EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 30, 2014

WAPO MASUPASTAA, MASTAA NA WAIGIZAJI


NITAELEWEKA tu! Sina ubishi kwamba kwa sasa Bongo, fani ya sanaa ya uigizaji ndiyo imeshika kasi kukubalika katika jamii (anayebisha anyooshe mkono, najua hakuna).
Elizabeth Michael 'Lulu'.
Siku hizi ukikatisha kwenye mitaa mbalimbali nchini Tanzania, hasa uswahilini, utagundua wengi wanaangalia ‘filamu za akina Kanumba’ kama vile Uncle JJ, Ndoa Yangu, Mr. Ben, World of Benefit na nyingine nyingi.
Haya ni maendeleo kwa wasanii wetu ambao zamani walikuwa wakihaha kutoka lakini walishindwa kutokana na soko la filamu Bongo kushikwa na ‘muvi za akina Rambo’ na baadaye akina Noa Ramsey.
ANGALIZO LANGU
Pamoja na yote hayo, kuna angalizo langu. Ili sanaa hiyo izidi kukua nchini ni lazima kuwe na ushirikiano mkubwa kati ya wasanii wenyewe (waigizaji) na vyombo vya habari.
Aunt Ezekiel.
Vyombo vya habari ndivyo vinavyotangaza kazi zao mpaka zikajulikana na akina mama Nyakomba kule kijijini Songea (nyumbi hii, bomba hii).
Lakini kumekuwa na ugumu wa ushirikiano kutoka kwa baadhi ya waigizaji, hasa wale ambao wanajiita (hawaitwi) wanajiita masupastaa au mastaa wa Bongo (Bongo Movies).  
Hawa jamaa baada ya kuamini wamekuwa na majina makubwa kupitia filamu (ni vyombo vya habari vilivyowafanya wawe na majina makubwa) wamekuwa na dharau, wamekuwa bize, wamekuwa hawana nafasi, simu wamekuwa wakiziweka mbali na wao walipo au hazina chaji tangu jana usiku (si unajua umeme wa Tanesco?).
Jack Wolper.
MBAYA ZAIDI
Mbaya zaidi, hao ‘mastaa’ wapo hata wale waliokwishaonekana kwenye filamu tatu tu tena si ‘mastering’, waliigiza kwenye udereva, kufungua mageti, wakaribisha wageni maofisini au wasaidizi wa kazi za ndani ‘mahausigeli’.
NINAVYOJUA MIMI
Kwa mujibu wa ufahamu wangu mdogo ni kwamba, katika kila tasnia duniani kuna masupastaa na mastaa. Pia wapo wahusika wa fani husika. Kama filamu tunasema waigizaji.
Sasa hawa wa Bongo ambao nao pia wamejiweka kwenye kundi la masupastaa na mastaa wananitatiza kila kukicha, kwamba ni wagumu kupatikana, iwe laivu au kwa simu kwa sababu wao ni maarufu katika fani.
 
Jacob Steven 'JB'.
MASUPASTAA
Kufuatia lawama zangu hizi kwa wasanii wa fillamu Bongo, kama mtu ataniuliza ninavyojua mimi nani supastaa, staa na mwigizaji orodha yao ninayo na niko tayari kuiweka wazi.
Siwezi kusema Ray, JB, Aunt Ezekiel, Nora, Wolper, Johari, Natasha, Monalisa, Dk. Cheni, Riyama Ali, Lulu, Mzee Majuto, Mzee Small siyo mastaa wa filamu Bongo.
Wamecheza filamu nyingi, wamejenga majina makubwa kupitia sanaa hiyo. Japokuwa miongoni mwao wapo ambao ni wababaishaji kwenye kupokea simu na kujifanya ‘aghali’ kupatikana.
Lakini pia kuna kundi la mastaa wa filamu za Bongo; hawa ni akina Baba Haji, Kuambiana, Maya, Jini Kabula, Wastara, Mr. Chuz, Frank Mwikonge, Mzee Chilo, Mzee Magali, Cloud, Penina, Richie, Bi. Chau na Thea.
Wengine ambao kwangu ni mastaa ni, Jack wa Chuz, Cathy, Lucy Komba, Big, Chekibudi, Baba Haji, Kelvin, Odama, Rose Ndauka, William Mtitu, Tino, Flora Mvungi, Nisha, Shilole, Mainda, Shamsa Ford, Snura, Mlela, Shumileta, Hemed, Yusuf Mlela, Dude na Maya.
Mbali na makundi hayo, kuna ambao wamepitiliza usupastaa na sasa wameingia kwenye kundi la wakongwe wa sanaa. Hawa ni kama akina Natasha, Mzee Small, Mzee Majuto, Bi. Hindu, Bi. Mwenda, Bi. Chau, Kemmy na Muhogo Mchungu.
Mzee Majuto.
Lakini napata tabu kusema, Batuli, Zamda, Tiko, Slim, Skaina, Rachel Haule, Chikoka, Kupa, Mafufu, Badra na wengine wengi ambao kwenye fani hawana hata mwaka mmoja ni mastaa.
Kwa nchi za wenzetu ‘majuu’, vyombo vya habari havitambulishi kila mwigizaji kama staa, ila wanakuwa mastaa katika filamu walizocheza tu, hususan kama amecheza filamu mbili au tatu.
Mfano; wakitaka kumtambulisha Rachel Haule watasema: “Staa wa filamu ya…..(wataitaja jina), Rachel Haule amepata mchumba (mfano lakini).
Majuu staa, kama wa filamu ni yule aliyekwishacheza muvi zaidi ya 10 akiwa ni stering na zikatikisa. Kibongobongo, hata akicheza filamu moja halafu akavuma sana, tena wengine huvuma kwa mambo nje ya filamu, ni staa.
Makala haya ni mtazamo wangu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate