EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 10, 2013

TAMKO LA WENYEVITI WA CCM-MIKOA LA KUMPONGEZA KATIBU MKUU WA CCM NDG. ABDULRAHAMAN OMAR KINANA NA SEKRETARIETI YA CCM TAIFA


Mgana Izumbe Msindai – Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM wa Mikoa akitoa tamko hilo kwenye makao makuu ya Chama Chama Mapinduzi Ofisi ndogo Lumumba jijini Dar es salaam leo,kulia ni Haji Juma Haji – Makamu Mwenyekiti Wa Wenyeviti Mikoa na kushoto ni Lucas Ole Mukusi – Katibu wa Wenyeviti Mikoa.
................................................................................................................
Sisi Wenyeviti wa CCM-Mikoa tuliokutana leo, Desemba10/2013 hapa Dar es salaam, kwa kauli moja na kwa niaba ya wanaCCM wa mikoa yetu, tunatoa kauli ya kumuunga mkono Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi ndugu Abrahamani Kinana na Sekretarieti yote kwa utekelezaji uliotukuka wa majukumu yao ya kichama.
Tangu alipopewa wadhifa wa Ukatibu Mkuu ameonyesha uwajibikaji mkubwa, uliokiwezesha Chama kupata uhai mpya na kuamsha Ari na matumaini zaidi ya Watanzania kwa Chama Cha Mapinduzi.
WanaCCM nchini tuko katika mstari wa mbele kuisimamia Serikali yetu kwa mujibu wa Ilani ya CCM ya mwaka 2010-2015 sura ya Tisa; Inayokitaka Chama kuisimamia Serikali yake.

Kwa pamoja tunaungana na kupinga kwa nguvu zote mambo yafuatayo;
1. Ubadhirifu unaofanywa katika Serikali za Mitaa nchini unaozifanya Halmashauri nyingi kujirudiarudia kupata hati chafu na zenye mashaka, inayosababisha hasara na manung’uniko kwa wananchi.
2. Utelezaji duni wa baadhi ya miradi ya maendeleo unaopelekea kuwepo kwa huduma duni na zisizokidhi thamani ya fedha na matakwa ya kitaalamu. Hii inaashiria uwepo wa Rushwa na ubadhirifu wa fedha kwa baadhi ya miradi ya maendeleo.
3. Ucheleweshaji wa maslahi na stahiki za watumishi wa Umma kunakopelekea kuwa wavunja moyo na ari watumishi, katika kutekeleza majukumu yao na hivyo kusababisha kutokea kwa migomo ya mara kwa mara kufuatia uzembe katika kuwapatia haki zao, kinyume na misingi ya utawala bora.
4. Gharama kubwa ya uendeshaji wa shughuli za Serikali na Taasisi zake ikilinganishwa na gharama zinazotumika kwenye miradi ya maendeleo na uboreshwaji wa huduma za jamii kwa wananchi.
5. Usimamizi mbovu wa Operation mbali mbali za Serikali zenye nia njema kwa Taifa. Mfano Operasheni kuhamisha wafugaji na Operasheni Tokomeza; Zina nia njema lakini usimamizi wake umekuwa mbovu hata kupelekea kuvuruga nia yake njema kwa Taifa.
6. Kushindwa na Kuchelewa kutatua baadhi ya Kero sugu kwa Wananchi kama malalmiko mbali mbali ya wakulima (mfano mbolea za minjingu kutofanya vizuri kwa asilimia kubwa, matatizo ya wakulima wa pamba na korosho nk.) na wafugaji; Rushwa zilizokithiri katika sehemu mbali mbali za utoaji wa huduma kwa wananchi na ucheleweshwaji wa fadha za miradi ya maendeleo nk.
Katibu Mkuu wa CCM daima amekuwa akikemea kwa nguvu zote madhaifu yote tuliyoyataja hapo juu na sisi kama Wenyeviti wa CCM Mikoa yote Tanzania. Tunaitaka Serikali ichukue hatua za haraka katika kurekebisha madhaifu hayo.
Viongozi na watendaji wengine wote wa Serikali, walioonesha udhaifu mkubwa katika kutekeleza majukumu yao, na ambao walipewa wito na wengine ambao wanatakiwa kupewa wito; wa kuhudhuria mbele ya Kamati Kuu ya CCM wachukuliwe hatua zinazostahili.
Tunawakumbusha viongozi wa Serikali watambue kuwa Chama cha Mapinduzi kinaisimamia Serikali kwa mujibu wa Ilani ya CCM ya mwaka 2010-2015 Sura ya Tisa.
_______________________________________________
Mgana Izumbe Msindai – Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM wa Mikoa
___________________________________________________
Haji Juma Haji – Makamu Mwenyekiti Wa Wenyeviti Mikoa

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate