EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 27, 2013

MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU MWANAMKE ALIYEONGOZA UGAIDI KENYA.

Mwanamke anayedaiwa kuongoza ugaidi Westgate, Samantha Lewthwaite.
Na Mwandishi wetu:
TUKIO kubwa la kigaidi lililotokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika jengo la maduka makubwa na ya bei mbaya jijini Nairobi la Westgate, limeelezwa kuwa liliongozwa na mwanamke raia wa Uingereza, Samantha Lewthwaite.
Yafuatayo ni mambo kumi usiyoyajua juu yake.
1. Samantha, mwenye umri wa miaka 29, ni mzaliwa wa Buckinghamshire, Uingereza anayeelezewa na magaidi wa kundi la Al Shabaab kama mwanamke mwenye akili nyingi, akiwa ni mama wa watoto watatu ambaye alikata mawasiliano na familia yake baada ya kuhamia Kenya mwaka 2007.

2. Ripoti za kipolisi zinaonesha kuwa ni mkufunzi wa wanawake wa kikundi hicho cha kigaidi wanaochukua mafunzo ya jihad, mke wa zamani wa Germaine Lindsay, ambaye alijiua baada ya kuhusika na shambulio la bomu kwenye treni ya chini ya ardhi jijini London, Julai 7, 2005.

3. Kwa mujibu wa nyaraka mbalimbali zinazoaminika kuwa ni zake, ambazo zilitangazwa na Gazeti la Daily Mail la Uingereza, mwanamke huyo anawalea watoto wake ili waje kuwa wanaharakati wa imani kali. Mumewe wa pili, Habib Saleh Ghani naye ilidaiwa kuwa aliuawa kwenye tukio lingine la ugaidi.

4. Baadhi ya nyaraka zinaonesha kuwa katika baadhi ya mawasiliano na mumewe, aliwahi kusema: “Ghani alizungumza na kijana wangu wa miaka nane na binti yangu wa miaka mitano akiwauliza wanachotaka kuja kufanya wakiwa wakubwa, wana majibu mengi lakini wote wanakubaliana kwamba watakuja kuwa Mujahidina.

5.  Ni mtaalamu wa kutengeneza vifaa vya kuficha sura, pua na kichwa, akiachana na taaluma yake ya zamani ya ubunifu wa mitindo ya mavazi ambayo sasa anashona yanayovaliwa na Waislamu, kazi aliyoianza akiwa chini ya uangalizi wa magaidi hao wakati akiishi Mombasa nchini Kenya.

6. Anahisiwa kuwa ndiye aliyetupa guruneti katika baa iliyokuwa imejaa mashabiki wa soka wakitazama mechi za Euro mwaka 2012 katika mechi kati ya England na Italia nchini Uganda Juni 24 na kuua watu watatu, akiwemo mtoto aliyekuwa na umri wa miaka mitatu. Isack Simiyu, (23), aliyekuwa nje ya Jericho Bar, alisema shambulio hilo lilifanywa na mwanamke wa kizungu aliyejifunga kitambaa cheusi kichwani. Alidai kumuona vizuri mlipuaji huyo na polisi walipompa picha nne za wanawake wa kizungu ili aone kama mlipuaji alikuwa mmojawapo, aliichagua ya Samantha.

7. Ni gaidi wa kike anayetisha zaidi kwa sasa tokea alipoondoka Ulrike Meinhof, mwanzilishi wa Kundi la Red Army ambalo lilihusika na milipuko ya mabomu katika Ujerumani Magharibi kwenye miaka ya 1970.

8. Alipokimbia katika nyumba aliyokuwa amepanga mjini Mombasa, polisi walikuta kitabu kidogo cha kumbukumbu akiwa ameandika kuwa anataka watoto wake waje kuwa wakujitoa mhanga. Pia walikuwa na bunduki za kisasa, risasi, pamoja na mapipa ya kemikali yanayotumiwa na wanaojilipua.

9. Akiwa na jina la Kiislamu la Asmaa Shahidah Bint-Andrews, kijana wake wa kiume, Abdur-Rahman Faheem Jamal, alizaliwa katika Hospitali ya Stoke Mandeville mwaka 2009. Katika cheti cha kuzaliwa cha mwanae, hakuna jina la baba lililoandikwa. Alislimu akiwa na miaka 18, akiachana na uvaaji wa jeans na Tisheti na badala yake akivaa mavazi ya Kiislamu, ikiwemo hijab.

10. Alisoma masomo ya dini na siasa katika shule iitwayo Oriental and African Studies huko Russell Square, London, umbali wa mtupo wa jiwe kutoka pale mumewe alipojiua kwa kujilipua.
CREDIT GLP

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate