Waziri Mkuu wa wa Latvia, Valdis Dombrovskis, 
amejiuzulu kufuatia kuporomoka kwa jengo moja nchini humo, Alhamisi 
iliyopita na kusababisha watu wapatao hamsini kuuawa.
Bwana Dombrovskis amesema amekubali kuwajibika 
kisiasa kutokana na mkasa huo ambapo paa ya duka moja kubwa la bidhaa 
katika mji mkuu, Riga, lilipinda na kuporomoka. 

Valdis Dombrovskis,waziri mkuu wa Latvia
Polisi wameanzisha uchunguzi wa kihalifu kubaini
 kama taratibu za ujenzi wa jengo hilo zilizingatiwa au la; bustani 
ilikuwa ikijengwa juu ya paa la jengo hilo la maduka wakati ajali hiyo 
ikitokea.
Latvia imekuwa na siku tatu za maombolezo 
kuwakumbuka waathirika wa janga hilo, ambalo ni baya kuwahi kutokea 
nchini Latvia, tangu nchi hiyo ijipatie uhuru wake mwaka 1981.
Kujiuzulu kwa Bwana Dombrovskis, ambaye ameiongoza Latvia katika kipindi cha mgogoro wa kiuchumi, kumekuja wiki kadhaa kabla ya nchi hiyo kujiunga na umoja wa Ulaya.
Kujiuzulu kwa Bwana Dombrovskis, ambaye ameiongoza Latvia katika kipindi cha mgogoro wa kiuchumi, kumekuja wiki kadhaa kabla ya nchi hiyo kujiunga na umoja wa Ulaya.
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment