EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 24, 2013

MAKUMBI JUMA AWATOLEA UVIVU VIONGOZI YANGA, ASEMA; “PESA SI KILA KITU, UTAALAMU UNAHITAJIKA”

Habari na Bin Zubeiry.
MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Makumbi Juma ‘Homa ya Jiji’ amewashauri viongozi wa klabu yake ya zamani, Yanga SC kuwashirikisha wachezaji wake wa zamani katika uongozi ili kusaidia masuala ya kitaalamu. Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana, Makumbi aliyekuwa akifahamika pia kwa jina lingine la utani kama Bonga Bonga alisema kwamba watu wenye fedha ni muhimu katika klabu, lakini hata wataalamu ni muhimu pia.
Pesa si kila kitu; Makumbi Juma akizungumza na BIN ZUBEIRY jana
Makumbi amesema Yanga SC hivi sasa ina hali nzuri kiuchumi kutokana na kuwa na viongozi wa wenye fedha kama Mwenyekiti wake Yussuf Manji na baadhi wa Wajumbe kama Abdallah Bin Kleb, Seif Ahmed ‘Magari’, Mussa Katabaro na Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga, lakini inakosa wataalamu wa masuala ya kiufundi.  
Amesema Yanga ina utajiri mkubwa wa wataalamu, lakini viongozi wa klabu hiyo wameshindwa kuutumia na ndiyo maana pamoja na utajiri wao wanakwama kuwa na timu bora.
“Kuna wachezaji wengi wa zamani wenye mapenzi na Yanga na ambao pia ni wanachama, lakini hawashirikishwi na ndiyo maana timu inashindwa kufanya vizuri. Lazima tushirikishwe kwa sababu sisi tunaujua mpira na tumeucheza, wao wawezeshe mipango ya fedha, na sisi tutengeneze mambo ya kitaaamu, mambo yawe mambo,”alisema Bonga.
Wakali wa enzi hizo; Kutoka kulia Thomas Kipese, Paschal Kaliasa na Mohamed Hussein, wachezaji wa zamani wa Yanga SC
Mshambuliaji huyo mwiba wa mahasimu wa jadi, Simba enzi zake, alisikitishwa na kipigo cha mabao 3-1 kwa wapinzani wao, Wekundu wa Msimbazi Jumamosi katika mechi ya Nani Mtani Jembe na akasema; “Viongozi wameyataka”.  
Alisema; “Hawataki kabisa kusikia wachezaji wa zamani wa Yanga katika mfumo wa uongozi, hicho kitu siyo sawa, kuna mambo ambayo yanahitaji utaalamu, lakini pia hata nidhamu ya wachezaji imekuwa mbovu kwa sababu hawajui historia ya klabu wala magwiji wake,”.  
“Leo hii mchezaji wa Yanga hamjui hata Sunday Manara ni nani wala Mohamed Huusein ni nani, kwa sababu viongozi hawathamini wachezaji wa zamani. Mimi wakati nasajiliwa Yanga (miaka ya 1980) nilipoingia pale klabuni nilikuta picha za wachezaji waliotutangulia akina Leonard Chitete, Maulid Dilunga na wengine na vikosi pia, lakini leo ukiingia Yanga hukuti hata picha ya kikosi cha msimu uliopita, haya ni makosa sana,”alisema Bonga.  
Bonga amesema anawaheshimu viongozi wa Yanga, lakini lazima ufike wakati waienzi historia ya timu na magwiji wake ndiyo hata wachezaji watakuwa na nidhamu na kuithamini klabu.  
“Leo pale Yanga kuna wachezaji wanajiona wanacheza mpira mkubwa sana, lakini ukweli ni kwamba hawajafikia uwezo wa wachezaji tuliowatangulia, ila kwa sababu klabu haina kumbukumbu za wachezaji wa zamani, basi Yanga inaonekana timu ya leo leo tu,”alisema.         Hoja za Makumbi ziliungwa mkono na wachezaji wengine wa zamani wa Yanga, washambuliaji Thomas Kipese ‘’Ucle Thom na Mohamed Hussein ‘Mmachinga’ ambao walimalizia soka yao kwa mahasimu, Simba SC aliokuwa wakati anazungumza. “Haya anayozungumza Bonga ni ukweli kabisa,”alisema Uncle Thom. “Lazima viongozi wa Yanga wawashirikishe wachezaji wa zamani, hata sisi tulipoingia pale Yanga tuliwakuta wachezaji wa zamani katika mfumo wa uongozi, kwa nini leo hawapo?”alihoji Mmachinga.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate