EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, August 8, 2013

MALI ZA BALALI ZAIBUA BALAA


FAMILIA ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, marehemu Daudi Balali imeingia katika mgogoro baada ya baadhi ya ndugu kudaiwa kugombania mashamba aliyoyaacha marehemu huyo, Amani linakupa ‘ei tu zedi’.


Mgogoro huo ulianza mara tu baada ya Balali kufariki dunia nchini Marekani, Mei 16, 2008.
Kwa mujibu wa chanzo, ndugu hao wanadaiwa kugombania mashamba hayo yaliyopo Bunju kwa Jeshi, jijini Dar es Salaam.
 

Deodatha Elius, ndugu wa marehemu, anadai shamba lake lenye ukubwa wa ekari sita limeuzwa bila yeye kuwa na taarifa.
 

Alisema eneo hilo alinunuliwa na Balali lakini bahati mbaya hakuwa na hati. Alidai kwamba yeye na Balali ni mtu na binamu yake.

Akizungumza na waandishi wetu juzikati huko Bunju, mwanamke huyo ambaye ni mjane, alisema kuwa kabla ya kuolewa alikulia mikononi mwa marehemu Balali, baada ya kupata mume aliondoka kwenda kuanza maisha mapya.

Alidai baada ya kufiwa na mume mwaka 1997, Balali alimwambia atafute eneo ili amnunulie aweze kuishi na watoto wake watatu aliowapata na marehemu mume wake.

“Nilianza kutafuta eneo, nikapata Bunju kwa Jeshi, kaka Balali akaninunulia eneo hilo kipande kidogo na palikuwa na kibanda cha kuishi. Baadaye kidogo nikapata eneo jingine jirani likiwa na nyumba nzuri, kaka akaninunulia nikawa na ekari sita,” alisema mwanamke huyo.

Alisema alishangaa baada ya kifo cha Balali ndugu zake walichukua jukumu la kuuza shamba lake hilo lenye nyumba bila kumwambia na wanunuzi kumtaka aondoke.
 

“Kabla Balali hajafariki dunia, hizi fujo hazikuwepo na waliouza eneo hilo ninawajua ni ndugu zetu wa karibu, wamefanya hivyo kwa lengo la kunikomoa,” alisema.
Pia aliziomba taasisi za haki za binadamu kumsaidia ili aweze kuishi na watoto wake kwa raha.
 

Aliongeza kusema kuwa wakati wa uhai wake, marehemu alihakikisha kila mtu anamsaidia na hata hao ndugu waliouza eneo hilo walipewa maeneo yao.

Baadhi ya majirani wanaofahamu sakata hilo walidai wanaomchezea mchezo mchafu ni ndugu zake wa karibu, kitendo ambacho walisema kinasikitisha.
 

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina gazetini, mkazi mmoja wa eneo hilo alidai kuwa, marehemu Balali aliwahi kuwaita na kuwaambia kuwa eneo hilo amemnunulia dada yake huyo.

“Ukweli ni kwamba baadhi ya ndugu waache tamaa za mali, wamuache mjane alee watoto wake kama alivyoachiwa eneo hili na kaka yake,” alisema jirani huyo.
 

Naye mjumbe mstaafu wa Shina Namba 41, Bunju ‘A’ Kilungule, Said Salum ambaye kwa wakati huo  alikuwa anajua mipaka ya wenyeji alisema eneo hilo lilikuwa linakaliwa na watu watatu tofauti, hao wote walimuuzia Balali naye akamkabidhi mwanamke huyo kwa kuwaambia asitokee mtu wa kumnyang’anya.

“Kuanzia hapo mama huyo alianza kuishi hapa na kufanyia usafi eneo ambalo lina ukubwa wa ekari sita, sasa tunashangaa kuona mama huyu akipata usumbufu,” alisema mjumbe huyo.
 

Amani lilifanikiwa kumpata mtu aliyekuwa msimamizi wa mali za Balali kwa wakati huo hadi sasa aliyejitambulisha kwa jina la Bernard Balinzako ambapo alisema:

“Mimi nilikuwa msimamizi wa shughuli za Balali, kweli Deodatha  ni mmoja ya ndugu wa marehemu. Ninachokifahamu mimi ni kuwa eneo lilinunuliwa na Balali kama alimkabidhi huyo dada sijui.”
 

Alisema muuzaji wa eneo hilo ni msimamizi wa mirathi ya marehemu huyo ambaye hakumtaja jina lakini alisema ni dada wa Balali.
CREDIT GLP

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate