EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 21, 2014

WANAWAKE NI JANGA

JANGA la kusafirisha madawa ya kulevya Bongo limezidi kuwa zito kufuatia takwimu za hivi karibuni kuonesha kwamba, idadi ya wanawake kujihusisha na shughuli hiyo inazidi kupanda.
Jack Patrick.
Akizungumza na Uwazi juzi, Kamanda wa Kudhibiti na Kuzuia Madawa ya Kulevya Tanzania, SACP Godfrey Nzowa alisema wanawake wamekuwa ni janga kwa kuwa  wanaongoza kwa kukamatwa kutokana na kujihusisha na biashara hiyo haramu ya ‘unga’.
NZOWA AANIKA MAMBO
Katika mahojiano maalum na gazeti hili, Kamanda Nzowa alisema inasikitisha, inashangaza kwani kwa kipindi kifupi cha kuanzia Desemba 11, 2013 mpaka Januari 6, 2014  watuhumiwa watano walikamatwa na unga, kati yao wanawake walikuwa wanne.
Masogange.
“Hata mwaka jana mpaka Juni, wengi wa watuhumiwa tuliowakamata ni wanawake ukilinganisha na wanaume, hii ni mbinu inayotumiwa na wasafirishaji wa mihadarati kwa kuwatumia wanawake,” alisema Nzowa.
ANAJUA KITAKACHOENDELEA
Kamanda Nzowa alikwenda mbele zaidi kwa kusema: “Tunajua, wahusika wakiona wanawake wanadhibitiwa sana watabadilisha na kutumia wanaume kusafirisha madawa hayo, hii hali inatisha lakini tumeigundua.”

UWANJA WA NDEGE DAR UPENYO?
Nzowa alisema kuwa, watuhumiwa wote hao walikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar wakiwa wamepakia kete za madawa hayo tumboni wakiyasafirisha kwenda nje ya nchi.
KUPANDA MAHAKAMANI WAKATI WOWOTE
Kamanda huyo aliongeza kwamba wanawake watatu walikamatwa Desemba 11, mwaka jana uwanjani hapo wakiwa na madawa tumboni wakielekea nchini China.
Aliwataja wanawake hao kwa ni, Mariam Hamad (29), mkazi wa Tabata- Kimanga, Dar. Alikutwa na pipi zenye uzito wa gramu 670. Hadija )Abdu (30, mkazi wa Magomeni, Dar alikutwa na kete zenye uzito wa gramu 1,227.
Wengine ni Sabrina Salum (34), mkazi wa Kiwalani, Dar. Alikutwa na unga wenye uzito wa gramu 310 na Salama Omar (miaka haikutajwa), mkazi wa Tabata, Dar alikutwa na madawa yenye uzito wa gramu 1,975. Alikamatwa Januari 6, mwaka huu.
Kwa mujibu wa Kamanda Nzowa, watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani wakati wowote kuanzia sasa mara baada ya upelelezi kukamilika.
Imeelezwa kuwa, wanawake wengi wamekuwa wakitumika kusafirisha unga kutokana na tabia iliyokuwepo huko nyuma kwamba, walikuwa wakiaminika na hawakuwa wakikaguliwa kwa undani walipokuwa wakipita viwanjani.
NZOWA ATAHADHARISHA
“Nawatahadharisha wale wote, wakiwemo wanawake wenye nia au wanaofanya biashara hii haramu kuacha kwa sababu vyombo vya dola vitawakamata,” alisema Nzowa.
WANAOGOPWA VIWANJA VYA NDEGE
Baadhi ya wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere walipohojiwa na gazeti hili kwa sharti la kutoandikwa majina yao gazetini, walisema wanawaogopa sana wanawake wanaosafiri siku hizi.
“Hivi sasa tunawaogopa sana wanawake wanaosafiri kwa ndege kuliko wanaume kwa sababu wanaweza kukuingiza katika matatizo ikiwa watapenya na madawa ya kulevya na kukamatwa hapa Dar au huko nje ya nchi,” alisema mfanyakazi mmoja.
Alifafanua kwamba, kutokana na hilo wamekuwa wakiwapekua wanawake kila sehemu za miili yao hata sehemu nyeti ikibidi ili kuhakikisha hawapiti na madawa hayo uwanjani hapo.
WANAWAKE HAO WAPO MASTAA
Hivi karibuni baadhi ya mastaa Bongo wamenaswa kwa kujihusisha na biashara hiyo. Baadhi yao walikutwa na hatia na kuhukumiwa, wengine kesi zao zinaendelea.
Wasanii hao ni Jacqueline Patrick (alikamatwa Macau-China), Saada Kilongo (JNIA-Dar), Agnes Gerald  ‘Masogange (Afrika Kusini) na Melisa Edward (Afrika Kusini). Pia yumo Mbongo aliyenaswa Misri aliyetajwa kwa jina moja la Fatuma huku Sandra Khan ‘Binti Kiziwi’ akitumikia kifungo cha miaka mitano China.
JK AKASIRIKA, AWAONYA WASANII
Akizungumza katika mkutano mmoja na wasaniiwa Rais  Tanzania, Jakaya Kikwete ‘JK’ alionesha hasira zake za wazi kwa wasanii wanaotumika kubeba unga kwenda nje ya nchi.
JK aliwaonya wasanii wenye tabia hiyo na wale ambao wapo katika ushawishi wa kujiingiza kwenye biashara hiyo inayopigwa vita kwa sasa duniani kote kuacha kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate