingine alikuwa akihamia.
Mjumbe wa Nyumba
Kumi, Musa alipotafutwa kwenye simu yake ya kiganjani ili kuzungumzia
sakata hilo alikiri kufikishiwa malalamiko ya Wolper.
Alisema kuwa msanii huyo alikuwa hajamaliza kulipa fedha, akawatuma ndugu zake wakachukue vitu vyake lakini kabla hawajavichukua mama mwenye nyumba aliwazuia mpaka alipwe chake na alipotimiza hilo ndipo akaachiwa vitu vyake.
Alisema kuwa msanii huyo alikuwa hajamaliza kulipa fedha, akawatuma ndugu zake wakachukue vitu vyake lakini kabla hawajavichukua mama mwenye nyumba aliwazuia mpaka alipwe chake na alipotimiza hilo ndipo akaachiwa vitu vyake.
CHANZO GLOBAL PUBLISHERS
No comments:
Post a Comment