Muhidin Maalim Gurumo akiwatembelea vijana wake mazoezini
Wakongwe wa kupuliza midomo ya bata Kinga Maluu (shoto) na Yahaya wakiwa mazoezini
Hafsa Kazinja, Edo Sanga, Juma katundu na Hussen Jumbe wakila tizi.Kwa picha zaidi na Saidi Mdoe BOFYA HAPA..
WANAMUZIKI
nyota waliowahi kutamba na bendi ya DDC Mlimani Park “Sikinde Ngoma ya
Ukae” watapiga bonge la show kwenye tamasha la Gurumo Jumamosi hii ndani
ya TCC Club Chang’ombe jijini Dar es salaam. Wakali hao ambao kwa sasa
hawako na Sikinde, jana walihitimisha mazoezi ya nyimbo tano
watakazopiga katika tamasha hilo.
Mazoezi
hayo makali yalifanyika Amana Club Ilala ambako kwa wiki nzima
wanamuziki watakaoshiriki tamasha hilo wamekuwa wakikutana hapo na
kupiga mazoezi ya kufa mtu. Baadhi ya nyimbo hizo ni pamoja na “Celina”
utunzi wake Gurumo kwa kushirikiana na marehemu Joseph Mulenga, “Barua
kutoka kwa Mama” uliotungwa na Cosmas Chidumule na “Gama” (Tshimanga
Kalala Assossa).
Mratibu
wa mazoezi hayo, Mzee Kassim Mapili alisema nyimbo mbili zingine za
Sikinde zitajulikana siku ya onyesho lakini akafichua kuwa zitakuwa ni
kati ya “Neema” (Chidumule), “Supu umeitia nazi” (Karama Legesu),
“Nachechemea” na “Isaya” (Hussein Jumbe).
Wasanii
waliowahi kuitumikia Sikinde ambao watakuwepo kumsindikiza Gurumo ni
pamoja na Cosmas Chidumule, Abdallah Gama, Hussein Jumbe, Mashaka
Shaaban, Kalamazoo, Henry Mkanyia na Karama Legesu.
Wengine
ni Ali Yahaya na Boniface Kachala, Tshimanga Kalala Assossa, Shaaban
Lendi na Ibrahim Mwinchande. Katika maendeleo mengine, Komandoo Hamza
Kalala naye kwa kushirikiana na wakongwe hao, amekamilisha mazoezi ya
nyimbo mbili “Vicky” na “Tumezaliwa wote Kijiji kimoja” ambazo zitapigwa
Jumamosi kusindikiza tamasha hilo.
Mkongwe
Mzee Makassy nae katika tamasha hilo atashuka na wimbo wake uliowahi
kutamba sana “Anifa”. Tamasha la Gurumo 53 ni maalum kwa ajili ya
kuhitimisha miaka 53 ya utumishi uliotukuka katika muziki wa dansi kwa
Muhidin Maalim Gurumo ambaye ametangaza rasmi kustaafu muziki. Wasanii
wengine wanaoshiriki mazoezi hayo ni Miraji Shakashia, Hafsa Kazinja,
Juma Katundu, Edo Sanga Majengo na King Maluu. Burudani zingine
zitakazokuwepo siku hiyo ni pamoja na bendi za Msondo Ngoma Music Band,
Talent Band, na Twanga Pepeta.
Hafsa
Kazinja anatarajiwa kumwaga kibao cha 'Nimuokoe nani' alichokipiga upya
kumuenzi Gurumo na sasa kinatamba katika redio nchi nzima. Yeye ni
mwanamuziki pekee wa kizazi kipya anayeshiriki katika hafla hii ya
kihistoria.
itakuwa kali kinoma
ReplyDelete