Mkuu 
wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza katika kikao cha 
baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kilichofanyika
 jana tarehe 25 Januari 2014 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo uliopo 
Sumbawanga Mjini. 
Mkuu 
wa Wilaya ya Sumbawanga Methew Sedoyyeka akizungumza katika kikao hicho 
ambapo alitilia mkazo juu kuboresha elimu na ufaulu katika halmashauri 
hiyo ambayo haijafanya vizuri katika siku za karibuni. Alisisitiza pia 
umuhimu wa upandaji miti hususani katika msimu huu wa masika.
Mbunge
 wa Jimbo la Kwela (CCM) Ignas Malocha akishukuru ujio wa Mkuu huyo wa 
Mkoa katika kikao hicho na maelekezo aliyoyatoa ambayo alisema ni 
muongozo mzuri na wa kuzingatiwa katika maendeleo ya halmshauri hiyo.
Mkuu 
huyo wa Mkoa akizungumza na wajumbe wa kikao hicho kushoto wakiwa 
madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na kulia wakiwa ni wakuu
 wa idara katika halmashauri hiyo.
Madiwani wa halmashauiri ya wailaya ya Sumbwanga.
Wakuu wa Idara Halmashauri ya Wilaya ya Sumbwanga.
Picha 
ya pamoja kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya, 
Madiwani na Viongozi wa Chama tawala (CCM) walioalikwa katika kikao 
hicho.
NA HAMZA TEMBA - OFISI YA MKUU WA MKOA RUKWA
........................................................
Mkuu 
wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya amewaonya watumishi wa Ofisi ya
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga wakiwemo wakuu wa 
idara wenye tabia ya kuwachonganisha madiwani na mkurugenzi mtendaji wa 
Halmashauri hiyo Ndugu Adam Misana, "watumishi mnaofanya mchezo huo 
nitawaondoeni" Alisema Manyanya. 
Manyanya
 aliyasema hayo jana katika kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri 
ya Wilaya ya Sumbawanga alipotembelea kutoa salam zake za mwaka mpya 
kwenye baraza hilo. Alisema kuwa tangu Mkurugenzi huyo ateuliwe 
kuiongoza Halmashauri hiyo amekuwa akifanya vizuri katika udhibiti wa 
mapato jambo ambalo limekuwa kero kubwa wakuu wa idara na watumishi wa 
ofisi hiyo.
Alieleza
 kuwa Mkurugenzi aliyekuwepo kabla ya Misana alikua akikaimisha ofisi 
mara kwa mara kwa watu tofauti jambo ambalo lilizorotesha utendaji na 
kupelekea mambo kufanyika kienyeji na kwa mazoea bila kujali matumizi 
sahihi ya mapato ya Halmashauri. Ujio wa Mkurugenzi huyu mpya 
umerekebisha hali hiyo kwa kiwango kikubwa hususani katika matumizi ya 
fedha za halmashauri, aliongeza Mkuu huyo wa Mkoa.
Katika
 salam zake alilieleza baraza hilo kuwa mpaka sasa toka ateuliwe kuwa 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ameshatembelea kata 51 sawa na asilimia 80% ya 
kata zote Mkoani Rukwa. Alisema baadhi ya kata hizo ameshazitembelea 
zaidi ya mara tano kutokana na umuhimu na matukio yaliyojitokeza.
Aliwata
 madiwani, viongozi wa chama na halmashauri pamoja watumishi kwa ujumla 
kutoa uongozi uliotukuka katika maeneo yao kwa kushirikiana katika kutoa
 huduma bora kwa wanachi na kuwafikia mara kwa mara pale inapowezekana 
na kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.
Katika
 hali nyingine Mkuu huyo wa Mkoa alishangazwa kwa Wilaya ya Sumbwanga 
kutokuwa na Hospitali yake ya Wilaya na badala yake kutegemea huduma 
katika Hospitali  Kuu ya Mkoa. Alisema mwaka huu 2014 ni mwaka wa afya 
na kwamba Halmashauri za Wilaya ya Sumbwanga zijipange kuhakikisha 
zinakuwa na hospitali yao ya Wilaya ili kuweza  kutoa nafasi kwa 
hospitali kuu ya Mkoa kuhudumia wagonjwa wa rufaa kuliko ilivyo hivi 
sasa ambapo ambapo inabebeshwa mzigo mkubwa na Wilaya hiyo.
Katika
 salam zake Injinia Manyanya aliwashauri madiwani na viongozi wa 
halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kujipanga kuhakikisha wanahamia 
katika Mji mdogo wa Laela uliopo takribani kilomita 100 kutoka mjini 
Sumbawanga. Alisema zipo faida kubwa za kufanya hivyo ikiwemo ya 
halmasahuri kuwa na mji wake watakaouendeleza kisasa na kujiwekea 
mikakati mbalimbali ya kimaendeleo. Aliongeza pia kuwa itakuwa fursa ya 
kuwasogezea wananchi huduma.
 Akielezea
 kuhusu jengo kubwa la kisasa la Halmashauri hiyo linaloendelea kujengwa
 mjini Sumabwanga alisema linaweza kutumika kama kitega uchumi cha 
Halmashauri ambapo litawapatia fedha nyingi za kujiendesha na kwamba 
wataomba fedha nyingine TAMISEMI ya kujenga ofisi kubwa kama hiyo Laela 
kwa lengo la kuwasogezea wananchi huduma.
Akizungumzia
 kilimo na ufugaji aliwataka viongozi wa halmashauri wakishirikiana na 
madiwani kuhakikisha wanajiwekea utaratibu maalumu wa maeneo ya wakulima
 na wafugaji na kuhakikisha kunakuwepo na idadi maalum ya mifugo 
inayotakiwa kufugwa katika maeneo yaliyotengwa na kuwekewa alama maalum 
za utambuzi.
Kwa 
upande wa ONYARU - Ondoa Nyasi Rukwa alisema kuwa mpango huu umekuwa na 
mafanikio makubwa kwani maeneo mengi wananchi wamehamasika kwa kuondoa 
nyasi na kuezeka kwa bati nyumba zao. Aliwataka viongozi na wasimamizi 
wa halmashauri kuendelea na uhamasihaji huo kuhakikisha nyumba za nyasi 
zinauhama Mkoa wa Rukwa.  
 
 
 
 
 
 
 







 
No comments:
Post a Comment