Napenda uigizaji.
Nilikuwa mwigizaji nikiwa shule lakini nikaachia huko huko kwani enzi zetu mambo ya kuigiza hata katika redio wakati huo tulikuwa tunaona ni kazi ya watu wasio na elimu kubwa. Naamini tumeendelea hivyo mpaka sasa.
Nilikuwa mwigizaji nikiwa shule lakini nikaachia huko huko kwani enzi zetu mambo ya kuigiza hata katika redio wakati huo tulikuwa tunaona ni kazi ya watu wasio na elimu kubwa. Naamini tumeendelea hivyo mpaka sasa.
Watu wengine wanasomea masuala ya sanaa mpaka ngazi za juu za shahada ya kwanza hata zile za mizania lakini sijui ni wangapi wameamua kutumia elimu yao katika fani hii ya uigizaji.
Mapenzi yangu ya fani ya uigizaji yananifanya
niangalie sana filamu, vichekesho na maigizo mengine ya nchi nyingi
ulimwenguni kupitia televisheni, ‘DVD’, Mitandao n.k. Nalinganisha
uigizaji wetu na wa wenzetu naona bado tuko nyuma.
Ni ukweli uwezo wetu kifedha bado ni mdogo na najua kutengeneza filamu moja inahitaji fedha nyingi, lakini bado hata kile kidogo tunachokitengeneza ni hafifu.
Hadithi zinazofanana, vipengele (scenes) visivyo
na ujumbe wowote, n.k. vyote hivyo vinaonyesha kwamba safari yetu katika
fani hii inayopendwa bado ni ndefu.
Nayasema haya kama mtazamaji wala si mtaalamu wa uigizaji, nikitambua kwamba hahitaji mtu kuwa mpishi mzuri kutambua kwamba chakula kilichopikwa ni kitamu au la. Ndiyo maana katika makala haya nawaalika wataalamu katika fani hii kuingilia kati na kuinusuru.
Lazima nikiri kwamba watu wa nchi hii vipaji vya
kuigiza wanavyo, kwani wengi wao wanafanya shughuli hii kwa kupata
mafunzo kidogo tu tena kupitia kwa walimu ambao nao hawana utaalamu wa
kutosha.
Lazima tutambue kwamba dunia inakuwa kijiji, kwa ving’amuzi, mitandao, n.k watu tunapata fursa ya kuangalia filamu na maagizo mengine kutoka nchi za nje.
Si rahisi mtu aache kuangalia filamu toka nchi nyingine kwa sababu tu ya uzalendo.
Sasa starehe hailetwi na nadharia ya uzalendo bali
na kile kinachoburudisha bila kujali kinatoka kona gani ya dunia hii.
Hivyo hakuna ujanja katika hili.
Ni lazima waliopo kwenye fani hii watuletee kilicho bora toka kwenye hadithi, uandishi, mpangilio wa vipengele mbalimbali, uigizaji wenyewe na kila kitu kihusucho uigizaji. Hili linahitaji wale waliosomea fani hii hasa wale waliomaliza vyuo vikuu kuingilia kati.
Kuna wakati mwigizaji mmoja alisema kwamba fani
hii ina upungufu wa waandishi (script writers) na hiyo ni changamoto
kubwa sana kwao.
Tunawaomba watu hawa watumike katika kuandaa maandishi. Natambua kwamba itamaanisha gharama zaidi kwa wenye filamu zao, lakini kuna maana gani kuepuka gharama halafu mtu kuleta au kupeleka sokoni kitu ambacho hakina ladha? Hii habari ya ‘stori’ - Bwana X, ‘producer’ Bwana X, ‘script writer’ – Bwana X, ‘Director’ – Bwana X n.k. hazitatufikisha kokote.
Kama wenzetu waliotutangulia wanatambua uwezo wa watu tofauti katika nyanja hizo, kwa nini sisi tuone ni kazi inayoweza kufanywa na mtu yeyote ili mradi tu aweze kuigiza?
Elimu hii ikiongezwa na kipaji mtu katika uandishi kinakuja kutoa mwandishi mzuri ambaye akitutengenezea maandishi ya filamu yatatufanya tupate filamu nzuri sana.
Nakumbuka miaka iliyopita tulikuwa na akina Penina Mhando na wasomi waliobobea waliokuwa wanaandika michezo mbalimbali sasa tunahitaji watu wa aina hiyo wengi zaidi.
Wa kwetu wanashindwa kuonyesha hisia inayotakiwa, utakuta waigizaji wanawake tena waliobobea katika fani hii wakiwa wanaigiza kulia kwa uchungu na watazamaji tusiione hisia hiyo.
Hata mimi nakubaliana naye kwamba hii ni changamoto kubwa lakini
wataalamu katika uandishi wa uigizaji wanaweza kuikabili. Kuna watu
wamemaliza shahada zinazowawezesha kuwa waandishi wazuri tu wa filamu na
maagizo mengineyo.
Tunawaomba watu hawa watumike katika kuandaa maandishi. Natambua kwamba itamaanisha gharama zaidi kwa wenye filamu zao, lakini kuna maana gani kuepuka gharama halafu mtu kuleta au kupeleka sokoni kitu ambacho hakina ladha? Hii habari ya ‘stori’ - Bwana X, ‘producer’ Bwana X, ‘script writer’ – Bwana X, ‘Director’ – Bwana X n.k. hazitatufikisha kokote.
Kama wenzetu waliotutangulia wanatambua uwezo wa watu tofauti katika nyanja hizo, kwa nini sisi tuone ni kazi inayoweza kufanywa na mtu yeyote ili mradi tu aweze kuigiza?
Lazima tutambue kwamba uandishi ni taaluma
inayohitaji mtu kukaa mafunzoni kwa muda fulani na watu ambao wana elimu
na uzoefu mkubwa wa fani hiyo.
Elimu hii ikiongezwa na kipaji mtu katika uandishi kinakuja kutoa mwandishi mzuri ambaye akitutengenezea maandishi ya filamu yatatufanya tupate filamu nzuri sana.
Kama waigizaji wanataka kuandika wenyewe filamu
zao basi wakubali pia kuingia shule kwa ajili ya hiyo. Lakini bado
watambue kwamba kuna suala la kipaji katika hilo.
Licha ya elimu na kipaji kuna suala la muda. Mtu
kujibebesha majukumu mengi kunaweza kumsababishia kutokuwa na ufanisi
kwenye majukumu yote aliyojibebesha.
Nakumbuka miaka iliyopita tulikuwa na akina Penina Mhando na wasomi waliobobea waliokuwa wanaandika michezo mbalimbali sasa tunahitaji watu wa aina hiyo wengi zaidi.
Tukiacha suala la uandishi, tunahitaji pia
waigizaji wenye uelewa wa juu wa kile wanachokifanya. Mimi hupenda
kuangalia ‘Isidingo’ na kitu kimoja kinachonifurahisha katika ‘Isidingo’
ni uigizaji unaoonekana kama ni halisia.
Wa kwetu wanashindwa kuonyesha hisia inayotakiwa, utakuta waigizaji wanawake tena waliobobea katika fani hii wakiwa wanaigiza kulia kwa uchungu na watazamaji tusiione hisia hiyo.
Huu ni udhaifu katika uigizaji. Wale tunaowaona
wanaigiza kwa umahiri huo niusemao ni kwamba wanakuwa pia wana elimu ya
kiwango kinachoridhisha.
Tuangalie wa kwetu na elimu zao, hakika elimu zao
ni za chini na upeo wao mdogo katika fani hii. Wengi wanafikiria kwamba
kuigiza hakuhitaji mtu kusoma, na uthibitisho ni wale wanaoacha shule
wakikimbilia kwenye uigizaji kwani kwa mawazo yao kwamba katika kuigiza
kunawezekana hata kama huna elimu. Huko ni kujidanganya.

No comments:
Post a Comment