EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, May 1, 2014

UNDANI VIFO VYA WATOTO 3 NDANI YA BWANA INASIKITISHA!

KUFUATIA vifo vya watoto watatu waliokufa kwa pamoja ndani ya bwawa la kuogelea ‘swimming pool’ kwenye Hoteli ya Landmark, Mbezi Beach jijini Dar, undani  wa vifo hivyo umejulikana, Amani lina kisa kamili.
Mmoja kati ya marehemu aliyepatwa na janga hilo.
CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo chetu, watoto walionusurika kufa ambao  walikuwa wakisherehekea siku ya kuzaliwa ya mwenzao ‘bethidei’ aliyejulikana kwa jina la Derrick Mboka, waliwaona marehemu wakielea kwenye maji ya bwawa hilo walilosema kuwa ni la kuogelea watu wazima.

Chanzo kiliendelea kuweka wazi kwamba baada ya kuwaona wenzao wakielea, watoto hao walipiga kelele jambo lililowashtua walinzi wa hoteli hiyo upande wa bwawa ambao walifika haraka kuwatoa marehemu wakiwa tayari wameshafariki dunia huku mtoto mmoja akihangaika kujiokoa.
Wanafunzi wakiomboleza kifo cha mwenzao.
“Unajua wale watoto sijui nisemeje? Waliingia mle kwenye bwawa, inaonekana walizama, hakuna aliyeweza kuja juu, maji yaliwazidi. Walipokata roho ndipo miili ikaibuka na kuelea, ndipo wenzao wakapiga kelele,” kilisema chanzo kwa masikitiko makubwa.

UZEMBE WATAJWA
Habari zaidi zinadai kuwa sababu kubwa iliyosababisha vifo vya watoto wote watatu ni uzembe uliofanywa na walinzi wa bwawa hilo ambao walidaiwa kutokuwa makini kuwadhibiti watoto wengi waliokuwa wakiogelea karibu na bwawa la watu wazima kiasi cha kutoka na kuingia huko.

Mmoja kati ya waombolezaji akilia kwa uchungu.
MAMA WA MTOTO MWENYE BETHIDEI ATUPIWA LAWAMA
Uzembe mwingine ulitajwa kufanywa na mama wa mtoto aliyekuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa aliyetajwa kwa jina la Anita Mboka kwa kuwachukua watoto wasio wake na kuondoka nao bila kutoa taarifa kwa wazazi wao japo kuwa mama wa marehemu Janeth Zakaria (9), Devotha Mbutwa alikiri kupokea taarifa kuwa mwanaye anakwenda kwenye bethidei ya mwenzake beach (baharini).

Inadaiwa mama huyo alipinga mwanaye kwenda kuogelea baharini, lakini alipoambiwa ni hotelini alikubali bila kujua kuwa nako walikuwa wakienda kupiga mbizi kwenye bwawa na baadaye kupewa taarifa za kifo chake. Marehemu alizikwa jana, Iringa Vijijini.
TAARIFA ZA MTOTO WA PILI
Kwa upande wao, ndugu wa karibu wa marehemu Ndimbumi Bahati (9) walisema hawakupata taarifa yoyote kuhusiana na mzazi huyo kumchukua mtoto huyo, wakadai siku ya tukio, marehemu alipelekwa na baba yake kula chipsi jirani na alipomaliza, baba aliondoka akimuahidi kuwa atakaporejea angemchukua kumpeleka matembezini, lakini jioni akapata taarifa amefariki dunia.
Marehemu alizikwa jana jijini Mbeya.

KUHUSU MTOTO WA TATU
Nao ndugu wa mtoto marehemu Eva Nicholaus (11) hawakupatikana mara moja kwa kuwa hadi gazeti hili linaelekea mtamboni hakukuwa na msemaji rasmi wa familia hiyo ambayo  msiba wake ulikuwa Kijitonyama-Mpakani, Dar. Alizikwa jana Makaburi ya Sinza jijini Dar.

WAZAZI WAVIPOKEA VIFO KWA MTAZAMO TOFAUTI
Inadaiwa baada ya vifo vya watoto hao wa mtaa mmoja, kuna wazazi  walivipokea vifo hivyo kwa mtazamo tofauti ambapo kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa familia ya Ndimbumi, baba wa mtoto huyo, Bahati Sisala alikuwa amechanganyikiwa kiasi cha kupoteza fahamu kwa siku nzima.

Naye mama mzazi wa mtoto Janeth, Devotha yeye alionekana kuzidi kudhoofu hali yake kwa kuwa alizipokea taarifa za kifo cha mwanaye akiwa anaumwa (ugonjwa haikujulikana).
KIJITONYAMA YAZIZIMA
Waandishi wetu walishuhudia wakazi wa Kijitonyama mahali walipokuwa wakiishi watoto hao wakiwa katika majonzi makubwa ambapo umati uligawanyika kuaga watoto hao.

Msiba wa marehemu Ndimbumi uliagwa nyumbani Kijitonyama huku mwili wa mtoto Janeth ukiagwa katika Hospitali ya Mkoa Kutabibu Kinondoni, Mwananyamala kabla ya miili hiyo kusafirishwa mmoja kuelekea Mbeya na mwingine mkoani Iringa.
WANAFUNZI WAMLILIA MWENZAO MSIBANI
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kijitonyama ambao walikuwa wakisoma na Ndimbumi walifika katika msiba huo na kusikitisha waombolezaji waliohudhuria msibani hapo baada ya kuangua vilio jambo lililoongeza simanzi. Marehemu alikuwa akisoma darasa la nne.

MWENYEKITI, AFISA ELIMU NA KIONGOZI WA DINI WANENA
Kwa upande mwingine Mwenyekiti wa Mtaa wa Kijitonyama, Alhaus Magoha alisema amesikitishwa sana na vifo hivyo vilivyotokea ndani ya mtaa wake na kuongeza kuwa hilo ni pigo kubwa.

Naye Afisa Elimu wa Kijitonyama, Alexandrina Kahando na Katekista wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Maximilian Kolbe, Mwenge jijini Dar, John Adolf walifika msibani hapo kuwafariji wazazi wa mtoto Ndimbumi ambao walikuwa wameishiwa nguvu kutokana na kumpoteza mtoto wao mpendwa.
HOTELI YAGHARAMIA USAFIRI
Habari zilizopatikana wakati gazeti hili linakwenda mitamboni zilisema kuwa, uongozi wa Hoteli ya Landmark ndiyo uliojitolea kubeba jukumu la kuisafirisha miili ya Ndimbumi na Janet.
Juzi waandishi wetu walifika kwenye hoteli hiyo kwa lengo ka kuzungumza na uongozi lakini waliambiwa kuwa viongozi wote walikuwa kwenye vikao.

Stori: Chande Abdallah, Shani Ramadhani, Denis Mtima na Mayasa Mariwata.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate