EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 26, 2013

ATEMBEZWA UCHI MTAANI BAADA YA KUFUMANIWA NA MKE WA MTU CHUMBANI

WANASEMA za mwizi arobaini, ikiongezeka moja mshukuru Mungu! Novemba 16, mwaka huu ilikuwa siku ya aibu kwa bosi Hussein Shaban (35) kufuatia kudaiwa kufumaniwa katika nyumba ya kiongozi mmoja wa Chama cha Mapinduzi (CCM) huko Tegeta jijini Dar es Salaam.
Hussein Shaban akiwa amevuliwa nguo na kupewa kichapo baada ya fumanizi.
Sakata hilo la aina yake lilitokea katika kitongoji cha Nyeishozi, Tegeta kwa kumuhusisha Hussein ambaye ni mfanyabiashara  na mke wa kigogo huyo ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sasa.
CHANZO CHA FUMANIZI, KUTOWEKA AMANI
Akisimulia tukio zima mwanzo hadi mwisho, kiongozi huyo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema miezi miwili iliyopita alianza kuhisi ndani ya ndoa yake kuna jambo lanaloendelea kwa siri baada ya nyumba yake kupoteza amani, mke alibadilika tabia ghafla.

Bwana Hussein akitembezwa mitaani.
“Siku moja nilikuwa natafuta nyaraka za kazini ambazo nilikuwa nimeziweka kwenye begi la kubebea kompyuta mpakato (laptop), lakini sikuzikuta.
“Niligundua vitu vyangu vingi havipo ndani kama vile mashati, suruali, redio ndogo na saa ya ukutani. Nilimuuliza mke wangu akanipa majibu rahisi.
UCHUNGUZI WA KINA WAANZA
“Nilianza uchunguzi, niliwahoji shambaboi wangu kuhusu tabia ya mke wangu ambapo waliniambia kila siku nikitoka kwenda kazini nyuma kuna mtu huingia nyumbani kwangu na kukaa na mke wangu kwa muda mrefu ndani.
“Kwa kidokezo hicho, siku moja nilichukua simu ya mke wangu ya kijanjani, nikaipekua na kugundua namba moja ambayo amekuwa akiwasiliana nayo mara kwa mara. Hii namba aliisevu kwa jina la Mwajuma Jumanne.
...Wananchi wakimpiga picha Hussein aliyefumaniwa na mke wa mtu.
“Ajabu ni kwamba, kwa namba hii nilikuta ujumbe mfupi wa maneno (SMS) wa mapenzi kati ya mke wangu na huyo Mwajuma Jumanne. Nilianza kuhisi kuna jambo.
“Moja ya meseji ilisema yeye (Mwajuma) hana mke! Nikajua huyo Mwajuma ni mwanaume niliyeambiwa na shambaboi kuwa huwa anakuja nyumbani kwangu.
“Pia upelelezi wangu uligundua kuwa mwanaume huyo ama huwa anamuibia vitu mke wangu au alikuwa anapewa.
“Niliwahi kuambiwa kuwa kuna siku mke wangu alimpa mwanaume huyo shilingi elfu sitini (60,000/) na akarudia tena hivi karibuni kumpa kiasi hichohicho,” alisema kiongozi huyo.
Hussein akijikinga sehemu za kichwa wakati akipewa kichapo na wananchi.
POLISI WAPEWA TAARIFA
Alisema kufuatia mambo yote hayo, aliamua kwenda Kituo cha Polisi Wazo, Dar kutoa taarifa ya kupotelewa na vitu akimtaja mwanaume huyo kwamba ndiye anayemtuhumu. Kwa ujasiri mkubwa, kiongozi huyo aliwaambia polisi kwamba mtu huyo angemtafuta mwenyewe, likafunguliwa jalada namba WP/RB//7720/2013 WIZI.
MUME AANDAA SAFARI YA UONGO
Akiendelea kusimulia mkasa huo, kiongozi huyo anasema:
“Siku ya tukio, nilijifanya nasafiri kwenda Dodoma kikazi ili kumpa mwanya mgoni wangu kujitawala, niliondoka nyumbani alfajiri huku nikiwa nimeweka wapelelezi wangu.
“Ilipofika saa tano asubuhi, Hussein aliingia nyumbani kwangu na kuanza kujimwaga kama kwake bila kujua arobaini yake ilikuwa inatimia siku hiyo.
...akizidi kutembezwa mtaani.
FUMANIZI LATIMIA
“Mimi na wapelelezi wangu tulivamia nyumba, tukagonga mlango, mke wangu akafungua. Aliponiona ni mimi alianguka kwa kiwewe.
“Nilichungulia ndani kupitia dirishani nikamwona mgoni wangu akivaa shati. Alitoka mbio kuelekea getini. Nilichomoa bastola na kupiga risasi moja hewani, ikampagawisha, akataka kupanda ukuta.
“Nilipiga filimbi watu wakaja, walipojua kisa, walimvua suruali na kuanza  kumpa kipigo huku wakimtembeza mpaka moja ya sehemu anazofanyia biashara zake za kuchemsha supu na kukaanga chipsi, bahati yake aliokolewa na polisi,” alisema kiongozi huyo.
Alipoulizwa alipo mkewe kwa sasa, alisema: “Nilimtimua mbio, kaondoka zake.”
Hussein akiwa ndani ya gari la polisi waliofika kumnusuru.
KAKA WA MTUHUMIWA
Kaka wa damu wa Hussein aliyejitambulisha kwa jina la Tambwe alisema kitendo alichokifanya mdogo wake ni cha aibu ila anapinga adhabu aliyopewa ya kutembezwa uchi.
“Hili tukio alilofanya mdogo wangu ni baya, hata baba yetu mdogo hapa mjini siwezi kumwambia kwa sababu linaweza kumpa presha,” alisema mtu huyo ambaye alimuwekea dhamana polisi mgoni huyo.
Kaka mwingine wa mtuhumiwa, Hamis alisema mama yao mzazi (hakumtaja jina) na bibi yao waliopo Tabora walizimia baada ya kusikia tukio hilo na wameongea kwa simu na mtendewa ili amsamehe mgoni wake.

MKE WA MTUHUMIWA
Mke wa mtuhumiwa, Pili Muhammed akizungumzia fumanizi la mumewe kwa njia ya simu akiwa Rufiji, Pwani alisema: “Mume wangu si mkweli katika mapenzi yetu tangu siku nyingi ila niliamua kuvumilia nikiamini atabadilika lakini badala yake sasa amekamatwa ugoni.”
Aliongeza: “Siku ya tukio mtoto wetu mchanga alikuwa anaumwa, nilipomuomba mume wangu anisindikize hospitali aliniambia hajisikii vizuri, akabaki nyumbani kulinda nyumba.
“Niliporudi sikumkuta  na mpaka giza linaingia hakurejea, baada ya muda kidogo nikaambiwa amekamatwa ugoni yupo Kituo cha Polisi Tegeta (si Wazo). Ndiyo nikawapigia simu kaka zake wakaenda kumdhamini.CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate