PICHA za aliyekuwa mke wa marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Wastara
Juma akiwa na mwigizaji Bondi bin Salim ‘Bond’ zimezua utata ambao
unakazia ukweli wa taarifa ya kuwa wawili hao ni wapenzi.

Kikizungumza
na Ijumaa Wikienda chanzo chetu kilicho makini, kilisema kinawashangaa
sana Wastara na mwenzi wake huyo kuukana upenzi wao kila kukicha wakati
picha zinajieleza.

“Wastara
amekuwa akimkana Bond kuwa si mpenzi wake ila ni kaka yake sasa hebu
tazama picha zao mpya, hata mtoto mdogo humdanganyi kitu,” kilisema
chanzo hicho huku wawili hao wakiendelea kukanusha kuwa na uhusiano wa
kimapenzi.
No comments:
Post a Comment