Bunge la seneti nchini Italia 
limepitisha hoja ya kumtimua Waziri Mkuu mstaafu wa Italia Silvio 
Berlusconi katika bunge kutokana na kupatikana na hatia ya kukwepa 
kulipa kodi.
Kufuatia hatua hiyo sasa Berlusconi anaweza kushtakiwa kutokana na kukosa kinga ya bunge.

Silvio Berlusconi
Kwa upande Berlusconi amewaambia 
wafuasi wake kuwa leo ni siku ya maombolezo katika demokrasia na kwamba 
kura hiyo ya bunge la seneti inaonyesha chuki binafsi ya wale wa upande 
wa kushoto.
                     
Berlusconi alijiondoa siku ya jumanne katika 
chama cha Forza Italia ambacho kipo ndani ya serikali ya mseto 
inayotawala nchi hiyo, hata hivyo serikali iliepuka kura ya kutokuwa na 
imani na kufanikiwa kupitisha bajeti.
Mjadala katika bunge la seneti umekuwa mkali ambapo maseneta kutoka pande zinazopingana wamekuwa wakitupiana maneno makali.
Manuela Ripetti kutoka chama cha Berlusconi cha 
Forza Italia alisikika akipaza sauti "Tunajua nia yenu ni kumwondoa 
Silvio Berlusconi".
Awali Berlusconi ambaye ametawala katika siasa 
kwa miongo miwili nchini Italia amewaomba maseneta kusogeza mbele kura 
hiyo ya kumwondoa kwa madai kwamba anao ushahidi unaothibitisha kuwa 
hajafanya kosa la kukwepa kodi.VIA BBC SWAHILI
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment