EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, April 2, 2014

YONDANI, KASEJA WATAJWA FEDHA ZA AZAM

Kipa wa Yanga, Juma Kaseja.
Na Sweetbert Lukonge
HALI si shwari Yanga, wachezaji wa timu hiyo, kipa Juma Kaseja na beki wake, Kelvin Yondani wamekalia kuti kavu ndani ya klabu hiyo na huenda wakatimuliwa baada ya kutuhumiwa kuihujumu katika mechi yake ya Ligi Kuu Bara dhidi ya JKT Mgambo kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, wikiendi iliyopita.
Wachezaji hao wanadaiwa kupokea mamilioni ya fedha kutoka Azam ili wacheze chini ya kiwango.
 
Beki wa Yanga, Kelvin Yondani.
Katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani, Yanga ilitandikwa mabao 2-1 ambayo yanadaiwa yalitokana na uzembe uliofanywa na wachezaji hao na kuiweka timu hiyo kwenye mazingira magumu ya kutetea ubingwa wake.

Habari za uhakika ambazo Championi Jumatano limezipata kutoka ndani ya Yanga, zimedai kuwa hivi sasa uongozi wa timu hiyo unawafanyia uchunguzi Kaseja na Yondani ili kujiridhisha kama kweli walichukua mamilioni hayo ya Azam.
Imedaiwa kuwa endapo itabaini kuwa ni kweli walipokea mamilioni hayo ili wacheze chini ya kiwango na kuifungisha timu hiyo katika mechi hiyo, basi watachukuliwa hatua kali za kinidhamu ambazo hazijawahi kutokea katika klabu hiyo tangu kuanzishwa kwake.

“Kaseja na Yondani ndiyo watuhumiwa wakuu wa tuhuma hizo na wanachukiwa vibaya sana hivi sasa na viongozi kwani hata baada ya mechi walikuwa na wakati mgumu, walisemwa sana huku wakituhumiwa kupokea hongo kutoka Azam ili wacheze chini ya kiwango.
“Hata hivyo uongozi hivi sasa upo katika uchunguzi kabambe juu ya jambo hilo na endapo itabainika kuwa ni kweli walichukua fedha kutoka Azam, watachukuliwa hatua kali za kinidhamu kama viongozi wanavyodai lakini siwezi jua ni adhabu gani,” alisema mtoa habari huyo ambaye yupo ndani ya klabu hiyo.  
Alisema jambo ambao linawauma zaidi viongozi wote wa klabu hiyo ni kupoteza mchezo huo dhidi ya JKT Mgambo ambao umewaweka katika mazingira magumu ya kutetea ubingwa wao wa ligi kuu kutokana na kuwa nyuma kwa tofauti ya pointi saba na wapinzani wao Azam ambao wanaongoza msimamo wa ligi hiyo.
Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, hakuwa tayari kuzungumza lolote juu ya tuhuma hizo wanazopewa wachezaji hao na kumtupia mpira ofisa habari wake, Baraka Kizuguto ambaye alisema:
“Taarifa za Yanga zinatolewa na uongozi kama ulivyofanya wakati ukitoa adhabu kwa kiungo wa timu hiyoAthuman Idd ‘Chuji’, hivyo kama tuhuma hizo ni kweli basi uongozi utatoa taarifa na siyo mtu mwingine.”
Katika mchezo huo Kaseja alipiga mpira kizembe ambao alirudishiwa na Yondani na kunaswa na Fully Maganga ambaye alitupia bao la kwanza la timu yake wavuni.
Yondani analaumiwa kuwa alicheza rafu ya kizembe ambayo ilisababisha penalti iliyopigwa na Balimi Basungu.
Matokeo haya yameiweka Yanga kwenye hali ngumu ya kutwaa ubingwa msimu huu kwani kwa sasa ina pointi 46 zikiwa ni saba nyuma ya Azam iliyopo kileleni na pointi 53.
 
Chanzo: Championi Jumatano

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate