EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, March 31, 2014

DIAMOND ATAMANI USHOGA!..BAADA YA KUTAJIRIKA, FEDHA ZAMCHANGANYA SASA

NYOTA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amewashangaza watu kufuatia kuvaa wigi (nywele bandia) la mpenzi wake, Wema Isaac Sepetu, kitendo kilichotafsiriwa kuwa ni dalili ya kutamani mambo ya ushoga.
Diamond alinaswa akiwa amevaa wigi hilo kichwani kisha kupiga nalo picha.
ILIVYOKUWA
Hivi karibuni, Diamond alinaswa akiwa amevaa wigi hilo kichwani kisha kupiga nalo picha huku Wema akilitafuta ili alitinge bila mafanikio.
Habari zilieleza kuwa baada ya Wema kutoka nje akiendelea kulitafuta wigi hilo, alipigwa na butwaa kumkuta Diamond amelivaa, tena akionekana kuwa na amani.
Wema Isaac Sepetu na mpenzi wake Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
WEMA AMWANIKA
“Jamani nimetafuta wigi langu muda mrefu sijaliona, nashangaa namkuta baby wangu (Diamond) amelivaa, lakini limempendezaje?” aliandika Wema kwenye ukurasa wake wa Instagram uliotembelewa na watu kibao.


WANACHOAMINI WATU KUHUSU USHOGA
Kitendo cha Diamond kuvaa wigi hilo, wengi wamekichukulia kama ni dalili zake za kupenda kuwa kama demu ambapo kwa mwanaume huitwa shoga, kwa vile wenye tabia hizo wengi walianza kwa kujihusisha na mambo ya kikekike, yakiwemo mavazi.

Emmanuel Adebayor (kushoto) na Diamond Platnumz wakiwa Four Point Hotel, jijini Lagos nchini Nigeria.
“Unajua watu wengi wanaojiingiza katika mambo ya ushoga huanza kwa kutamani kuvaa vitu vya kike kama nguo, hereni, viatu, kujipodoa na vingine vingi,” alisema staa mmoja ambaye hakutaka kutajwa gazetini.
WANAOMFAHAMU DIAMOND
Watu ambao wanamfahamu vizuri mwanamuziki huyo, walisema huenda fedha ambazo ameanza kuzipata hivi karibuni zimekuwa zikimpeleka puta kwa kufanya vitu ambavyo si sahihi.
ALIANZA MUDA
Miezi kadhaa iliyopita, Diamond na Wema walipokutana nchini China, jamaa huyo alipiga picha zilizomuonesha akiwa amevaa cheni ya mpenzi wake huyo na kuziweka kwenye mtandao wake wa kijamii wa Instagram.

Jokate Mwegelo.
SURUALI KAMA YA WEMA, JOKATE
Mwaka jana akiwa nchini Nigeria, Diamond aliingizwa kwenye mitandao ya kijamii kufuatia kitendo chake cha kuvaa suruali yenye mistari ya pundamilia ambayo wachunguzi walibaini kuwa, Wema na Jokate Mwegelo pia wanazo.
Jokate (kushoto) na Wema.
TABIA ZA MASTAA WAKIKAMATA FEDHA
Mastaa wengi duniani wamekuwa na tabia ya kufanya vitu ambavyo ni kinyume na maadili mara baada ya kupata ustaa na kushika fedha nyingi.
Mfano mkubwa, aliyekuwa mfalme wa Pop duniani, marehemu Michael Jackson, yeye alianza kufanya vituko kwa kujibadilisha ngozi na pua  mwaka 1984 ili aonekane mweupe. Ni baada ya kuwika kwenya anga la muziki huku kiasi kikubwa cha fedha kikiingia mfukoni mwake.
Hali hiyo ilimsababishia kupata ugonjwa wa Vitiligo hadi akaaga dunia Juni 25, 2009.

ELTON JOHN
Mwanamuziki Elton John wa Uingereza, naye alijikuta akijibadili na kuwa shoga baada ya kuzikamata fedha nyingi.
Mwaka 1984, Elton John alifunga ndoa na mwanamke aliyeitwa Renate Blauel. Mwaka 1988 walitengana, Elton akajiingiza katika mapenzi ya jinsi moja hadi kufikia hatua ya kufunga ndoa na mwanaume mwenzake, David Furnish mwaka 2005.
WHITNEY HOUSTON
Mwanamuziki mwingine ambaye alijizolea umaarufu mkubwa kutokana  na sauti yake nzuri ni Whitney Elizabeth Houston ambaye baadaye alijiingiza kwenye masuala ya usagaji na matumizi ya madawa ya kulevya ambayo aliyatumia kwa muda mrefu na kumsababishia kifo.
Whitney alifariki dunia mwaka 2013 katika bafu la Hoteli ya Baverly Hills nchini Marekani. Vyombo vya habari vilimwelezea marehemu huyo kuwa, alitumbukia kwenye matumizi ya ‘unga’ kwa sababu ya kumiliki mkwanja mnono akiwa na mumewe, Bobby Brown.
UZOEFU
Uzoefu kwamba mashoga wengi huanza kwa kupenda vitu vya mademu upo kwa baadhi ya vijana Bongo ambao nao ni ‘chakra’. Wengi waliowahi kuzungumza na vyombo vya habari wamekuwa wakisema kuwa walikuwa wakipenda kuongozana, kukaa, kuvaa au kulala kwenye vyumba vya dada zao.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate