Daktari wa rais Kikwete, Profesa Mohammed Y. Janabi.
 Profesa
 Mohammed Y. Janabi, Daktari wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefanikiwa kuingia katika kundi dogo 
la madaktari wa Afrika waliothibitisha kuwa na ujuzi na utaalam wa 
kuwapima na kutoa liseni za vipimo vya afya kwa watumishi wa anga 
wakiwamo marubani.
Profesa
 Mohammed Y. Janabi, Daktari wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefanikiwa kuingia katika kundi dogo 
la madaktari wa Afrika waliothibitisha kuwa na ujuzi na utaalam wa 
kuwapima na kutoa liseni za vipimo vya afya kwa watumishi wa anga 
wakiwamo marubani.
Katika barua ambayo aliipokea Dkt. Janabi wakati anaandamana na Rais 
Kikwete katika ziara ya kikazi ya Marekani na Canada iliyomalizika  
Jumamosi, Septemba 28, 2013, Wizara ya Usafirishaji ya Marekani kupitia 
Utawala wa Shughuli za Anga wa Marekani (FAA) imesema kuwa imemteua 
Profesa na Dkt. Janabi kuwa Daktari wa Shughuli za Anga (AME) kuanzia 
Agosti 14, mwaka huu, 2013.
“Uamuzi huu una maana kuwa sasa unaweza kuwapima na kuendesha 
shughuli za kitibabu na kutoa ama kukataa kutoa liseni ya kuthibtisha 
afya za watumishi wa sekta ya anga wakiwemo marubani wa ndege za 
usafirishaji, wa ndege za biashara za abiria, marubani wa ndege binafsi 
na marubani wanafunzi.
Profesa Janabi anakuwa daktari wa 31 katika Afrika na wa tatu katika 
Afrika Mashariki kupatiwa hadhi hiyo ambayo inapatikana baada ya kazi 
ngumu ambayo ni pamoja na kufanya mtihani maalum.
Nchi pekee katika Afrika Mashariki iliyokuwa na madaktari wa kiwango 
hicho kabla ya Dkt. Janabi kuingia katika kundi hilo ni Kenya yenye 
madaktari wawili. Tanzania sasa inakuwa nchi ya pili katika Afrika 
Mashariki kuwa na hadhi hiyo.
Kwa upande wa Afrika, Profesa Janabi anaungana na madaktari kutoka 
Burkina Faso (1), Cameroun (2), Misri (6) ambayo ndiyo madaktari wengi 
zaidi katika kundi hili, Ghana (1), Libya (1), Morocco (1), Nigeria (5),
 Ethiopia (4), Kenya (2), Afrika Kusini (5) kukubaliwa kuifanya kazi hii
 ya kimataifa.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
29 Septemba, 2013
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
29 Septemba, 2013
 
 
 
 
 
 
 

 
No comments:
Post a Comment