EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, January 22, 2014

BABY MADAHA: NIMEUMBUKA!


Jambo limezua jambo! Ile skandali ya kunaswa baada ya kuingia mkenge kwenye mtego wa kujiuza imemtokea puani staa wa sinema na Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha ambaye amekiri kuumbuka.
Habari hiyo iliruka hewani kwenye gazeti dada la hili, Ijumaa wiki iliyopita toleo namba 862 la Januari 17 hadi 23 likiwa na kichwa cha habari ‘BABY MADAHA ANASA MTEGO WA KUJIUZA.
SAFARINI

Ilielezwa kuwa wakati skendo hiyo ikiingia mitaani, mwanadada huyo alikuwa safarini kuelekea Nairobi, Kenya ambako ndiko yaliko Makao Makuu ya Kampuni ya Candy n Candy iliyompa mkataba mnono wa takribani Sh. milioni 200 ili wasambaze na kuuza kazi za Baby Madaha.
MAPOKEZI

Kwa mujibu wa chanzo chetu makini nchini humo, imezoeleka kuwa kila Baby Madaha anapotua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, Nairobi kwa ajili ya kazi za kampuni hupokelewa na timu maalum kisha kuchukuliwa na lile gari la bei mbaya aina ya Audi TT.
Ilielezwa kuwa baada ya habari ya kunaswa kwake kusambaa, alipotua uwanjani hapo hakukuwa na mtu aliyekwenda kumpokea kwa kile kilichoelezwa kuwa viongozi wa kampuni hiyo walichukizwa na jambo hilo.

“Unajua tatizo ni simu ambazo viongozi wa Candy n Candy wanapigiwa na vyombo vya habari kutaka kujua undani wa skendo hiyo,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:

NYUMBANI
Baada ya kugundua kuwa alitelekezwa uwanjani, Baby Madaha alifanya mpango wa kwenda kwenye nyumba ya kampuni hiyo ambayo huwa anaishi lakini huko nako alikutana na ‘mbwa mkali’. Aliambiwa uongozi umekataza yeye kutia maguu ndani ya nyumba hiyo.
Kiliendelea kutiririka kuwa wakati huo, tayari Mkurugenzi wa Candy n Candy, Joe Kairuki alishawasiliana na Baby Madaha ambaye alimwambia kuwa skendo hiyo haikuwa ya kweli bali ‘promo’ ya filamu yake mpya ya The Gal Bladder.


OFISINI
“Hata angejitetea vipi, wale jamaa walikuwa hawamwelewi kwani alikwenda hadi ofisini kwao lakini hawakutaka kumsikiliza hadi hapo baadaye.
“Wanacholalamikia ni kwamba Baby Madaha amechafua sura ya kampuni na wanaonekana wanafanya kazi na msanii anayejihusisha na ufuska,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:

GARI
“Hata hilo gari la Audi TT atakuwa analisikia kwenye bomba. Alizoea kukatiza nalo mitaa hapa Nairobi lakini sasa matatuu (daladala) zinamhusu.”

MSIKIE
Baada ya kujazwa data hizo, gazeti hili lilimtafuta Baby Madaha ambaye mwanzoni alikataa kutoa ushirikiano kwa kigezo kwamba ameharibiwa maisha.
Risasi: Baby lakini ni vizuri ukawa muwazi kuliko kuwa mkali. Je, ni kweli Candy n Candy wamevunja mkataba na wewe?
Baby: (kilio) Nasema niacheni kwanza mimi siyo msemaji wa Candy n Candy, mtafuteni mkurugenzi.
Alipomaliza kusema kwa hasira, Baby alikata simu.

MKURUGENZI
Hata hivyo, alipotafutwa mkurugenzi huyo, Joe alikuwa na haya ya kusema:
“Yaa tumeingia kwenye matatizo kwa sababu ya hiyo habari.”
Risasi: Matatizo gani?
Joe: Tumepigiwa sana simu na vyombo vya habari kuthibitisha hiyo skendo. Tunaonekana tunafanya kazi na mtu ambaye siyo. Anatuharibia image (sura) ya kampuni.
Risasi: Kwa yeye (Baby Madaha) amewaambiaje?
Joe: Anasema ni mambo yake ya filamu, kimsingi hatujamuelewa ndiyo maana hatujampa muda wa kumsikiliza kiundani.
Risasi: Kwa hiyo mtavunja mkataba wake na ninyi?
Joe: Ndiyo lengo letu lakini siyo jambo la haraka kwani kuna masuala ya kisheria.
Risasi: Vipi kuhusu gari na nyumba mlivyomkabidhi?
Joe: Kwa sasa kila kitu kipo chini ya kampuni.
Risasi: Nini hatima yake (Baby Madaha) sasa?
Joe: Yeye ndiye mumuulize nini hatima yake.

BABY MADAHA TENA
Baada ya mazungumzo hayo, gazeti hili lilimrudia Baby Madaha ambapo safari hii alikuwa mpole: “(kilio cha kwikwi) jamani nimeumbuka. Yaani huku wameichukulia kuwa ishu kubwa sana.”
Risasi: Sasa nini hatima yako?
Baby Madaha: Mi nipo Nairobi najaribu kuweka mambo sawa. Namwamini Mungu, najua atanijalia haja ya moyo wangu.

AMEFIKAJE HAPA?
Baby Madaha aliingia mkataba na kampuni hiyo mwaka jana ambapo mpaka sasa amesharekodi nyimbo mbili za Squeeze na Summer Holiday huku akirekodi filamu moja ya The Gal Bladder iliyozinduliwa hivi karibuni, jijini Dar.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate