EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, April 23, 2014

NISHA: SIJAWAHI KUCHUKULIWA NA PEDESHEE

SALMA Jabu maarufu kama Nisha, ni mmoja wa waigizaji wanaofanya vizuri katika kiwanda cha filamu Tanzania. Amefanya kazi nyingi zinazomfanya kuwa mmoja wa mastaa wanaoongoza kwa kushiriki katika movie nyingi.

Salma Jabu 'Nisha'.
Risasi Mchanganyiko lilimtafuta na kufanya naye mahojiano maalum kuhusu mambo mbalimbali yanayohusiana na sanaa yake.
Risasi: Mambo vipi Nisha?
Nisha: Poa kabisa, niambie
Risasi: Unaizungumziaje sanaa yako kwa ujumla wake?
Nisha: Sanaa yangu ni safari ndefu sana na naamini ndiyo kwanza nipo robo yake.
Kuna mambo mengi magumu, mojawapo ni kupata vikwazo vya hapa na pale, pia wapo baadhi yetu wanapata labda skendo, badala ya kuwahukumu wenyewe, lakini tunachukuliwa kuwa wote ndivyo tulivyo jambo ambalo siyo kweli.
Mtu unatamani kuwa fulani, lakini unawekewa vikwazo kwa sababu tu ya ule msemo wa samaki mmoja akioza, basi wote wameoza.
Risasi: Vipi kuhusu soko la bidhaa zetu?
Nisha: Soko ni zuri sana, ni kujua tu mashabiki wako wanapenda nini basi.
Risasi: Unadaiwa wewe una fedha sana, kuna mtu yuko nyuma yako?
Nisha: Sina mtu nyuma yangu, pesa ni juhudi zako mwenyewe, kikubwa nafanya kazi kwa bidii, napenda sana kazi yangu, alhamdulilah sasa nimekuwa na kampuni yangu mwenyewe ya kuandaa filamu (Nisha’s film production).
Nisha katika pozi.
Kwa mfano nimeandaa filamu kama Tikisa, Pusi na Paku, Kashfa na Gumzo na zingine. Hiyo ndiyo siri ya hizo pesa wanazozitaja, napenda kuweka akiba kwa kufungua mradi, saluni yangu na duka la samani, ndiyo vinaendesha maisha ya kawaida ya nyumbani.
Risasi: Umri unaenda, vipi umeolewa?
Nisha: Nina mtu alhamdulilah, Inshaalah niombeeni dua, sijawahi sumbuliwa kwani mimi mapema nimeanza kujiajiri mwenyewe.
Risasi: Umejaaliwa kupata mtoto?
Nisha: Sina watoto ila napenda watoto, kila mtoto ni wangu inshaallah nataka kuanzisha familia, nasubiri Mwenyezi Mungu ajibu kwani kila kitu kimeandikwa na yeye, mimi siwezi jua lini, saa na wapi.
Risasi: Kuna maneno juu ya wasanii kujirahisisha kwa watu wenye fedha, wanaoitwa mapedeshee, unazungumziaje?
Nisha: Mimi sijawahi kuwa na pedeshee wala simuhitaji, nakuwa na mtu kwa mapenzi ya kweli, awe maskini au tajiri ilimradi moyo wangu umempenda, kikubwa tabia na maelewano na anipende kwa dhati.
Risasi: Unafikiri kwa nini baadhi ya wasanii na wasichana wengine wanaamua kujiuza?
Nisha: Wengine wanashindwa kujiajiri kwa kukosa mtaji (kwa wasiokuwa nao nawaombea wapate) wanaojiuza ni tamaa,
kutojitambua na kukosa malengo, mimi nina malengo na siku moja niwe mfano kama Oprah Winfrey na kadhalika, sijaridhika kwa nikipatacho, nafanya kazi kwa bidii ili kupata zaidi Inshaalah.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate