EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 20, 2014

MAKUBWA! MAMA WEMA AKESHA AKIOMBA DIAMOND AFUMANIWE

MAMA wa Miss Tanzania 2006 aliye pia staa wa muvi za Bongo, Wema Sepetu, Mariam Sepetu amesema anamwomba Mungu bintiye huyo amfumanie mpenzi wake asiyemkubali, Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Amani  lina picha kamili.
Wema na Diamond.
Akizungumza na mapaparazi wetu juzikati jijini Dar es Salaam, mama Wema alisema:
“Najua kwa sasa sina tena mamlaka ya kuingilia mapenzi ya binti yangu kwani mambo hayo yamenichosha, yananiumiza na kichwa.
“Lakini naomba sana kwa Mungu itokee siku moja Wema amfumanie Diamond akiwa na mwanamke mwingine labda ndiyo itakuwa kikomo chao cha kuwa wapenzi kwani ndiyo ndoto ninayoiota kila siku.”
KWA NINI ANAOMBA DUA BAYA?
Mama Wema alikwenda mbele zaidi kwa kusema kwamba, amegundua binti yake huyo hana ubavu wa kuachana na Diamond hata kama atasikia ana mwanamke mwingine.
Mama Wema, Mariam Sepetu.
MAGAZETI PIA YAMESHINDWA
Mwanamke huyo anayemwogopa Mungu tu, alikwenda mbele zaidi kwa kusema kwamba, kuna wakati baadhi ya magazeti pendwa nchini yaliandika Diamond kuwa na demu mwingine lakini Wema hakukasirika wala kuachana na staa huyo wa muziki wa kizazi kipya.
MSIKIE MWENYEWE
“Kwa hiyo mchezo mzuri ni yeye (Wema) kumfumania huyo Diamond wake, maana magazeti tu  kuandika kwamba ana uhusiano na mwanamke mwingine mwanangu alivyofanywa mjinga wa kutupwa, hatamwacha.
“Mimi najua Wema anashindwa kukaa chonjo kwa sababu ndumba zimemtawala, amefunikwa labda baadaye atafunguka,” alisema mama Wema.
AIGUSA SAFARI YA DIAMOND NCHINI NIGERIA
Mama Wema akaanika jambo ambalo halijawahi kujulikana kabla.
Alisema: “Huyo Diamond ndo maana alikwenda Nigeria akashindwa kupiga muziki kwa sababu hakwenda na Wema, sasa ameona ampumbaze ili aweze  kwenda naye nchi za nje kwa masilahi yake binafsi, ataishia kumuahidi tu hana uwezo wa kumnunulia Wema kitu chochote chenye thamani kubwa, ni mpenda misifa tu. 
“Si mnamjua huyo ni mtoto wa Tandale? Anajiita yeye m...(alitaja jina la kinyesi) na kweli yuko hivyo.
NDUGU WA DIAMOND WAMEJAZANA KWA WEMA
“Ndugu zake walivyo washamba wamejazana hovyo pale kwa Wema. Wajinga mno, maana mshamba siku zote ni mshamba,”     alisema mama huyo.

HATAKI KUSIKIA WEMA ANA MIMBA YA DIAMOND
Katika hali iliyoonesha kwamba kweli hampendi Diamond, Bi. Mariam alisema hataki kusikia binti ana ujauzito wa msanii huyo.
Alisema: “Mbegu (uzao) gani atakayoileta kwangu, huyo mjukuu si atakuwa balaa, siwezi kuharibiwa wajukuu. Mtoto asiyeeleweka siwezi kumshika.”
Wema.
ACHIMBA MKWARA
“Halafu nataka kuwaambia enyi watu wa magazeti, haya mambo ya kumwongelea huyo domo acheni mara moja, dunia itamnyoosha,” alisema.
AJIRUDI KWA MWANAYE
Mama Wema alisema hawezi kumlaumu sana binti yake  kwa vile akili si yake, yeye (Wema) ni mwanake na atabaki kuwa mwanamke, ila siku zote lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho.
DIAMOND SASA
Juzi, Amani lilimtafuta Diamond kwa njia ya simu na kumjulisha kuhusu ndoto za mama mkwe wake huyo ambapo aliishia kucheka.
“Teh! Teh! Teh! Thubutu.”
Diamond.
HAIJAWAHI KUTOKEA
Kumbukumbu za makabrasha ya Amani zinaonesha kwamba, katika historia ya wapenzi wa Wema, mzazi huyo hakuwahi kutokea kumkubali Diamond hata siku moja tu.
Amekuwa akimshukia mara kwa mara, madai yake siku zote ni kwamba, katika maono yake hajawahi kuona mapenzi ya kweli ya Diamond kwenda kwa Wema.
Japokuwa pia hajawahi kusema kama kuna mapenzi ya kweli ya Wema kwa Diamond.
Wema amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na marehemu Steven Kanumba, Jumbe Yusuf, Chalz Baba na Clement ‘kigogo wa ikulu’. Pia amewahi kudaiwa kutembea na TID na Mr Bluu.
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate