EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, April 25, 2014

MAZUNGUMZO NJIA PEKEE YA KUREJESHA AMANI YA KUDUMU DARFUR - GEN-MELLA

Jenerali Mella, Kamanda wa Jeshi la UNAMID akibadilisha mawazo na Balozi Mwinyi, ambapo pamoja na mambo mengine, amesema wanajeshi kutoka JWTZ ambao ni sehemu ya UNAMID wameendelea kuonesha weledi na kujituma kwa hali ya juu katika eneo la ulinzi wa amani, ulinzi wa raia na usimamiaji wa misaada ya kibinadamu. Akasema kutokana na mapingano ya kikabili yanajitokeza mara kwa mara, na kuwa sehemu kubwa ya mapigano hayo yamekuwa yakitokea katika maeneo zilipo kambi za wanajeshi kutoka Tanzania, wanajeshi wetu wamejikuta wakilazimika kutoa huduma mbalimbali zikiwamo za kuwazalisha wanawake waja wazito. Utoaji wa huduma hiyo ya uzazi salama nje ya mamlaka yao imewafanya wazazi waliojifungua kuwapatia majina ya kitanzania watoto wao, kama shukrani yao kwa madaktari hao wa kitanzania kwa kuokoa maisha yao na ya watoto wao. Kushoto kwa Jenerali Mella, ni Luteni Kanali, Wilbert Ibuge, Mwambata Jeshi katika Uwakilishi wa Kudumu
Luteni Jenerali Paul Mella, Kamanda wa Jeshi la Mseto la Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa katika Darfur ( UNAMID) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa ( hayupo pichani). Jenerali Mella alifika katika Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kufuatia ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika Umoja wa Mataifa ambapo alikuwa na mazungumzo na Wakuu mbalimbali wa UN. Akielezea tathmini yake ya miezi nane kama Kamanda wa UNAMID Jenerali Mella anasema njia pekee ya kupatikana kwa amani ya kudumu katika jimbo la Darfur ni kwa pande zinazopingana kukaa katika meza ya mazungumzo na kumaliza tofauti zao.

Na Mwandishi Maalum

Kamanda wa Jeshi la Mseto la Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa katika Darfur ( UNAMID) Luteni Jenerali Paul Mella, amesema, mazungumzo yatakayozihusisha pande zote zinazopingana katika mgogoro na machafuko yanayoendelea katika Jimbo la Darfur ndiyo suluhu pekee inayoweza kurejesha hali ya Amani, usalama na utulivu katika jimbo hilo.

Jenerali Mella, ameyasema hayo wakati alipokuwa akibadilishana mawazo na Balozi Ramadhani Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, wakati Jenerali Mella alipoutembelea Uwakilishi wa Kudumu.

Kamanda wa Jeshi la UNAMID alikuwa hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwa ziara ya kikazi ya siku tatu, ambapo alikutana na kufanya mazungumzo na Viongozi mbalimbali wa Umoja wa Mataifa.

“Katika kipindi changu za miezi nane sasa kama kamanda wa UNAMID yapo mambo mengi ambayo nimejifunza zikiwamo pia changamoto mbalimbali katika eneo zima la ulinzi wa Amani katika Jimbo la Darfur. Kubwa la msingi ambalo nimejifunza, ni kwamba, Amani ya kudumu haiwezi kurejea katika jimbo la Darfur kama pande zote zinazopingana hazitaweza kukaa katika meza moja na kufanya mazungumzo” anasema Jenerali Mella.

Na kuongeza “ kwa tathmini yangu , wanajeshi wanaounda UNAMID wapo pale kulinda Amani, kutoa ulinzi kwa wananchi na kusaidia usambazaji wa misaada ya kibinadamu. Lakini kwa kweli, hakuna Amani ya kulinda, kwa sababu moja kubwa, nayo ni kwamba pande zinazopingana hazijafikia makubaliano ya kusitisha mapigano na kurejea katika meza ya mazungumzo.”

Akielezea zaidi tathmini yake katika kipindi hicho ya miezi nane ambapo anaongoza zaidi ya walinzi wa Amani (wanajeshi)14,379 wanaounda UNAMID. Jenerali Mella, anaeleza kwamba, tangu achukue uongozi huo, kumekuwapo na mabadiliko katika mwenendo mzima wa mapigano katika jimbo hilo.

“ Changamoto kubwa niliyokumbana nayo ni kuwa katika miezi hiyo nane ya uongozi wangu, mwenendo mzima wa machafuko au mapingano umebadilika na kujikita zaidi katika mapigano ya kikabila” anabainisha na kuongeza.

“Mapigano hayo ya kikabili na ambayo chimbuko lake ni kugombea raslimali zikiwamo dhahabu mafuta na malisho, yamepelekea kuwapo kwa wimbi kubwa la wakimbizi wa ndani.

Jenerali Mella anasema, sehemu kubwa ya mapingano hiyo baina ya makabila yalikuwa yanatokea karibu na maeneo zilipo kambi zetu kwa maana ya wanajeshi kutoka Jeshi la wananchi wa Tanzania ( JWTZ). Ninafarijika sana kueleza kwamba wanajeshi wetu wameonyesha weledi na uhodari wa hali ya juu kwanza kwa kutoa ulinzi kwa raia waliokuwa wakikimbia machafuko na pili kuwapatia misaada ya kibinadamu zikiwamo huduma za afya”.

“Ni katika kipindi hicho cha mapigano ambapo licha ya utoaji wa huduma za kibinadamu kwa wakimbizi hao, walinzi wetu wa Amani ( JWTZ), walijikuta wakilazimika kutoa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito zaidi ya saba waliojifungua salama watoto wao katika kambi zetu”.

“ Huduma hii ya kuwasaidia akina mama wajawazito kujifungua salama watoto wao, kuliwafanya wazazi wale kuwapa watoto wao majina ya kitanzania kama shukrani yao kwa msaada na huduma nzuri waliyopatiwa na madaktari wa kitanzania katika kipindi hicho kigumu. Kuna watoto wenye majina ya kitanzania” anasema Jenerali Mella kwa furaha.

Kwa upande wake, Balozi Mwinyi ameshukuru Kamanda wa Jeshi la UNAMID kwa kutenga muda wake na kufika Uwakilishi wa Kudumu. Akashukuru pia kwa maelezo yake ya kina kuhusu hali ilivyo katika jimbo hilo la Darfur na mchango mzima wa walinzi wa Amani.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ina kikosi UNAMID kinacho kalia maeneo matatu ambayo ni Khor Abeche, Menawashe na Shangil Tobaya.

Tanzania inakuwa nchi ya tatu kongoza UNAMID , nchi nyingine ambazo zimewahi kuongoza ni Nigeria na Rwanda.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate