EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 9, 2013

DUH! MASTAA WAUMBUKA MWALIKO WA BONGO MUVI KWENDA IKULU.


DUH! Ule mwaliko wa wasanii wa Bongo Muvi kwenda Ikulu kwenye futari kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, umeota mbawa baada ya kuambiwa ‘msije’ hivyo kusababisha baadhi ya mastaa waliokusanyika kuumbuka.
 
Ishu hiyo ilitokea mwanzoni mwa wiki hii ambapo mastaa hao walipata mwaliko huo wa kutakiwa kwenda Ikulu kufuturu na JK baada ya wale wa Bongo Fleva.

UJIO WA CLINTON
Habari zilidadavua kuwa chanzo cha kutoswa kwa mastaa hao ni kufuatia ujio wa Rais Mstaafu wa 42 wa Marekani, Bill Clinton.
Wakiwa tayari wamelipuka ‘madela’ na ‘makanzu’ kwa ajili ya kwenda kugonga mnuso na ‘mkubwa’ na kuzungumza naye, ghafla mambo yalibadilika na kujikuta wakiwa wamenunaje?
Mastaa wakiwa wamepigwa butwaa baada ya mwaliko kuota mbawa.
WAKOPA MADELA, KANZU
Habari za chini ya kapeti zilidai kuwa baadhi ya mastaa hao walikuwa wamekopa madela na makanzu hivyo kusitishwa kwa mwaliko huo kuliwauma kupita maelezo kwani walikuwa tayari kwa kuuza sura na JK.
Huku Ijumaa likiwachabo kila ‘step’, mastaa hao walikubaliana kukutana pamoja kwenye Viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar kwa ajili ya kuanza safari ya kuelekea Ikulu huku kila mmoja akisisitizwa kuwa ‘smati’.
 
Kwa upande wa mastaa wa kiume walinunua na wengine kukopa kanzu za gharama huku upande wa wanawake wakiwa wametinga madela yao maalum ya gharama tayari kwenda kupata futari ‘White house’.

KIKAO CHA DHARURA
Wakiwa wamekusanyika viwanjani hapo kama wanavyoonekana pichani, ilipofiki saa 11:30 jioni, aliyekuwa Katibu wa Bongo Movie, Salum Mchoma Chiki ghafla alisimama na kuwaomba wasanii wasogee kwa pamoja kwani kulikuwa na kikao cha dharura.

WAKATWA MAINI
Walipokusanyika, Chiki alipaza sauti na kusema: “Jamani tuliokuwa tunakwenda kwa Mheshimiwa Rais  kwa ajili ya kufuturu, safari hiyo haipo tena kama tulivyokuwa tumejuzana.”
Kauli hiyo iliwakata maini mastaa hao ambao wote walionekana kunywea huku wakitia huruma.
Chiki aliendelea: “Safari yetu imekatishwa na ugeni alioupata Mheshimiwa Rais lakini bado tutajulishwa ni siku gani ya kwenda kufuturu naye.”
Maneno ya Chiki yaliendelea kuwasononesha wasanii hao huku wengine wakiangua kicheko, kila mmoja akimuangalia mwenzake alivyojipigilia nguo za maana.

STEVE NYERERE
Komediani Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ aliweka maneno ya utani kwa kusema kwa wale waliojitundika dela lakini halikumkaa vizuri au kama alikopa na hajalipa, ndiyo ulikuwa muda mzuri wa kujipanga zaidi hivyo wasisononeke.

WATIWA MOYO
Alisema: “Jamani kama mlibandika madela, msijali kabisa huu ndiyo muda muafaka wa kujipanga zaidi na kulipa madeni ambayo mlikuwa nayo kutokana na viwalo mlivyovaa leo.”

LULU, MAMA KANUMBA
Baadhi ya mastaa ambao walionekana kujipigilia na kupendeza tayari kwa kwenda Ikulu kabla ya mambo ‘kuharibika’ ni pamoja na Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye alitimba na mama wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa.
Jacob Steven ‘Jb’, Mohamed Nice ’Mtunisi’ na Ben Kinyaiya wakiwa wametinga makanzu mapya nao walikuwa wamelipuka vilivyo.

WAONDOKA WAKIWA WAMENUNA
Baada ya taarifa hiyo chungu kwa mastaa hao, kila mmoja aliondoka viwanjani hapo akiwa amenyong’onyea.
Badala ya Jumamosi, kuna habari kuwa walitakiwa waende siku inayofuatia (Jumapili) lakini nayo ikashindikana na kusemekana itakuwa Jumatatu ambayo nayo pia hawakwenda hadi ratiba za kufuturisha Ikulu zikamalizika, wakipewa moyo kwamba labda itakuwa mwakani.
CHANZO CHA HABARI NI GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate