EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 14, 2014

REDIO NYINGI HAZINA HABARI ZA USAWA WA KIJINSIA - UMOJA WA MATAIFA‏

DSC_0010
Mshehereshaji Meneja wa Maadili wa Baraza la Habari Tanzania( MCT), Bw. Allan Lawa, akiwakaribisha wageni waalikwa kwenye maadhimisho ya siku ya Redio Duniani yaliyofanyika Kitaifa mkoani Dodoma. Maadhimisho hayo yameandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) na kufadhiliwa na UNESCO.
Na Mwandishi Wetu, Moblog Tanzania, Dodoma
UMOJA wa Mataifa umesema kwamba bado redio nyingi duniani ziko nyuma katika kuhabarisha habari za usawa wa jinsia na sauti za wanawake na wasichana hazipati nafasi ya kutosha katika matangazo ya kila siku katika vyombo vingi vya habari.
Akisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw, Ban Ki-Moon na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi Irina Bokova, katika maadhimisho ya siku ya Radio Duniani jijini Dodoma, Afisa Habari wa umoja wa Mataifa, Bi Usia Nkhoma Ledama amesema mbaya zaidi katika bodi za mashirika ya vyombo vya habari wanawake ni robo tu ya wanabodi.
“Ninavihimiza vituo vya redio kuwatambua kwa usawa wanawake kama wafanyakazi na kama wasikilizaji wake,”
“Maadhimisho ya mwaka huu yanatukumbusha wajibu wa watangazaji wa redio duniani kote kuipaza sauti ya wanawake na kuthamini nafasi ya wanawake katika mashirika ya utangazaji,” akisoma taarifa hiyo
Bi Usia akisoma taarifa hiyo amesema Radio pia inaweza kusaidia sana kumaliza unyanyapaa dhidi ya wanawake na programu zisizozingatia usawa wa kijinsia kwa wote.
DSC_0019
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi akisalimiana na Mkufunzi wa Redio za Jamii kutoka Unesco, Mama Rose Haji Mwalimu meza kuu wakati wa maadhimisho ya siku ya Redio Duniani yaliyofanyika Kitaifa mkoani Dodoma. Katikati ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. Kajubi Mukajanga.
Amesema kwenye hotuba hiyo ya wakuu wa Umoja wa Mataifa kwamba hii ni fursa kwao wote, kusherehekea Siku Ya Radio Duniani kwa kuwatambua wanawake na kufanya yale yaliyo ndani ya uwezo wao kuzilea sauti mpya za kesho.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi Irina Bokova amesema na ninanukuu; Katika Siku ya Redio Duniani, tunaadhimisha chombo ambacho kinategemewa zaidi na watu wengi, wanaume kwa wanawake, duniani kote. Redio huwapa sauti wale wasio na sauti, husaidia kuelimisha watu wasio na elimu, na inaokoa maisha wakati wa majanga.
Akisoma taarifa hiyo amesema ikiwa ni chachu ya uhuru wa kujieleza na ushirikishwaji wa wengi, redio ni muhimu katika kujenga jamii yenye uelewa na kukuza heshima na uelewano baina ya watu.
DSC_0036
Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari (MCT), Bw.Kajubi Mukajanga akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Rehema Nchimbi.
Ujumbe huo wa Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO ulisisitiza kwamba Radio ni muhimu zaidi katika kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake.
“Tangu wakati wa watendaji waanzilishi mwanzoni mwa karne ya 20 hadi hawa wa sasa wanaoripoti kutoka kwenye maeneo yenye vita, wanawake wamefanya kazi kubwa katika ukuaji wa redio,Kama waandishi wa habari wa kiraia, maripota, watengenezaji vipindi, mafundi, na watu muhimu wanaofanya maamuzi, wanawake wanafanya kazi katika kila ngazi ya sekta ya utangazaji kuhakikisha ubadilishanaji huru wa maoni, habari na mawazo kupitia masafa,” ilisema taarifa hiyo.
Bi Usia amesema kupitia ujumbe huo kwamba ni kwa sababu hiyo UNESCO inafanya kazi duniani kote kuendeleza radio kama chombo huru na kinachoshirikisha watu wengi kwa ajili ya wanaume na wanawake, na kutengeneza mazingira salama zaidi kwa waandishi wa habari wote, kwa kutambua kwa namna ya pekee vitisho kwa waandishi wa habari wanawake.
DSC_0120
Pichani juu na chini ni Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Rehema Nchimbi akizungumza na wadau wa sekta ya Habari nchini kwenye maadhimisho ya siku ya Redio Duniani yaliyofanyika Kitaifa mkoani Dodoma.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dr.Rehema Nchimbi ambaye aliwaasa waandishi kutangaza vipindi vyenye manufaa kwa jamii ili kusaidia kusukuma maendeleo.
“Tungependa kusikia vipindi vya maendeleo zaidi katika redio kuliko vipindi vya muziki,”alisema
Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari (MCT)Kajubi Mukajanga alisema maadhimisho hayo yamewashirikisha washiriki kutoka nchi nzima na yanalenga kuwakumbusha wajibu watangazaji wa redio juu ya nafasi ya radio katika kuelimisha jamii.
DSC_0103 DSC_0157
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa(UNIC), Bi. Usia Nkhoma Ledama, akisoma Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi Irina Bokova katika Maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani.
DSC_0288
Mchokonozi wa Mada na Mkufunzi wa Redio za Jamii kutoka Unesco Mama Rose Haji Mwalimu akiwasilisha mada inayosema kutumia fursa ya Redio kukuza usawa wa Kijinsia na kuwawezesha Wanawake katika Uongozi.

DSC_0181
Meneja Machapisho, Utafiti na Uhifadhi Hati wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. John Mireny, akitoa maelezo mafupi kuhusu machapisho mbalimbali ya baraza hilo yanayotoa mafunzo mbalimbali ya tasnia ya habari.
DSC_0218
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi akizindua machapisho ya Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwenye maadhimisho ya siku ya Redio Duniani. Kushoto ni Mkufunzi wa Redio za Jamii kutoka Unesco Mama Rose Haji Mwalimu na Kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari (MCT), Bw.Kajubi Mukajanga.
DSC_0225
DSC_0045
Baadhi ya Wadau wa Sekta ya Habari, Watangazaji na waandishi wa Redio za Jamii nchini wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya Redio Duniani yaliyofanyika Kitaifa mkoani Dodoma.
DSC_0052
DSC_0024
DSC_0066
DSC_0063
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma Ledama akifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani.
DSC_0060
Wadau wa UNESCO na MCT.
DSC_0323
Baadhi ya waandishi wa habari wa Redio za jamii nchini na wadau wa sekta ya habari wakichangia maoni wakati wa majadiliano ya kuzungumzia changamoto zinazozikabili redio za jamii nchini.
DSC_0321
DSC_0274
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa Sekta ya habari walihudhuria maadhimisho ya siku ya Redio duniani yaliyofanyika Kitaifa mkoani Dodoma kwa mara ya kwanza.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate