EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 21, 2014

MAWAZIRI WAANZA KWA TAMBO

Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA Naibu Waziri wa Fedha na Mhe. Adam Kighoma Ali MALIMA (Mb) Naibu Waziri wa Fedha na baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya fedha. (PICHA NA IKULU)
MAWAZIRI na manaibu waziri walioteuliwa kushika nafasi mbalimbali jana waliapishwa na Rais Jakaya Kikwete katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam, huku baadhi yao wakianza na tambo za uwajibikaji  na wengine wakiomba ushirikiano wa karibu kutoka kwa wadau ili waweze kutimiza majukumu yao.
Rais Kikwete na Mhe. Mathias Meinrad CHIKAWE (Mb) Waziri wa Mambo ya Ndani wakiwa na wakuu wa vyombo vilivyo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani.
Wakizungumza na waandishi wa habari, baadhi ya mawaziri hao, Saada Mkuya Salum (Wizara ya Fedha na Uchumi), Juma Nkamia (Naibu Waziri  Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na  Michezo) na Dk. Asha-Rose Migiro (Wizara ya Katiba na Sheria), kila mmoja aliomba ushirikiano kutoka kwa wadau na Watanzania kwa ujumla.
Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, alisema changamoto ya kwanza atakayokabiliana nayo ni kuimarisha eneo la fedha ili nchi iweze kujitegemea na kuwabeza wanaomwita ‘waziri mzigo’, wasubiri waone utendaji wake.
Akizungumzia suala la mishahara ya wafanyakazi, alisema kama kuna upungufu uliojitokeza kipindi cha nyuma kwa mishahara kuchelewa, halitajirudia na kwamba mishahara itatolewa kwa wakati husika.
Alisema wanachotarajia kufanya kama wizara ni kuimarisha mapato ya ndani ili kuweza kuondokana na utegemezi wa mataifa mengine, hasa katika miradi ya ndani.

Alisema lazima serikali ijielekeze katika kupata miundombinu ya kiuchumi kwa ajili ya kuondoka katika hatua ya sasa na kuelekea hatua nyingine.
Aliongeza kuwa wakati wa uhai wa William Mgimwa, kuna mipango mingi ya kimaendeleo waliyofanya na kuahidi kuitekeleza kwa nafasi yake mpya ya uwaziri.
“Mimi sijui dhana ya kuitwa mizigo ina tafsiri gani, ninachojua ni kuwa Katibu Mkuu wetu, Kinana, alikuwa mikoani na wananachi walikuwa wanalalamikia baadhi ya mambo, hivyo ilikuwa ni wajibu wake kutuita na kupata ufafanuzi wa yale yaliyokuwa yanalalamikiwa na wananchi na si kwamba sisi ni mizigo,” alisema Mkuya.
Mwigulu aahidi kupambana na fedha chafu
Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi (Sera), Mwigulu Nchemba, amesema jambo la msingi atakalolitilia mkazo ni udhibiti wa fedha chafu na kwamba hiyo ni moja ya sekta iliyo katika Benki Kuu.
Alisema taasisi za kifedha zitafanya uchambuzi wa kitaalamu na  kisha kuwasilisha bungeni mipango dhabiti ya  kuwabana watu wanaotafuta njia ya kusafisha fedha haramu.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro, alisema alipokuwa nje ya majukumu ya kiserikali amejifunza mengi ambayo atayatumia katika majukumu yake ya sasa, huku akieleza kuwa uzalendo utatawala katika suala zima la upatikanaji wa Katiba mpya.
Alisema hataruhusu hisia za kichama zitawale katika kuwapatia Watanzania katiba waitakayo, kwa kile alichoeleza kuwa mchakato wa katiba unamhusu kila Mtanzania pasipo kuangalia itikadi yake ya chama.
Nkamia alilia ushirikiano kwa waandishi

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia, kwa upande wake alisema pasipo ushirikiano kutoka kwa wadau wasitegemee miujiza katika sekta nzima ya habari.

“Naomba kila mmoja wetu kwa nafasi yake ashiriki na tushirikiane, katika hili hakuna muujiza utakaofanywa na mtu mmoja, hasa ninyi ndugu zangu waandishi ni nguzo muhimu katika kutoa ushirikiano, naomba tushirikiane,” alisema Nkamia.

Mwanza waponda
Naye mwandishi, Sitta Tumma, kutoka Mwanza, anaripoti kuwa baadhi ya wananchi wakiwemo wanasiasa jijini Mwanza na mjini Musoma, mkoani Mara, wameponda na kubeza uteuzi huo, ambapo wameuita ni mtindo wa kupeana fadhila na kutesa kwa zamu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, baadhi ya wananchi na wanasiasa hao walisema baraza hilo ni mzigo usiobebeka kwa wananchi, na Rais Kikwete amejitwisha mzigo ambao hatima yake ni kiama kwa taifa, kwani Watanzania walitarajia kuona mawaziri wawajibikaji, na si watu wa kutafuta fedha za uchaguzi mwaka 2015.

Walieleza kushangazwa na kuingizwa wizarani Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Mwigulu Nchemba, ambaye amepewa Unaibu Waziri wa Fedha (Sera), Dk. Titus Kamani (Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi), Shukuru Kawambwa (Wizara nyeti ya Elimu), Hawa Ghasia (TAMISEMI), Juma Nkamia (Wizara ya Habari, Vijana,  Utamaduni na Michezo), Profesa Anna Tibaijuka (Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi), Lazaro Nyalandu (Wizara ya Maliasili na Utalii), pamoja na Mathias Chikawe kupewa Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mwenyekiti mstaafu wa CCM Wilaya ya Nyamagana, jijini hapa, Athumani Zebedayo, alieleza kushangazwa na hatua ya Rais Kikwete kumbakisha serikalini Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa na mawaziri wengine mizigo waliotakiwa na CCM kuondolewa.

Alisema kuachwa kwa mawaziri hao kunatia shaka iwapo kuna dhamira ya kweli ya kuwasaidia wananchi kupata maendeleo yaliyodumaa, na kwamba ni maajabu pia kuingizwa katika baraza hilo, Nchemba, Dk. Kamani, Ghasia, Chikawe, Nyalandu, Tibaijuka na Nkamia, kwani watu hao hawawezi kuwasaidia wananchi maskini.
(CHANZO NI TANZANIA DAIMA/ PICHA NA IKULU)

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate