EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, January 25, 2014

SITASITA KUWAONDOA WATUMISHI / WAKUU WA IDARA WANAOWACHONGANISHA MADIWANI NA MKURUGENZI WAO - INJINIA MANYANYA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kilichofanyika jana tarehe 25 Januari 2014 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo uliopo Sumbawanga Mjini. 
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Methew Sedoyyeka akizungumza katika kikao hicho ambapo alitilia mkazo juu kuboresha elimu na ufaulu katika halmashauri hiyo ambayo haijafanya vizuri katika siku za karibuni. Alisisitiza pia umuhimu wa upandaji miti hususani katika msimu huu wa masika.
Mbunge wa Jimbo la Kwela (CCM) Ignas Malocha akishukuru ujio wa Mkuu huyo wa Mkoa katika kikao hicho na maelekezo aliyoyatoa ambayo alisema ni muongozo mzuri na wa kuzingatiwa katika maendeleo ya halmshauri hiyo.
Mkuu huyo wa Mkoa akizungumza na wajumbe wa kikao hicho kushoto wakiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na kulia wakiwa ni wakuu wa idara katika halmashauri hiyo.
Madiwani wa halmashauiri ya wailaya ya Sumbwanga.
Wakuu wa Idara Halmashauri ya Wilaya ya Sumbwanga.
Picha ya pamoja kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya, Madiwani na Viongozi wa Chama tawala (CCM) walioalikwa katika kikao hicho.


NA HAMZA TEMBA - OFISI YA MKUU WA MKOA RUKWA
........................................................

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya amewaonya watumishi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga wakiwemo wakuu wa idara wenye tabia ya kuwachonganisha madiwani na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndugu Adam Misana, "watumishi mnaofanya mchezo huo nitawaondoeni" Alisema Manyanya. 

Manyanya aliyasema hayo jana katika kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga alipotembelea kutoa salam zake za mwaka mpya kwenye baraza hilo. Alisema kuwa tangu Mkurugenzi huyo ateuliwe kuiongoza Halmashauri hiyo amekuwa akifanya vizuri katika udhibiti wa mapato jambo ambalo limekuwa kero kubwa wakuu wa idara na watumishi wa ofisi hiyo.

Alieleza kuwa Mkurugenzi aliyekuwepo kabla ya Misana alikua akikaimisha ofisi mara kwa mara kwa watu tofauti jambo ambalo lilizorotesha utendaji na kupelekea mambo kufanyika kienyeji na kwa mazoea bila kujali matumizi sahihi ya mapato ya Halmashauri. Ujio wa Mkurugenzi huyu mpya umerekebisha hali hiyo kwa kiwango kikubwa hususani katika matumizi ya fedha za halmashauri, aliongeza Mkuu huyo wa Mkoa.

Katika salam zake alilieleza baraza hilo kuwa mpaka sasa toka ateuliwe kuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ameshatembelea kata 51 sawa na asilimia 80% ya kata zote Mkoani Rukwa. Alisema baadhi ya kata hizo ameshazitembelea zaidi ya mara tano kutokana na umuhimu na matukio yaliyojitokeza.

Aliwata madiwani, viongozi wa chama na halmashauri pamoja watumishi kwa ujumla kutoa uongozi uliotukuka katika maeneo yao kwa kushirikiana katika kutoa huduma bora kwa wanachi na kuwafikia mara kwa mara pale inapowezekana na kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.

Katika hali nyingine Mkuu huyo wa Mkoa alishangazwa kwa Wilaya ya Sumbwanga kutokuwa na Hospitali yake ya Wilaya na badala yake kutegemea huduma katika Hospitali  Kuu ya Mkoa. Alisema mwaka huu 2014 ni mwaka wa afya na kwamba Halmashauri za Wilaya ya Sumbwanga zijipange kuhakikisha zinakuwa na hospitali yao ya Wilaya ili kuweza  kutoa nafasi kwa hospitali kuu ya Mkoa kuhudumia wagonjwa wa rufaa kuliko ilivyo hivi sasa ambapo ambapo inabebeshwa mzigo mkubwa na Wilaya hiyo.

Katika salam zake Injinia Manyanya aliwashauri madiwani na viongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kujipanga kuhakikisha wanahamia katika Mji mdogo wa Laela uliopo takribani kilomita 100 kutoka mjini Sumbawanga. Alisema zipo faida kubwa za kufanya hivyo ikiwemo ya halmasahuri kuwa na mji wake watakaouendeleza kisasa na kujiwekea mikakati mbalimbali ya kimaendeleo. Aliongeza pia kuwa itakuwa fursa ya kuwasogezea wananchi huduma.

 Akielezea kuhusu jengo kubwa la kisasa la Halmashauri hiyo linaloendelea kujengwa mjini Sumabwanga alisema linaweza kutumika kama kitega uchumi cha Halmashauri ambapo litawapatia fedha nyingi za kujiendesha na kwamba wataomba fedha nyingine TAMISEMI ya kujenga ofisi kubwa kama hiyo Laela kwa lengo la kuwasogezea wananchi huduma.

Akizungumzia kilimo na ufugaji aliwataka viongozi wa halmashauri wakishirikiana na madiwani kuhakikisha wanajiwekea utaratibu maalumu wa maeneo ya wakulima na wafugaji na kuhakikisha kunakuwepo na idadi maalum ya mifugo inayotakiwa kufugwa katika maeneo yaliyotengwa na kuwekewa alama maalum za utambuzi.

Kwa upande wa ONYARU - Ondoa Nyasi Rukwa alisema kuwa mpango huu umekuwa na mafanikio makubwa kwani maeneo mengi wananchi wamehamasika kwa kuondoa nyasi na kuezeka kwa bati nyumba zao. Aliwataka viongozi na wasimamizi wa halmashauri kuendelea na uhamasihaji huo kuhakikisha nyumba za nyasi zinauhama Mkoa wa Rukwa. 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate