EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, December 5, 2013

BABY MADAHA APASUA JIPU: DIAMOND FUSKA!

ACHANA na mabifu yaliyotangulia, hili ni jipya kabisaa! Msanii wa sinema na Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha ameingia kwenye bifu zito na Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ na kudai staa huyo wa Wimbo wa Number One ni mzinzi ‘fuska’, Amani lina mkanda mzima.
Baby Madaha akiwa na Diamond.
Bila kumung’unya maneno, mapema wiki hii, Baby Madaha alimvaa Diamond ambaye ni Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB) akimtuhumu kuwa na tabia za kifuska.
Baby Madaha alidai hata muziki anaoufanya Diamond kamwe hauwezi kulingana na mafanikio makubwa ya jina lake zaidi ya kubebwa na skendo tu.
 
Diamond na Wema.
CHOKOCHOKO ZILIVYOANZA
Kupitia mitandao ya kijamii, ilivuja posti ambayo ilidaiwa kutoka kwa Baby Madaha ikimpaka Diamond kuwa siyo mwanamuziki kama ilivyo kwa wasanii wengine wenye uwezo mkubwa, akitolea mfano Elias Barnaba wa THT.
Sehemu ya posti hiyo ilionesha kuwa, Diamond si msanii wa muziki bali ni mzinzi f’lani hivi anayefanya biashara ya muziki kupitia mapenzi.
“Siku wanawake maarufu nchini Tanzania watakapojitambua na kuacha kulewa penzi la Diamond, huo ndiyo utakuwa mwisho wa maisha yake kimuziki kwa sababu hatakuwa na jipya na hivyo soko lake litaporomoka,” ilisomeka posti hiyo.
Diamond na Penny.
UKWELI NI UPI?
Baada ya ishu hiyo kugeuka habari ya mjini na kuibuka kwa makundi mawili yanayokinzana, Amani lilimtafuta Baby Madaha ili kujua ukweli wa posti hiyo ndipo akatiririka aya za kuthibitisha kuwa picha haziivi, hamkubali Diamond na kudai hata kimuziki hamkubali kwani anaamini wapo wanamuziki wanaofanya vema katika gemu kuliko yeye.
“…tuseme ukweli, Diamond ni mfanyabiashara siyo mwanamuziki. Kuhusu hiyo posti iwe ni mimi nimeandika au si mimi lakini kimsingi hayo maneno yanamstahili kabisa. Mzinzi tu.
“Diamond anabebwa na media (vyombo vya habari). Kuna wanamuziki wengi wazuri sembuse yeye? Ana nini haswa?” alihoji Baby.
 
Diamond na Jokate.
AMANI LAMGEUKIA DIAMOND
Baada ya kusikia maelezo ya Baby kwa kifupi, Amani lilimuweka ‘pending’ kwa muda na kumwendea hewani Diamond ili liweze kujua upande wake analizungumziaje bifu hilo ambalo lilikuwa likienea mitandaoni kama moto wa kifuu.
Tofauti na matarajio ya mapaparazi wetu kwamba huenda angejibu mashambulizi makali kwa Madaha, Diamond au ‘Sukari ya Warembo’ aling’aka huku akimponda mwanadada huyo na kumshangaa:
BOFYA HAPA KUMSIKIA
“Daaah! Huko ni kunishusha…mimi na huyo (Baby) wapi kwa wapi kamwe huwezi kunilinganisha na mtu ambaye yupo chini yangu sana, nikijibizana naye nitajishusha tu. Ingekuwa ni mtu mkubwa mwenye levo yangu hapo ningesema natakiwa kusema neno.
“Hana lolote huyo anatafuta ‘kiki’ tu kupitia mimi, nipo na dili zangu za maana nipoteze muda kwake? Atafute wa levo yake na wala si mimi.”
UZINZI VIPI?
Alipoulizwa kuhusu suala la uzinzi ambalo Baby Madaha aliumaanisha katika posti yake, Diamond aliendelea kukazia kuwa hana muda wa kupoteza kwa mtu kama Baby Madaha ambaye kimsingi ni kama ardhi na mbingu.
“Huyo anatafuta kiki tu, aachane na mimi…mbona hatufanani kabisa mimi na yeye wapi kwa wapi?” alikazia Diamond a.k.a Weka Mbali na Watoto Wazuri wa Kike.
BABY AREJEA HEWANI
Wakati mapaparazi wetu wakimalizana na Diamond, kilongalonga kimoja cha paparazi wetu kilikuwa kikionesha kinaita, ilivyokatika ya Diamond, Baby akapanda hewani kwa mara nyingine.
Safari hii alimchana laivu: “Nimeisoma upya posti yenyewe, kilichopo humu ni ukweli mtupu. Hakuna hata tone la uongo, wewe utamlinganisha Diamond na mtu kama Barnaba? Huyu ni mfanyabiashara tu, hajui kuimba kwa kutumia vyombo kama mimi.
“Diamond hawezi kupiga chombo hata kimoja cha muziki atajiitaje mwanamuziki? Anastahili kabisa ujumbe huu.”
UFUSKA
Mapaparazi wetu walilazimika kumtwanga swali Baby Madaha kuhusiana na ufuska ambao ulikuwa umetajwa katika maelezo ya awali, kama endapo Diamond ni mzinzi au yeye ndiyo mzinzi.
Katika maelezo yake, Baby Madaha aliwashangaza mapaparazi wetu kwa kutaja namna gani anaweza kumuita Diamond mzinzi. Sikia:
Amani: “Umesema Diamond si mwanamuziki, je, suala la uzinzi ni nani analo kati yako na yeye?”
Baby: “Mimi si mzinzi. Diamond ndiyo mzinzi tena sana tu.”
Amani: “Uzinzi wake upo wapi?”
Baby: “Kitendo cha kubadilisha wanawake, kufumaniwa na Wema Sepetu akiwa na Jokate Mwegelo ndiyo uzinzi wenyewe huo.”
Amani: “Kwani wewe hujawahi kuwa na wanaume tofauti? Hujawahi kufumaniwa?”
Baby: “Mimi sijawahi, yeye amewahi na hakuwahi kukanusha hivyo inadhihirisha kuwa ni kweli. Kwangu mimi kila aliyetajwa kutoka na mimi kama haikuwa kweli, nilikanusha mara moja yeye mbona hakanushi?”
Amani: “Kwani Diamond alifumaniwa na nani?”
Baby: “Acha hizo, kwani hukumbuki kipindi cha Wema? Mara alinaswa na Aunt mara na… yule ndiyo mzinzi sasa.”
KWANI WALITONGOZANA?
Kuhusu suala la kutongozwa, Baby alisema Diamond hajawahi. Cha kushangaza zaidi, alisema hata kama ikitokea siku staa huyo akamtongoza kamwe hawezi kumkubalia kwani hawaendani hata kidogo.
Alisema yeye ni mtu wa kutembea na vigogo na si vitoto kama Diamond.
“Hana hela, kamwe siwezi kumkubalia. Ni mtu ambaye ana vihela mbuzi sasa mtu kama yeye mimi wa nini? Ndiyo maana aliwahi kukimbiwa na mwanamke kwa kuwa hana hela.
“Tena yule mwanamke akaenda kwa kigogo mwenye hela, mimi na yeye ni mbalimbali kabisa. Hata muziki ninaofanya hauwezi, mimi ninaimba RnB yeye anafanya Pop, tuko tofauti kabisa,” alisema Baby pasipo kumtaja mwanamke aliyemkimbia Diamond.
TUJIKUMBUSHE PANDE ZOTE
Diamond aliwahi kuripotiwa kutoka kimapenzi na ‘totoz’ kibao wakiwemo yule wa mwanzo aliyemzingua aitwaye Sarah, Rehema Fabian, Jacqueline Wolper, Upendo Mushi ‘Pendo wa Maisha Plus’, Wema Sepetu, Natasha (Video Queen wa Wimbo wa Moyo Wangu), Najma (aliwahi kuwa mpenzi wa Mr. Blue), Jokate Mwegelo, yule demu wa Kenya na aliyekuwa mwigizaji aliyefulia ambaye ni mke wa mtu.
Kwa upande wake Baby Madaha anayekimbiza na ngoma yake ya Summer Holiday naye si haba kwani aliwahi kuripotiwa kuminya kimapenzi na yule mtoto wa mwanasiasa maarufu Bongo (jina lipo), Mwisho Mwampamba, Dokta Pakir, Juma Nature na Joe Kairuki aliye naye sasa ambaye ni mume wa mtu.
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate