EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, April 19, 2014

LULU AOGESHWA POMBE UKUMBINI

Stori: Musa Mateja na Gladness Mallya
Kha! Katika hali isiyoitarajiwa, nyota wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ amejikuta akiangua kilio cha ukweli kama mtoto kufuatia kuogeshwa kwa pombe mwilini, jambo ambalo hakulitarajia, Risasi Jumamosi limetonywa.
Nyota wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ akimwagiwa pombe kwenye birthday yake.
Tukio hilo la aina yake lilijiri Aprili 16, mwaka huu ndani ya Hoteli ya Regency, Mikocheni jijini Dar es Salaam ambapo
                                                               Keki iliyoandaliwa kwa ajili ya lulu
marafiki wa Lulu wasio mastaa walimwangushia ‘sapraizi’ ya nguvu ya kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa (bethidei). Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho kilizama ndani ya sherehe hiyo bila waalikwa wote kujua kuwa ni ‘shushushu’ wa kujitegemea, Lulu aliitwa kwenye sherehe hiyo akiwa hajui kitu japokuwa akilini mwake alitambua kuwa siku hiyo ni bethidei
yake.
TAARIFA YA AWALI
Awali, Risasi Jumamosi lilitonywa na mtonyaji wake wa habari za mastaa wa Bongo kwamba, Lulu siku hiyo anafanya bethidei ya

nguvu maeneo ya Mikocheni lakini eneo sahihi likiwa halijulikani.
“Jamani nawapa habari ya mjini kama kawaida yangu. Leo (Jumatano), Lulu anafanya bethidei. Nasikia ni Mikocheni, nimejaribu

kupeleleza ni sehemu gani nimeshindwa, kwa sababu ninyi ni wadaku hebu jiongezeni mpeleleze wenyewe,” kilisema chanzo hicho.
Kikaongeza: “Lakini nahisi kuna mazingira ya usiri. Hakuna staa hata mmoja atakayekuwepo kwa sababu sherehe yenyewe

imeandaliwa na marafiki zake wa kawaida.”

LULU APIGIWA SIMU, AKIRI, AKWEPA    
Baada ya chanzo hicho kuachia taarifa hiyo nyeti, Risasi Jumamosi lilimsaka Lulu kwa njia ya simu yake ya mkononi.
Risasi Jumamosi: Mambo vipi Lulu?
Lulu: Poa, niambie.
Risasi Jumamosi: Poa. Tumesikia leo ni bethidei yako, ni kweli?
Lulu: Ni kweli ndiyo.
Risasi Jumamosi: Itafanyika wapi?
Lulu: Mikocheni.
Risasi Jumamosi: Mikocheni sehemu gani?
Lulu: We tambua tu ni Mikocheni, mi mwenyewe sijui ni sehemu gani ndiyo nataka kwenda. Kwanza nimefanyiwa sapraizi na
marafiki zangu.

BAADA YA KUPIGWA CHENGA NA LULU
Baada ya Lulu kukwepa kutaja eneo la tukio, ndipo timu ya Risasi Jumamosi ikawasiliana na kamanda wa kikosi maalum cha

Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ na kumpa kazi ya kujua bethidei ya Lulu itafanyika wapi katika jijini la Dar es Salaam siku
hiyo.
NDANI YA DAKIKA 45
Ndani ya dakika arobaini na tano, kamanda wa OFM alirejesha majibu kwamba, sherehe hiyo itafanyika kwenye Hoteli ya Regency

iliyopo Mikocheni, Dar lakini hakutakuwa na mastaa na inafanywa kuwa siri ili mapaparazi wasijue na kufika kupiga picha.

KILICHOTOKEA
Usiku uliingia, Risasi Jumamosi likatia timu kwenye eneo la hoteli hiyo ambapo lilibahatika kumpata mtu mmoja akiwa anaelekea

kwenye sherehe hiyo.
Katika mazungumzo yake na Risasi Jumamosi, mtu huyo (jina lipo) alisema kila kitakachotokea ndani ya shughuli hiyo atakiweka

wazi ili mradi asitajwe jina gazetini tu!

BAADA YA SHEREHE
Saa saba na nusu usiku, sosi wetu huyo alilipigia simu Risasi Jumamosi na kuweka wazi yaliyotokea kwenye bethidei hiyo.
Sosi: Jamani shughuli imekwisha.
Risasi Jumamosi: Nini kimetokea?
Sosi: Lulu aliogeshwa pombe hivihivi nikishuhudia. Mbaya zaidi wale waliomwogesha nahisi walikuwa wanafanya makusudi, maana

walikuwa wanammiminia kuanzia kichwani hadi miguuni, yaani mwili wote chapachapa.
Risasi Jumamosi: Mwenyewe alikuwa anasemaje?
Sosi: Kilio. Lulu Amelia sana. Siyo kwamba alikuwa analia utani, ukweliukweli. Si unajua yeye aliacha kunywa pombe tangu ule

mkasa wake na marehemu Steven Kanumba, sasa leo kuogeshwa pombe hiyohiyo mwili mzima, nadhani ndiyo maana amelia sana.

MAMA YAKE AMSHANGAA
“Ilibidi Lulu ampigie simu mama yake (Lucresia Karugila) na kumweleza yaliyomkuta, akajuta hata kuhudhuria. Mama alishangaa

lakini alimuuliza kama yupo salama akasema yupo salama,” alisema shushushu wetu.

LULU ABADILI NGUO
Sosi huyo aliendelea kuweka wazi kwamba, baada ya kuwa chapachapa kwa kulowa pombe, Lulu aliyetengenezewa keki tano,

alilazimika kwenda kuoga na kubadili nguo mara mbili. Mwisho alivaa gauni la rangi ya kahawia.
“Naamini alibadili hata nguo za ndani, maana alilowa pombe mwili mzima,” kilisema chanzo hicho huku kikisisitiza kwamba jina
lake liwekwe kapuni.

MASTAA WAKAUKA
Ilidaiwa kuwa tofauti na shughuli nyingine za mastaa ambapo mastaa wenzake hujaa, bethidei hiyo ya Lulu mtu mwenye jina kubwa

Bongo aliyehudhuria sherehe hiyo ni Mahsin Awadh ‘Dk. Cheni’ peke yake.

KWA MAANA HIYO
Kwa sherehe hiyo, Lulu ametimiza miaka 19 tangu kuzaliwa kwake. Alizaliwa Jumapili ya Aprili 16, 1995.
CHANZO GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate