EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, April 21, 2014

BALAA LA PASAKA


KIFO njenje! Baba aliyetajwa kwa jina moja la Nuhu maarufu kama ‘Mzee Kijana’ (54), nusu auawe na raia wenye hasira kali, msimu wa Pasaka kisa kikiwa ni kuachiwa kwa dhamana isiyoeleweka baada ya kunaswa kwa kosa la ulawiti wa madenti.
Baba aliyetajwa kwa jina moja la Nuhu maarufu kama ‘Mzee Kijana’ (54) anusurika kifo baada ya fumanizi Aprili 19 (Ijumaa Kuu), mwaka huu maeneo ya Tuangoma Mjimwema, Kigamboni jijini Dar.
Tukio hilo la kutisha lilijiri Aprili 19 (Ijumaa Kuu), mwaka huu maeneo ya Tuangoma-Mjimwema, Kigamboni jijini Dar,  mbele ya ofisi ya serikali ya mtaa huo ambapo awali, Aprili 9, mwaka huu ilidaiwa kuwa mzee huyo alidakwa na mmoja wa wazazi wa wanafunzi hao akiwa amemfungia kwa kufuli mwanaye ndani ya chumba chake huku mwenyewe akiwa katika shughuli zake za kuuza kuni.

Picha inaonyesha gari lililotumika kumchua mpaka kituoni.
Ilisemekana kwamba akiwa na mjumbe wa kitongoji hicho, mzazi huyo aliyepata fununu kuwa mwanaye wa kiume analawitiwa na mzee huyo, alifanya jitihada za kumsaka mzee huyo hadi kibaruani kwake ambapo alipohojiwa kama amemfungia mwanafunzi wake ndani ya chumba chake, mzee huyo alijiumauma na mwishoni kukubali.
Mzee huyo akijaribu kujificha kwa aibu.
Ilidaiwa kwamba wananchi na mzazi wa mwanafunzi huyo walimbeba mzee huyo msobemsobe hadi nyumbani kwake na kumtaka amfungue denti huyo ambapo alifanya kama alivyoagizwa kisha mwanafunzi huyo alichomolewa ndani ya chumba hicho.
Habari zilieleza kuwa sakata hilo lilitinga katika ofisi ya mtendaji ambapo walitoa taarifa kwa askari wa Kituo cha Polisi cha Kizuiani. Hata hivyo, ilisemekana kwamba askari hao walishindwa kufika kwa kuwa siku hiyo daraja la Kongowe lilikuwa limeharibika.
Ilisemekana kuwa baadaye walipata msaada kutoka kwa polisi wa Kituo cha Kibada, Kigamboni ambao walimchukua mtuhumiwa na baadaye kupelekwa Kizuiani kwa ajili ya taratibu za kisheria huku mwanafunzi huyo akipewa PF-3 kwa ajili ya uchunguzi kama kweli alikuwa akiingiliwa kinyume na maumbile.
Baadhi ya raia wenye hasira kali wakiwa nje ya kituo cha polisi alipofikishwa mtuhumiwa huyo.
Ilidaiwa kuwa kabla hata majibu ya daktari hayajachukuliwa, Mzee Kijana alionekana akirandaranda mitaani, jambo lililosababisha viongozi wa mtaa huo kuwasiliana na polisi kuhoji kulikoni?
Ilielezwa kuwa wakati wakuu hao wakihangaika na suala hilo ndipo wananchi wenye hasira kutoka kila upande waliivamia ofisi hiyo wakidai kuwa wamechoshwa na rushwa za wazi zinazofanywa na viongozi wao na kudai kuwa watampa adhabu mzee huyo wao wenyewe.
Ilidaiwa kwamba kufumba na kufumbua, watu hao wasio na idadi walivunja mlango na kumchomoa Mzee Kijana aliyekimbilia ofisini humo kwa ajili ya hifadhi na kuanza kumshambulia kwa kila aina ya silaha kiasi cha almanusura kumuua.
Kipigo hicho kilisababisha askari waliofika hapo ili kutuliza ghasia, kushindwa kazi, jambo lililowalazimu kutoka nduki ili kuokoa roho zao. Akizungumza na wanahabari wetu, mwenyekiti wa mtaa huo, Mohamed Chande alisema kuwa ilibidi aikimbie ofisi yake kwa kuwa watu walikuwa na ghadhabu kupita maelezo.
Inadaiwa kuwa msamaria mwema mmoja alimnyakua Mzee Kijana kutoka katika kundi la watu na kumpakiza kwenye gari lake haraka na kumsalimisha mikononi mwa Polisi wa Kizuiani ambapo inadaiwa kuwa hadi sasa yupo huko.
Akizungumza na waandishi wetu, bibi wa mwanafunzi huyo anayedaiwa kulawitiwa aliyejitambulisha kwa jina moja la Rugwesi (38), alisema kuwa alishangaa kuona mtuhumiwa akiachiwa kwa dhamana siku chache kabla hata majibu ya daktari hayajatoka.
“Ripoti imeonesha kuwa mjukuu wangu alikuwa akilawitiwa kwa muda mrefu na mzee huyo na si mjukuu wangu tu inadaiwa anawafanyia hivyo wanafunzi wengine watatu,” alisema bibi huyo huku simu ya mkuu wa Kituo cha Polisi Kizuiani ikiita bila kupokelewa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate