EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, September 3, 2013

Majambazi wachezea JWTZ, Polisi..Kombati za jeshi, mihuri 27, leseni vyanaswa

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kukutwa na vifaa mbalimbali vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Polisi kinyume cha sheria za nchi.

Tukio hilo limekuja wakati ambapo matukio ya ujambazi yameshamiri nchini huku watuhumiwa wa ujambazi wakitumia sare na silaha za majeshi hayo kufanikisha mikakati yao.

Akizungumzia kukamatwa kwa watuhumiwa hao jana, Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema kuwa Agosti 31, mwaka huu, saa 4:00 asubuhi maeneo ya Mwasonga Kigamboni alikamatwa Saida Mohamed (30) akiwa na vifaa vya JWTZ.

Kamishna Kova alisema kuwa Saida alikamatwa na askari waliokuwa doria akiwa na suruali saba za kombati za JWTZ, mashati saba, kofia 10 za kombati, na viatu jozi tatu.

Alivitaja vitu vingine kuwa ni ponjoo moja, koti, begi la kuweka nguo za jeshi, shati mbili nyepesi, fulana, kofia aina ya bareti, cheo kimoja cha koplo na mikanda miwili.
Kamishna Kova aliongeza kuwa katika tukio jingine, mkazi mmoja wa Gongo la Mboto, Hussein Mkondoa (25) alikamatwa na kofia ya sare ya Jeshi la Polisi.
Alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Septemba mosi mwaka huu akiendesha pikipiki akiwa amevalia kofia hiyo iliyopauka nembo.

Kova aliwataka wale wote wenye sare za majeshi wazisalimishe kwani msako huu unaendelea.

Alisema pamoja na kubadilisha uongozi katika Kituo cha Ubungo, jeshi limejipanga vema kukabiliana na utapeli eneo hilo ambalo watu hujifanya askari.
Katika kamata kamata hiyo, ndugu wawili Shadrack Mwangwi (27) na Mwangwi Samweli (38) wanashikiliwa kwa kosa la utapeli.

Kova alisema kuwa watu hao walikamatwa na mihuri 27 ya idara mbalimbali za serikali na taasisi, kumbukumbu za Jeshi la Polisi, vitabu vya mapato, namba za usajili wa magari, leseni za biashara, bima na karatasi za ukaguzi wa magari.
Fastjet wanusurika
Katika tukio jingine, Kamishna Kova alisema watu wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kula njama na kujaribu kufanya tukio la uporaji katika Kampuni ya Ndege ya Fastjet.

Alisema kuwa tukio hilo limehusisha mmoja wa wafanyakazi, Enea Dawson (29) ambaye alikuwa anawasiliana na majambazi hao kwa njia ya simu.
Kova aliwataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni Issa Karimu (40), mkazi wa Buguruni, Paulo Baltazary (38) mkazi wa Buza na Rajabu Shaaban (40).

Alisema kuwa Agosti 30, mwaka huu, Mtaa wa Samora katika ofisi za shirika hilo, watuhumiwa hao walikamatwa baada ya kuwa na mawasiliano na Enea, ambaye ni tarishi aliyekuwa akiwapa taarifa zote za fedha katika kampuni hiyo.

“Baada ya kuwakamata majambazi hao polisi walifuatilia namba ya simu waliyokuwa wakiwasiliana nayo ambayo iliita huku sauti ikitokea sehemu za siri katika nguo za mtumishi huyo,” alisema.

Kova alisema kuwa katika tukio hilo fedha zaidi ya sh milioni 60 zilizokuwa ziibiwe ziliokolewa.
Alisema kuwa pia walikamata dawa za kulevya aina ya bangi kete 805, puli 56, misokoto 196 na gongo lita 330, ambapo watuhumiwa 120 wanashikiliwa na jeshi hilo.
CHANZO CHA HABARI TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate