Morogoro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Hawa Ghasia amewaagiza makatibu tawala na wakurugenzi wa halmashauri nchini kusimamia fedha za umma kwa uaminifu na kurejesha imani kwa wananchi na Serikali na kusoma taarifa ya mapato na matumizi kila baada ya miezi mitatu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Hawa Ghasia amewaagiza makatibu tawala na wakurugenzi wa halmashauri nchini kusimamia fedha za umma kwa uaminifu na kurejesha imani kwa wananchi na Serikali na kusoma taarifa ya mapato na matumizi kila baada ya miezi mitatu.
Ghasia aliyasema hayo mkoani Morogoro wakati
akifunga mafunzo ya siku nne ya wakurugenzi na makatibu tawala wote
nchini mkoani Morogoro.
Alisema wakurugenzi na makatibu tawala wanatakiwa kubeba dhamana kwa niaba ya Serikali na kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo yanayotakiwa.
Alisema makatibu tawala na wakurugenzi kwa kila
mkoa wanatakiwa kuandaa utaratibu wa kutoa ajira kwa wanawake na vijana
wamachinga baada ya kutumia nguvu kuwaondoa katika maeneo yao ya
bihashara .
Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Jumanne Sagini alisema lengo la mkutano huo lilikuwa kuwakumbusha washiriki husika malengo ya kazi na uzoefu wa kazi kwa wakurugenzi wapya katika kusimamia rasilimali fedha na watu.
Alisema mkutano huo utawewezasha kubadilishana
uzoefu wa kazi ili waweze kufanya kazi kwa ushirikiano na kutimiza ahadi
walizopewa na wananchi
No comments:
Post a Comment