EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, August 8, 2013

KUTANA NA MASTAA… UCHUMBA 100%, NDOA 0%.

...WALIANZA UHUSIANO WA KIMAPENZI TANGU MWAKA 2000 WAKATI HUO ISABELA AKIWA KIDATO CHA PILI HIVYO KUUFANYA...
NDOA ni matokeo mazuri ya uchumba. Ili mtu ufikie kwenye ndoa lazima upitie katika hatua ya uchumba lakini kwenye uchumba huo, watu hutofautiana.
Wapo wanaoudumu kwa muda mrefu bila ndoa lakini wapo ambao hawachukui hata mwaka kwenye uchumba, wanaoana.
 
Ukilinganisha wale wanaodumu kwa mwaka mmoja wa uchumba, wale wa zaidi ya miaka mitatu watakuwa wanaleta tafsiri rahisi kwamba uchumba wao umeshiba asilimia mia moja lakini wanakuwa hawaamui kuoana.
Leo katika makala haya tunawachambua baadhi ya mastaa ambao wamedumu kwa zaidi ya miaka mitatu bila ndoa, baadhi yao wamefikia hadi hatua ya kuzaa kabla ya ndoa.

ROSE NDAUKA & MALIKI BANDAWE
Rose ni msanii wa filamu Bongo. Wawili hawa ni wachumba wa muda mrefu, zaidi ya miaka mitatu tangu walipoanza kusema watafunga ndoa. Hadi sasa hakuna ndoa, wanaogelea katika uhusiano wa kimapenzi kwa kuishi pamoja.

RACHEL HAULE ‘RECHO’ &   GEORGE SAGUDA
Msanii huyu wa filamu za Kibongo na mchumba wake ambaye huwa anakaa nyuma ya kamera kama muongozaji huku akiwa anapiga mzigo TRA, wamedumu kwenye uhusiano kwa miaka mitano ambapo kwa mujibu wa Recho hakuna hata mpango wa ndoa, bado sana.
Wawili hao wanaishi pamoja kama mke na mume.

SHAMSA FORD & DICKSON
Wawili hawa wamedumu kwenye uchumba kwa takriban miaka minne sasa. Katika uchumba wao wamejaliwa kupata mtoto mmoja. Hivi karibuni Shamsa alitangaza kuwa lazima wafunge ndoa ndani ya mwaka huu lakini kabla ya hapo, alikuwa amekataa katakata suala la ndoa.

ISABELA MPANDA & LUTENI KALAMA
Isabela ni msanii wa filamu na muziki pia, aliwahi kushikilia Taji la Miss Ruvuma. Kalama ni msanii wa muziki wa kizazi kipya. Wawili hawa wanaongoza kwa kudumu, walianza uhusiano wa kimapenzi tangu mwaka 2000 wakati huo Isabela akiwa kidato cha pili hivyo kuufanya uhusiano wao udumu kwa takriban miaka 13.
Pamoja na kukaa katika uhusiano kwa miaka yote hiyo, suala la ndoa bado halijulikani kwani kila mara wamekuwa wakitangaza kuoana lakini ahadi haitimii.
ELIAS BARNABA ‘BARNABA’ & ZUBEDA
Barnaba ni mwanamuziki wa Bongo Fleva yeye na Zubeda (Mama Steve) ni mtu na mzazi mwenzake kwani wamejaliwa kupata mtoto mmoja, Steve.
Wawili hawa wamedumu kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa miaka minne sasa lakini suala la ndoa hawajawahi kulizungumzia, wapenzi hawa waliunganishwa na msanii wa filamu, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ ikiwa ni baada ya Barnaba kumkuta Zubeda nyumbani kwa Aunty Lulu.

EMMANUEL ELIBARIKI ‘NAY WA MITEGO’ & SIWEMA
Nay wa Mitego ni msanii wa Bongo Fleva. Msanii huyo amedumu kwenye uhusiano wa kimapenzi na mchumba wake Siwema kwa zaidi ya miaka mitatu.
Hivi karibuni wawili hawa walipatwa na tatizo baada ya ujauzito aliokuwa nao Siwema kutoka, suala la kufunga ndoa bado halieleweki.

HERRY SAMIR ‘MR BLUE’ & WAHIDA
Mr Blue staa wa Bongo Fleva na Wahida ni wapenzi wa muda mrefu na uhusiano wao kwenye vyombo vya habari una zaidi ya miaka miwili, imedaiwa kabla ya hapo pia walishakaa miaka kadhaa.
Wawili hao wamejaliwa kuwa na mtoto mmoja lakini mpaka sasa hawajatoa muafaka wa kufunga ndoa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate