EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, January 15, 2014

WAISLAMU WATAKIWA KUTOLALAMIKIA WAKRISTO


 
Shekhe Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Simba.
SHEKHE Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Simba, ametaka Waislamu kuacha kulalamika, kwamba Wakristo wamekuwa wakipewa upendeleo, badala yake watumie fursa wanazopata kuondokana na malalamiko hayo. Akizungumza katika maadhimisho ya Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW), yaliyofanyika kitaifa mkoani Kigoma jana, Mufti Simba alisema chanzo cha malalamiko hayo ni Waislamu kushindwa kujitolea katika mambo mbalimbali ya maendeleo.

Akitoa mfano, alisema Waislamu wanapaswa kupeleka watoto wao kusoma elimu zote mbili na kuwaandaa kushika nafasi za kiutendaji ambazo wanalalamikia kuwa zimetolewa kwa upendeleo kwa Wakristo.
Alisema hata katika kukamata maeneo ya uwekezaji, Waislamu wamebaki nyuma kutokana na kushindwa kujitolea kuchangia fedha za kutosha za kuanzisha miradi ya maendeleo kwa ajili ya kuimarisha dini na kuendesha maisha yao.

“Msilalamike, tunisheni mifuko katika misikitini yenu muwe na fedha za kutosha zitakazokuwa kichocheo cha ninyi kushiriki katika shughuli muhimu za kiuchumi. Kosa ni lenu, msilalamikie Wakristo hawana tatizo hata kidogo katika hilo,” alisema Mufti Simba.
Madaraka misikitini Mjumbe wa Baraza la Ulamaa la Taifa, Ally Mkoyogore, alitaka Waislamu kuongeza bidii katika elimu na uchumi, badala ya kutumia muda mwingi kupigania madaraka misikitini.

Alisema kurudi nyuma kwa Waislamu, kunasababishwa nao wenyewe kushindwa kufuata maadili na misingi ya dini yao, badala yake wanagombea uongozi misikitini kwa ajili ya maslahi binafsi.
Maadhimisho hayo ya Maulid yalihudhuriwa na viongozi wa dini kutoka mikoa mbalimbali nchini, mashekhe kutoka Burundi huku Serikali ikiwakilishwa na Mkuu wa Mkoa Kigoma, Issa Machibya.
Mshikamano Akizungumza katika mkesha wa Maulid usiku wa kuamkia jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, Rais mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi, alitaka Watanzania kujenga mshikamano kwa kusikilizana na kuvumiliana, kwa lengo la kudumisha tunu ya amani na utulivu iliyodumu kwa miaka mingi sasa nchini.

Katika salamu zake za siku hiyo, Alhaji Mwinyi alisema dini zote ukiwamo Uislamu, hazikatazi waumini kushirikiana katika masuala mbalimbali, hivyo ni wajibu wa kila upande kuusikiliza mwingine.
“Nchi zinaijua Tanzania kuwa kisiwa cha amani kisicho na utofauti wa dini, kabila wala rangi. Sote ni ndugu wamoja, tunapaswa kuendelea kuishi kwa usalama na amani.

“Pale inapotokea hali ya kutofautiana, tukae pamoja na kuzungumza ili tufikie mwafaka na si kugombana,” alisema Mwinyi.

Alisema Mtume aliongoza dini kwa kuhubiri mshikamano, kupenda wengine na kuthamini utu na si vurugu kama ambavyo wengine wanadhani.

Akimkaribisha Mwinyi kutoa salamu hizo, Shekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salumu, alisema amani na utulivu nchini ndio ujumbe wa sherehe hizo na kukumbusha Watanzania kuishi kwa umoja na kuwa watu wa Taifa moja lisilo na uvunjifu wa amani.

Kutokana na umuhimu huo, Shekhe Alhad alisema ndiyo maana sherehe hizo zikapewa kaulimbiu ya ‘Uislamu ni amani kwa wote’ lengo likiwa kukumbusha wanaofikiri kuwa misingi ya dini hiyo ni vurugu na kuhatarisha usalama au kujenga uadui kwa watu wengine.

Katiba mpya Shekhe Alhad pia alimpongeza tena Rais Kikwete kwa kufanikisha kwa kiasi kikubwa mchakato wa Katiba mpya ambao hivi karibuni utaingia katika hatua ya uundwaji wa Bunge Maalumu.

“Kama ni safari basi tayari mchakato wa Katiba umevuka Nungwi na karibu unaingia bandarini. Ni jambo la kumpongeza kwa sababu si mataifa yote yangeweza kufika hadi hapa tulipo bila vurugu, ila sisi tumeweza na hata pale palipotokea changamoto fulani, alikabiliana nazo,” alisema Shekhe Salum.

Alisema ni vema Watanzania wazidi kumwombea kiongozi huyo ili akamilishe salama mchakato huo na kumalizia muda wa uongozi na kumkabidhi mtu mwingine kuongoza Taifa. Miongoni mwa wageni waliokuwepo ni Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
Imeandikwa na Fadhili Abdallah, Kigoma na Oscar Job, Dar
CHANZO NI HABARI LEO

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate