EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 9, 2013

MAUAJI YA BILIONEA ARUSHA…

MAUAJI ya bilionea ambaye ni mfanyabiashara mkubwa wa madini ya Tanzanite huko Mererani mkoani Arusha, Erasto Msuya aliyeuawa kwa kumiminiwa risasi kibao juzi, yamesababisha kutanda kwa hofu jijini hapa.
 
Mwili wa Msuya ukiwa ndani ya difenda.
Tukio hilo lililojiri maeneo ya KIA alipokuwa akitokea Mererani kuelekea Moshi, Kilimanjaro limeacha maswali mengi ambayo yanahitaji majibu.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa, bilionea huyo anayemiliki Hoteli ya SG Resort iliyopo Sakina jijini hapa alipigiwa simu akielezwa kuwa kuna biashara ya kufanya Moshi lakini kabla ya kufika alivamiwa njiani.

Ilidaiwa kuwa Erasto aliuawa akiwa na gari lake jipya aina ya Range Rover Voque la 2013 alilonunua hivi karibu kwa dola za Kimarekani 250,000 (zaidi ya Sh. milioni 400 za Kitanzania).
 
Wanausalama wakiubeba mwili wa marehemu Msuya.
Habari za kiuchunguzi zilibaini kuwa kuna vitu vingi nyuma ya mauaji hayo huku suala visasi vya kibiashara likipewa kipaumbele.
 
“Kuna jamaa mwingine aliuawa juzikati kule Mererani, walikuwa wakifanya biashara na Erasto hivyo inawezekana ikawa ni kisasi katika mambo ya biashara ya madini.


“Unajua hii biashara ni ya kuvizianaviziana sana kwa hiyo itakuwa ni njama kwa sababu kuna watu wanadai wakati anaondoka Mererani alikuwa ameshanunua mzigo mkubwa.

“Pia inawezekana kweli ni majambazi ambao walijua kabisa Erasto ana mzigo ndiyo maana wakamfanyizia na kuchukua mzigo.
 
“Hii inaonesha kuna aina fulani ya utekaji na majibizano ya risasi kwa sababu tukio lenyewe limefanyika nje ya barabara, porini kabisa na gari linaonekana limepaki kwa utaratibu wa kawaida bila vurugu ‘so’ kwa vyovyote ni ishu iliyopangwa,” alisema mmoja wa wafanyabiashara wa madini aliyefika eneo la tukio.
Mwili wa Erasto Msuya (kulia) baada ya kupigwa risasi. Kushoto ni gari lake.
Uchunguzi mwingine uliibuka na madai kuwa huenda kuna visasi vya kimapenzi lakini kuvizungumzia inakuwa ngumu kwa sababu ya kukosekana kwa ushahidi wa moja kwa moja.

“Mimi nakwambia tusubiri, mauaji haya yataibua mambo mengi sana kwa sababu ndani ya kipindi kifupi kumetokea vifo vya vijana matajiri wenye umri mdogo kati ya 37 na 40.
“Ukihesabu sasa hivi wanafika matajiri kama watano na wote walikuwa ni ‘kampani’ moja.
 
“Alianza Wakili Mawala aliyejirusha gorofani Nairobi, Kenya. Akafuatia Henry Nyiti, akaja Babu Sameke, akafuatia yule jamaa aliyejirusha gorofani Kariakoo na yule mwingine aliyepigwa risasi kule Masaki, Dar.

“Sasa Erasto naye ameuawa. Kwa vyovyote kuna kitu. Kama siyo mambo ya kulogana, basi kuna kitu waligusa,” alisema jamaa mwingine anayewajua vizuri wafanyabiashara wa madini Arusha.
 
Habari zinadai kuwa baadhi ya matajiri wamepanga kulikimbia jiji hilo kutokana na hofu juu ya maisha yao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alipotafutwa na gazeti hili, simu yake iliita bila kupokelewa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate