EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, March 27, 2014

UONGOZI WA DAMPO WAAGIZWA KUREKEBISHA MIUNDOMBINU YA BARABARA‏

DSC_0458
Gari la Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick likiwasili Dampo kuu la taka la Pugu Kinyamwezi, lililopo maeneo ya Gongo la Mboto jijini Dar alipofanya ziara ya ghafla kwenye dampo hilo.(Picha na Zainul Mzige wa MOblog).
Na. Damas Makangale, MOblog
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick ametoa agizo mara moja kwa uongozi wa Dampo nje kidogo la jiji la Dar, Pugu Kinyamwezi, kurekebisha miundombinu ya barabara pamoja na taa ili kurahisisha umwagaji wa taka katika dampo hilo. MOblog inaripoti
Akizungumza na baadhi ya viongozi wa wilaya na jiji hivi karibuni baada ya kufanya ziara ya ghafla katika maeneo kadhaa ya jiji la Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa amesema tatizo la miundombinu ya barabara kuelekea katika Dampo la Pugu Kinyamwezi linasababisha foleni kwa malori ya kusomba taka katika jiji la Dar.
“mara ya mwisho wakati nakuja hapa kukagua hili dampo kulikuwa na taa na kazi ilikuwa inafanyika usiku na mchana sasa kumetokea nini,” alihoji Mkuu huyo wa Mkoa
Sadick aliagiza kwa viongozi wa jiji kushughulikia haraka tatizo la miundombinu ya barabara kuelekea Dampo ili kuongeza tija katika kazi ya kumwaga na kusomba taka katika jiji la Dar es Salaam.
DSC_0468
Kaimu Mkuu wa Idara ya Udhibiti taka kutoka halmashauri ya jiji, Bi. Enezael Ayo (kushoto) akifafanua jinsi magari ya taka yanavyomwaga taka katika dampo kuu taka la Pugu Kinyamwezi jijini Dar wakati wa ziara ya Mkuu wa mkoa wa Dar.
Alisisitiza kwamba utaratibu mbovu wa umwagaji taka na miundombinu mibovu katika Dampo la Pugu Kinyamwezi vinasababisha mrundikano wa taka katika manispaa zote za Temeke, Ilala na Kinondoni.
Amesema kwamba ni muhimu kwa viongozi wa jiji kupata nguvu kazi ya kutosha ili kuwe na watu watakaosimamia umwagaji wa taka wakati wa usiku ili kudhibiti madereva wakorofi wanaomwaga taka ovyo bila kuzingatia taratibu.
Sadick aliongeza kuwa watendaji wa jiji ni lazima wawe na utaratibu wa kutoa mafuta kwa wakati kwenye magari ya kusomba (Bull Dozer) na vitendea kazi vingine.
DSC_0485
Mkuu wa mkoa wa Dar, Said Meck Sadick akitoa agizo mara moja kwa uongozi wa Dampo nje kidogo la jiji la Dar, Pugu Kinyamwezi, kurekebisha miundombinu ya barabara pamoja na taa ili kurahisisha umwagaji wa taka katika dampo hilo. Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ndg. Raymond Mushi(mwenye suti nyeusi).
Wakati akitembelea maeneo kadhaa kati kati ya jiji kuanzia soko la Kisutu na mitaa ya Libya, Mkuu wa Mkoa aliagiza mamlaka zinazohusika kushughulikia haraka tatizo la maji machafu kupunguza harufu na kuzuia magonjwa ya mlipuko.
“nawaagiza mkae pamoja na mje na mpango mkakati utakaowezesha kumaliza tatizo la maji machafu yanayotoka katika mitaro na mifereji ya maji machafu katika ya jiji,” aliongeza
Wakati huo huo, wadau kadhaa wa usombaji taka katika jiji la Dar es Salaam wameomba serikali kutoa kipaumbele kwa Dampo la Pugu Kinyamwezi na kulitengea bajeti ya kutosha ili liweze kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
DSC_0479
Mkurugenzi Mtendaji wa Tirima Enterprises, Bw. Robert Ngeleshi akizungumzia changamoto na matatizo ya mawakala wa kusomba taka katika jiji la Dar ambao waliongozana na Mkuu wa mkoa kwenye ziara hiyo.
DSC_0557
Mkuu wa mkoa wa Dar, Said Meck Sadick aliyeambata na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ndg, Raymond Mushi wakiondoka eneo la tukio mara baada ya kuhitimisha zoezi la kukagua miundo mbinu ya Dampo la taka la Pugu Kinyamwezi. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Minael Mshanga.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate