EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, September 3, 2013

TAZARA bado kugumu.. hali Bado tete.

WAKATI hali ikiwa tete wafanyakazi wa Mamlaka ya Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) wanaoendelea na mgomo wa kusotea malipo yao, suala hilo jana lilitinga bungeni na kuibua tafrani kubwa.

Akizungumza Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu) Kanda ya Dar es Salaam, Theresia Mahagatila, alithibitisha kuendelea kwa mgomo huo kutokana na uongozi wa TAZARA kuwadanganya wafanyakazi.

Licha ya TAZARA kuahidi kulipa malimbikizo hayo ya mshahara ya miezi minne ifikapo Agosti 29 mwaka huu, ahadi hiyo imeota mbawa na badala yake imelipa mshahara wa mwezi wa tano pekee.

“Sisi tulifika ofisini tayari kwa kazi siku hiyo kama walivyotangaza kwenye vyombo vya habari, cha kushangaza tumelipwa mshahara wa mwezi wa tano tu na waliolipwa ni baadhi yetu,” alisema.

 Makuu ya TAZARA jana na kukuta wafanyakazi hao wakiwa kwenye makundi huku huduma zote zikiwa zimesimama.

Wakati hali ikiwa hivyo TAZARA, mjini Dodoma, Bunge nusura zisimame baada ya mbunge wa Viti Maalum, Suzan Kiwanga (CHADEMA), kutaka shughuli zisitishwe ili lijadili kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi hao.

Kiwanga alibainisha kuwa kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi hao kunawafanya baadhi ya wananchi hususan wa mikoa ya Kusini kujawa na hofu ya reli hiyo kuhujumiwa na hivyo uchumi wa mikoa hiyo kutetereka.

Mbunge huyo mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, aliomba mwongozo wa Spika kwa mujibu wa Kanuni za Bunge kifungu cha 47 (1) na 48 inayolitaka Bunge kusitisha shughuli zake ili kujadili jambo zito litakalowasilishwa na mbunge.

Kiwanga alibainisha kuwa kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi hao kumemfanya asipate usingizi na familia zaidi ya 9,000 zimeathirika.

Alisema kuwa alipigiwa simu nyingi na wananchi baada ya wafanyakazi 1,500 wa TAZARA kufukuzwa wakihofia uchumi wao kuporomoka.

“Ninaliomba Bunge liahirishe shughuli zake ili lijadili jambo la TAZARA kwa kuwa linagusa maslahi ya wananchi wengi.
“Hivi jamani tuwe wakweli tungefanyaje kama sisi wabunge tungekuwa hatujalipwa mishahara yetu kwa miezi minne, tungekubali?” alihoji.

Kiwanga alibainisha kuwa anashangazwa na hatua zilizochuliwa na menejimenti ya TAZARA (Tanzania) kuwafukuza kazi wafanyakazi wake wakati wenzao wa Zambia waliwalipa wafanyakazi wao waliogoma kwa siku nne.
Mbunge huyo alihoji kwa nini serikali ya Tanzania ina kigugumizi cha kuzungumzia jambo hilo au kutekeleza mahitaji ya wafanyakazi.

“Zambia waligoma kwa muda wa siku nne na walitimiziwa stahiki zao lakini Tanzania hali imekuwa sivyo, inasuasua kwenye suala hilo linaloweza kusababisha uchumi wa nchi kuporomoka kutokana na athari za mgomo huu, kwa nini tumefikia hapa?” alisisitiza.
Baada ya Kiwanga kumaliza kuomba mwongozo huo, Naibu Spika Ndugai, alimtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, kutoa ufafanuzi kuhusu sakata hilo.
Lukuvi alisema kuwa menejimenti ya TAZARA imefuta uamuzi wa kufukuzwa kwa wafanyakazi hao na serikali itatoa taarifa bungeni kulingana na nafasi ya Bunge.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate